Isaya 51:1-23

  • Sayuni larudishwa kuwa kama bustani ya Edeni (1-8)

  • Faraja kutoka kwa Muumba wa Sayuni mwenye nguvu (9-16)

  • Kikombe cha ghadhabu ya Yehova (17-23)

51  “Nisikilizeni mimi, ninyi mnaofuatia uadilifu,Ninyi mnaomtafuta Yehova. Uangalieni mwamba ambao mlichongwa kutoka kwakeNa machimbo ambamo mlichimbwa kutoka ndani yake.   Mwangalieni Abrahamu baba yenuNa Sara+ aliyewazaa.* Kwa maana Abrahamu alikuwa mmoja tu nilipomwita,+Nami nilimbariki na kumfanya kuwa wengi.+   Kwa maana Yehova atalifariji Sayuni.+ Ataleta faraja kwa magofu yake yote,+Naye ataifanya nyika yake kuwa kama Edeni+Na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.+ Kutakuwa na furaha na shangwe ndani yake,Kutoa shukrani na nyimbo tamu.+   Nisikilizeni, enyi watu wangu,Na mnitegee sikio, taifa langu.+ Kwa maana sheria itatoka kwangu,+Nami nitaifanya haki yangu kuwa nuru kwa watu.+   Uadilifu wangu unakaribia.+ Wokovu wangu utatoka,+Na mikono yangu itayahukumu mataifa.+ Visiwa vitanitumaini mimi,+Navyo vitaungojea mkono wangu.*   Inueni macho yenu mbinguni,Na mtazame chini duniani. Kwa maana mbingu zitatawanyika vipandevipande kama moshi;Nayo dunia itachakaa kama vazi,Na wakaaji wake watakufa kama mbu.* Lakini wokovu wangu utadumu milele,+Na uadilifu wangu hautashindwa kamwe.*+   Nisikilizeni mimi, ninyi mnaoujua uadilifu,Watu walio na sheria* yangu moyoni mwao.+ Msiogope dhihaka za wanadamu wanaoweza kufa,Na msiogopeshwe na matusi yao.   Kwa maana nondo atawala kabisa kama vazi;Nondo* alaye nguo atawala kabisa kama sufu.+ Lakini uadilifu wangu utadumu milele,Na wokovu wangu kwa vizazi vyote.”+   Amka! Amka! Jivike nguvu,Ee mkono wa Yehova!+ Amka kama katika siku za zamani za kale, kama katika vizazi vilivyopita. Je, si wewe uliyemvunja Rahabu*+ vipandevipande,Uliyemchoma kwa silaha yule mnyama mkubwa sana wa baharini?+ 10  Je, si wewe uliyeikausha bahari, maji ya kilindi kikubwa?+ Uliyevifanya vilindi vya bahari kuwa njia ili watu waliokombolewa wavuke?+ 11  Watu wa Yehova waliokombolewa watarudi.+ Watakuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe,+Na shangwe isiyokoma itakuwa taji lao.*+ Watakuwa na furaha na shangwe. Huzuni na kilio cha uchungu vitakimbia.+ 12  “Mimi mwenyewe Ndiye ninayewafariji.+ Kwa nini umwogope mwanadamu anayeweza kufa ambaye atakufa+Na mwana wa binadamu atakayenyauka kama majani mabichi? 13  Kwa nini unamsahau Yehova Muumba wako,+Yule aliyezitandaza mbingu+ na kuweka msingi wa dunia? Mchana kutwa uliendelea kuhofu ghadhabu ya mkandamizaji,*Kana kwamba angeweza kukuangamiza. Iko wapi sasa ghadhabu ya mkandamizaji? 14  Yule aliyejikunja katika minyororo atawekwa huru hivi karibuni;+Hatakufa na kuingia shimoni,Wala hatakosa mkate. 15  Lakini mimi ni Yehova Mungu wako,Ninayeitibua bahari na kuyavuruga mawimbi yake+—Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+ 16  Nitayaweka maneno yangu katika kinywa chako,Nami nitakufunika kwa kivuli cha mkono wangu,+Ili kuzipanda mbingu na kuuweka msingi wa dunia+Na kuwaambia watu wa Sayuni, ‘Ninyi ni watu wangu.’+ 17  Amka! Amka! Simama, Ee Yerusalemu,+Wewe ambaye umekunywa kutoka mkononi mwa Yehova kikombe chake cha ghadhabu. Umekunywa bilauri;Umemaliza kabisa kikombe kinachofanya watu wapepesuke.+ 18  Kati ya wana wote aliowazaa hakuna hata mmoja aliye hapo ili kumwongoza,Na kati ya wana wote aliowalea hakuna hata mmoja ambaye anamshika mkono. 19  Mambo hayo mawili yamekupata. Ni nani atakayekusikitikia? Maangamizi na uharibifu, njaa na upanga!+ Ni nani atakayekufariji?+ 20  Wana wako wamezimia.+ Wanalala chini katika kila pembe ya barabaraKama kondoo mwitu katika wavu. Wamejaa ghadhabu ya Yehova, kemeo la Mungu wako.” 21  Kwa hiyo tafadhali sikiliza jambo hili,Ewe mwanamke uliyeteseka na kulewa, lakini si kwa divai. 22  Bwana wako Yehova, Mungu wako anayewatetea watu wake anasema hivi: “Tazama! Nitakichukua kutoka mkononi mwako kile kikombe kinachofanya watu wapepesuke,+Ile bilauri, kikombe changu cha ghadhabu;Hutakinywa tena.+ 23  Nitakitia mkononi mwa wale wanaokutesa,+Wale waliokuambia, ‘Inama chini ili tutembee juu yako!’ Basi ukaufanya mgongo wako kama ardhi,Kama barabara yao ya kutembea juu yake.”

Maelezo ya Chini

Au “aliyewazaa kwa uchungu wa kuzaa.”
Au “vitangojea nguvu zangu.”
Aina ya mbu anayeitwa hak·kin·namʹ katika Kiebrania.
Au “hautavunjwa.”
Au “mafundisho.”
Au labda, “Mnyoo.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “juu ya vichwa vyao.”
Au “yule anayekubana.”