Isaya 5:1-30

  • Wimbo kuhusu shamba la Yehova la mizabibu (1-7)

  • Ole kwa shamba la Yehova la mizabibu (8-24)

  • Hasira ya Mungu dhidi ya watu wake (25-30)

5  Tafadhali, acha nimwimbie mpenzi wanguWimbo kuhusu mpenzi wangu na shamba lake la mizabibu.+ Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu kwenye kilima kinachozaa sana.   Akalilima na kuondoa mawe ndani yake. Akapanda mzabibu bora mwekundu,Akajenga mnara katikati yake,Naye akachimba shinikizo la divai ndani yake.+ Kisha akaendelea kutumaini kwamba litazaa zabibu,Lakini lilizaa zabibu za mwituni peke yake.+   “Na sasa, enyi wakaaji wa Yerusalemu na watu wa Yuda,Tafadhali hukumuni kati yangu na shamba langu la mizabibu.+   Ningelifanyia nini kingine shamba langu la mizabibuAmbacho bado sijafanya?+ Kwa nini, nilipotumaini kwamba litazaa zabibu,Lilizaa zabibu za mwituni peke yake?   Sasa, tafadhali, acheni niwaambieKile nitakacholifanyia shamba langu la mizabibu: Nitaondoa uzio wake,Nalo litateketezwa kabisa.+ Nitaubomoa ukuta wake wa mawe,Nalo litakanyagwa-kanyagwa.   Nami nitalifanya liwe ukiwa;+Halitapunguzwa matawi wala kulimwa. Litamea vichaka vya miiba na magugu,+Nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua yoyote juu yake.+   Kwa maana shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli;+Watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda sana. Aliendelea kutumaini haki itendwe,+Lakini tazama! kulikuwa na ukosefu wa haki;Alitumaini uadilifu ufanywe,Lakini tazama! kulikuwa na kilio cha huzuni.”+   Ole wao wanaounganisha nyumba moja na nyingine+Na wanaounganisha shamba moja na lingine+Mpaka nafasi inapokosekana kabisaNanyi mnaishi peke yenu nchini!   Yehova wa majeshi ameapa masikioni mwanguKwamba nyumba nyingi, ingawa ni kubwa na maridadi,Zitakuwa kitu cha kutisha,Bila mkaaji.+ 10  Kwa maana ekari kumi za* shamba la mizabibu zitazaa kipimo kimoja tu cha bathi,*Na kipimo kimoja cha homeri* ya mbegu kitazaa efa* moja tu.+ 11  Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili wanywe kileo,+Wanaokawia hadi giza linapoingia jioni mpaka divai inapowawasha! 12  Wana kinubi na kinanda,Tari, filimbi, na divai katika karamu zao;Lakini hawafikirii utendaji wa Yehova,Wala hawaioni kazi ya mikono yake. 13  Kwa hiyo watu wangu wataenda uhamishoniKwa sababu ya kukosa ujuzi;+Wanaume wao wenye utukufu watakuwa na njaa,+Na watu wao wote watakauka kwa kiu. 14  Kwa hiyo Kaburi* limejipanua*Nalo limefungua kinywa chake bila kikomo;+Na fahari yake,* umati wake wenye kelele, na watu wake wanaosherehekeaHakika watashuka na kuingia ndani yake. 15  Na mwanadamu atainama,Mwanadamu atashushwa,Na macho ya wenye majivuno yatashushwa. 16  Yehova wa majeshi atakwezwa kupitia hukumu yake;*Mungu wa kweli, Aliye Mtakatifu,+ atajitakasa mwenyewe kupitia uadilifu.+ 17  Na wanakondoo watalisha kama katika malisho yao;Wakaaji wageni watakula katika maeneo yenye ukiwa ya wanyama waliolishwa vizuri. 18  Ole wao wanaokokota hatia yao kwa kamba za udanganyifuNa dhambi yao kwa kamba za gari la kukokotwa; 19  Wale wanaosema: “Na aharakishe kazi yake;Na ije upesi ili tuione. Kusudi la* Mtakatifu wa Israeli na litimizweIli tulijue!”+ 20  Ole wao wanaosema kwamba wema ni uovu na uovu ni wema,+Wale wanaoweka giza badala ya nuru na nuru badala ya giza,Wale wanaoweka uchungu badala ya utamu na utamu badala ya uchungu! 21  Ole wao walio na hekima katika macho yao wenyeweNa walio na busara machoni pao wenyewe!+ 22  Ole wao walio hodari katika kunywa divaiNa wanaume walio stadi katika kuchanganya vileo,+ 23  Wale wanaomwondolea mwovu hatia kwa rushwa+Na wanaomnyima haki mwadilifu!+ 24  Kwa hiyo, kama mwali wa moto unavyoteketeza majani makavuNa majani makavu yanavyonyauka katika moto,Mizizi yao wenyewe itaoza,Na maua yao yatatawanyika kama ungaunga,Kwa sababu walikataa sheria* ya Yehova wa majeshi,Na kulidharau neno la Mtakatifu wa Israeli.+ 25  Ndiyo sababu hasira ya Yehova inawaka dhidi ya watu wake,Naye ataunyoosha mkono wake dhidi yao na kuwapiga.+ Milima itatetemeka,Na maiti zao zitakuwa kama takataka barabarani.+ Kwa sababu ya hayo yote, hasira yake haijapoa,Lakini mkono wake bado umenyooshwa ili kupiga. 26  Ameliinulia ishara* taifa lililo mbali;+Amewapigia mluzi waje kutoka miisho ya dunia;+Na tazama! wanakuja upesi sana.+ 27  Hakuna yeyote kati yao aliyechoka wala kujikwaa. Hakuna yeyote anayesinzia au kulala. Mshipi ulio kwenye kiuno chao haujalegezwa,Wala kamba za viatu vyao hazijakatika. 28  Mishale yao yote ni mikali,Na pinde zao zote zimepindika.* Kwato za farasi wao ni kama jiwe gumu lenye makali,Na magurudumu yao kama upepo wa dhoruba.+ 29  Mngurumo wao ni kama wa simba;Wananguruma kama wanasimba.*+ Watanguruma na kukamata mawindoNa kuyabeba bila mtu wa kuyaokoa. 30  Siku hiyo watanguruma juu yakeKama mngurumo wa bahari.+ Mtu yeyote anayeitazama nchi ataona giza lenye kutaabisha;Hata nuru imetiwa giza kwa sababu ya mawingu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “viganja kumi vya”
Au “wakuu wake.”
Au “limepanua nafsi yake.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “haki yake.”
Au “Uamuzi wa; Shauri la.”
Au “mafundisho.”
Au “nguzo ya ishara.”
Au “ziko tayari kupiga mshale.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”