Isaya 49:1-26

  • Kazi ya mtumishi wa Yehova (1-12)

    • Nuru ya mataifa (6)

  • Faraja kwa Waisraeli (13-26)

49  Nisikilizeni, enyi visiwa,Kazeni fikira, enyi mataifa yaliyo mbali.+ Yehova aliniita kabla sijazaliwa.*+ Tangu nilipokuwa katika tumbo la mama yangu amelitaja jina langu.   Alikifanya kinywa changu kuwa kama upanga mkali;Amenificha katika kivuli cha mkono wake.+ Alinifanya kuwa mshale uliosuguliwa;*Alinisitiri katika podo lake.   Aliniambia: “Wewe ni mtumishi wangu, Ee Israeli,+Ambaye kupitia kwake nitaonyesha fahari yangu.”+   Lakini nilisema: “Nimejitaabisha bure. Nilitumia nguvu zangu kwa ajili ya jambo lisilo halisi, kwa ubatili. Lakini kwa hakika hukumu yangu iko na Yehova,*Na malipo yangu yako* na Mungu wangu.”+   Na sasa Yehova, Yule aliyeniumba tangu tumboni niwe mtumishi wake,Amesema kwamba nimrudishe Yakobo kwake,Ili watu wa Israeli wakusanyike kwake.+ Nitatukuzwa machoni pa Yehova,Na Mungu wangu tayari atakuwa nguvu zangu.   Naye akasema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wanguIli kuyainua makabila ya YakoboNa kuwarudisha wale waliohifadhiwa wa Israeli. Nimekutoa pia ili uwe nuru ya mataifa,+Ili wokovu wangu ufike kwenye miisho ya dunia.”+  Yehova, Mkombozi wa Israeli, Mtakatifu wake,+ anamwambia hivi yule anayedharauliwa,+ yule anayechukiwa na taifa, mtumishi wa watawala: “Wafalme wataona na kusimama,Na wakuu watainama chiniKwa sababu ya Yehova, ambaye ni mwaminifu,+Mtakatifu wa Israeli, ambaye amekuchagua.”+   Yehova anasema hivi: “Wakati wa kibali* nilikujibu,+Na katika siku ya wokovu nilikusaidia;+Niliendelea kukulinda ili nikutoe uwe agano kwa ajili ya watu,+Ili kuitengeneza upya nchi,Ili kuwafanya wamiliki urithi wao ulio ukiwa,+   Ili kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni nje!’+ Na wale walio gizani,+ ‘Tokeni nje mwonekane!’ Watalisha kando ya barabara,Malisho yao yatakuwa kando ya njia zilizokanyagwa.* 10  Hawatakuwa na njaa, wala hawatakuwa na kiu,+Wala joto kali wala jua halitawachoma.+ Kwa maana Yule anayewaonyesha rehema atawaongoza,+Naye atawaongoza kando ya chemchemi za maji.+ 11  Nitaifanya milima yangu yote kuwa barabara,Na barabara zangu kuu zitainuliwa.+ 12  Tazameni! Hawa wanakuja kutoka mbali sana,+Na tazameni! hawa wanatoka kaskazini na kutoka magharibi,Na hawa kutoka nchi ya Sinimu.”+ 13  Pigeni vigelegele vya shangwe, enyi mbingu, na ushangilie, Ee dunia.+ Milima na ichangamke kwa kilio cha shangwe.+ Kwa maana Yehova amewafariji watu wake,+Naye huwaonyesha rehema watu wake mwenyewe wanaoteseka.+ 14  Lakini Sayuni aliendelea kusema: “Yehova ameniacha,+ na Yehova amenisahau.”+ 15  Je, mwanamke anaweza kumsahau mtoto wake anayenyonyaAu asimhurumie mwana wa tumbo lake? Hata wanawake hawa wakisahau, mimi siwezi kamwe kukusahau.+ 16  Tazama! Nimekuchonga kwenye viganja vyangu. Kuta zako ziko mbele zangu daima. 17  Wana wako wanarudi haraka. Wale waliokubomoa na kukuharibu wataondoka kwako. 18  Inua macho yako utazame pande zote. Wote wanakusanyika pamoja.+ Wanakuja kwako. “Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova,“Utajivika hao wote kana kwamba ni mapambo,Nawe utajifunga watu hao kama bibi harusi anavyofanya. 19  Ingawa maeneo yako yaliharibiwa na kuwa ukiwa na nchi yako ikawa magofu,+Sasa itakuwa ndogo sana kwa wale wanaokaa humo,+Na wale waliokumeza+ watakuwa mbali sana.+ 20  Wana waliozaliwa ulipokuwa umefiwa watasema hivi ukisikia,‘Mahali hapa ni padogo sana kwangu. Nipeni nafasi zaidi hapa nikae.’+ 21  Nawe utasema moyoni mwako,‘Ni baba gani aliyenizalia watoto hawa,Kwa kuwa mimi ni mwanamke niliyefiwa na watoto, nami ni tasa,Nami nilipelekwa uhamishoni na kufungwa? Ni nani aliyewalea hawa?+ Tazameni! Nilibaki peke yangu,+Sasa hawa wametoka wapi?’”+ 22  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazameni! Nitayainulia mataifa mkono wangu,Nami nitawainulia watu ishara yangu.*+ Watawaleta wana wako wakiwa wamewabeba mikononi mwao*Na kuwabeba mabinti wako kwenye mabega yao.+ 23  Wafalme watakuwa watunzaji wako,+Na mabinti wao wa kifalme watakuwa walezi wako. Watakuinamia kifudifudi+Na kuyaramba mavumbi ya miguu yako,+Nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova;Wale wanaonitumaini hawataaibika.”+ 24  Je, wale waliotekwa wanaweza kuchukuliwa kutoka kwa mtu mwenye nguvu,Au, je, mateka wa mtu mkatili wanaweza kuokolewa? 25  Lakini Yehova anasema hivi: “Hata mateka wa mtu mwenye nguvu watachukuliwa,+Na wale waliotekwa na mtu mkatili wataokolewa.+ Nitawapinga wale wanaokupinga,+Nami nitawaokoa wana wako mwenyewe. 26  Nitawafanya wale wanaokutesa wale nyama yao wenyewe,Nao watalewa kwa damu yao wenyewe kana kwamba ni kwa divai tamu. Na watu wote* watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+Mwokozi wako+ na Mkombozi wako,+Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoka katika tumbo la uzazi.”
Au “uliong’arishwa.”
Au “Yehova atanitendea kwa haki.”
Au “thawabu yangu iko.”
Au “nia njema.”
Au labda, “vilima visivyo na kitu.”
Au “nguzo yangu ya ishara.”
Tnn., “kifuani.”
Tnn., “wote wenye mwili.”