Isaya 47:1-15

  • Kuanguka kwa Babiloni (1-15)

    • Wanajimu wafunuliwa (13-15)

47  Shuka uje uketi mavumbini,Ewe binti ya Babiloni uliye bikira.+ Keti ardhini ambapo hakuna kiti cha ufalme,+Ewe binti ya Wakaldayo,Kwa maana watu hawatakuita tena wewe mwororo na aliyedekezwa.   Chukua jiwe la kusagia na usage unga. Vua shela yako. Vua rinda lako, funua miguu yako. Vuka mito.   Uchi wako utafunuliwa. Aibu yako itaonekana. Nitalipiza kisasi,+ na hakuna mtu atakayenizuia.*   “Yule anayetukomboa—Yehova wa majeshi ndilo jina lake—Ndiye Mtakatifu wa Israeli.”+   Keti hapo kimya na uingie gizani,Ewe binti ya Wakaldayo;+Hawatakuita tena Bimkubwa* wa Falme.+   Nilikuwa na ghadhabu kuwaelekea watu wangu.+ Niliutia unajisi urithi wangu,+Nami nikawatia mkononi mwako.+ Lakini hukuwaonyesha rehema.+ Hata juu ya wazee uliweka nira nzito.+   Ulisema: “Sikuzote nitakuwa Bimkubwa,* milele.”+ Hukutia mambo haya moyoni mwako;Hukufikiria mwisho wa jambo hilo.   Sasa sikia jambo hili, ewe mpenda raha,+Unayeketi kwa usalama, unayesema moyoni mwako: “Mimi ndiye, na hakuna mwingine.+ Sitakuwa mjane. Sitajua kamwe inavyokuwa kupoteza watoto.”+   Lakini mambo haya mawili yatakupata ghafla, kwa siku moja:+ Kupoteza watoto na ujane. Yatakupata kwa kipimo kamili+Kwa sababu ya* ulozi wako mwingi na uchawi wako wenye nguvu.+ 10  Uliutumaini uovu wako. Ulisema: “Hakuna anayeniona.” Hekima na ujuzi wako ndivyo vilivyokupotosha,Nawe unasema moyoni mwako: “Mimi ndiye, na hakuna mwingine.” 11  Lakini utapatwa na msiba,Na hakuna hirizi yako yoyote itakayouzuia.* Utapatwa na shida; nawe hutaweza kuizuia. Utakumbwa na uharibifu wa ghafla ambao hujawahi kamwe kuona.+ 12  Basi, endelea kufanya uchawi na ulozi wako mwingi,+Ambao umeutaabikia tangu ujana wako. Labda utafaidika;Labda utawatisha watu. 13  Umechoka kwa wingi wa washauri wako. Na wasimame sasa na kukuokoa,Wale wanaoabudu mbingu,* wanaotazama nyota,+Wale wanaotoa ujuzi wakati wa miezi mipyaKuhusu mambo yatakayokupata. 14  Tazameni! Wao ni kama majani makavu. Moto utawateketeza kabisa. Hawawezi kujiokoa* kutoka kwenye nguvu za mwali wa moto. Hawa si makaa ya kujipasha moto,Na huu si moto wa kuota. 15  Ndivyo wachawi wako watakavyokuwa kwako,Wale ambao ulitaabika nao tangu ujana wako. Watatangatanga, kila mmoja kuelekea upande wake.* Hakutakuwa na yeyote wa kukuokoa.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “sitakutana na yeyote kwa fadhili.”
Au “Malkia.”
Au “Malkia.”
Au labda, “Licha ya.”
Au “Nawe hutajua jinsi ya kuuzuia kwa hirizi.”
Au labda, “Wale wanaozigawa mbingu; Wanajimu.”
Au “kuziokoa nafsi zao.”
Tnn., “kuelekea eneo lake.”