Isaya 50:1-11

  • Dhambi za Waisraeli zasababisha matatizo (1-3)

  • Mtumishi mtiifu wa Yehova (4-11)

    • Ulimi na sikio la waliofundishwa (4)

50  Yehova anasema hivi: “Kiko wapi cheti cha talaka+ cha mama yenu, ambaye nilimfukuza? Au niliwauza kwa yupi kati ya wakopeshaji wangu? Tazameni! Mliuzwa kwa sababu ya uovu wenu,+Na mama yenu alifukuzwa kwa sababu ya makosa yenu wenyewe.+   Basi, kwa nini nilipokuja, hapakuwa na mtu yeyote mahali hapa? Kwa nini hakuna aliyejibu nilipoita?+ Je, mkono wangu ni mfupi usiweze kukomboa,Au je, sina nguvu za kuokoa?+ Tazameni! Mimi huikausha bahari kwa kemeo langu;+Ninaifanya mito kuwa jangwa.+ Samaki waliomo huoza kwa kukosa maji,Nao hufa kwa sababu ya kiu.   Mimi hulivisha mbingu giza,+Nami huzifunika kwa nguo za magunia.”   Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenipa ulimi wa waliofundishwa,*+Ili nijue jinsi ya kumjibu* aliyechoka kwa neno linalofaa.*+ Yeye huniamsha asubuhi baada ya asubuhi;Huliamsha sikio langu ili lisikilize kama wale waliofundishwa.+   Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amelifungua sikio langu,Nami sikuwa mwasi.+ Sikugeuka upande ulio kinyume.+   Niliwapa mgongo wangu wale waliokuwa wakinipigaNa mashavu yangu wale waliozing’oa ndevu zangu. Sikuuficha uso wangu kutoka kwa mambo yenye kufedhehesha na kutoka kwa mate.+   Lakini Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atanisaidia.+ Ndiyo sababu sitafedheheka. Ndiyo sababu nimeufanya uso wangu uwe kama jiwe gumu,+Nami ninajua kwamba sitaaibika.   Yule anayenitangaza kuwa mwadilifu yu karibu. Ni nani anayeweza kunishtaki?*+ Na tusimame pamoja.* Ni nani aliye na kesi dhidi yangu? Na anikaribie.   Tazameni! Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atanisaidia. Ni nani atakayenitangaza kuwa na hatia? Tazameni! Wote watachakaa kama vazi. Nondo* atawala. 10  Ni nani kati yenu anayemwogopa YehovaNa kusikiliza sauti ya mtumishi wake?+ Ambaye ametembea katika giza zito, bila mwangaza wowote? Na alitumaini jina la Yehova na kujitegemeza juu ya* Mungu wake. 11  “Tazameni! Ninyi nyote mnaowasha moto,Mnaorusha cheche,Tembeeni katika nuru ya moto wenu,Kati ya cheche ambazo mmewasha. Hili ndilo mtakalopata kutoka mkononi mwangu: Mtalala kwa maumivu makali.

Maelezo ya Chini

Au labda, “kumwimarisha.”
Tnn., “kwa neno.”
Au “ulimi uliozoezwa vizuri.”
Au “kushindana nami?”
Au “tutazamane.”
Aina fulani ya mdudu mharibifu.
Au “kumtegemea.”