Isaya 52:1-15

  • Amka, Ee Sayuni! (1-12)

    • Miguu ya wale wanaoleta habari njema inapendeza (7)

    • Walinzi wa Sayuni wapaza sauti kwa pamoja (8)

    • Wale wanaobeba vyombo vya Yehova lazima wawe safi (11)

  • Mtumishi wa Yehova atakwezwa (13-15)

    • Sura iliyoharibika (14)

52  Amka! Amka! Jivike nguvu,+ ewe Sayuni!+ Vaa mavazi yako maridadi,+ ewe Yerusalemu, jiji takatifu! Kwa maana mtu ambaye hajatahiriwa na mtu asiye safi hawataingia ndani yako tena.+   Yakung’ute mavumbi, inuka na uketi, ewe Yerusalemu. Fungua pingu zilizo shingoni mwako, ewe binti ya Sayuni uliye mateka.+   Kwa maana Yehova anasema hivi: “Ninyi mliuzwa bila malipo,+Na mtakombolewa bila pesa.”+   Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Mwanzoni watu wangu walishuka kwenda Misri ili waishi huko wakiwa wageni;+Kisha Ashuru ikawakandamiza bila sababu.”   “Basi nifanye nini hapa?” auliza Yehova. “Kwa maana watu wangu walichukuliwa bila malipo. Wale wanaowatawala wanaendelea kupiga mayowe ya ushindi,”+ asema Yehova,“Na daima, mchana kutwa, jina langu linavunjiwa heshima.+   Kwa sababu hiyo watu wangu watalijua jina langu;+Kwa sababu hiyo watajua siku hiyo kwamba mimi Ndiye ninayesema. Tazama, ni mimi!”   Jinsi inavyopendeza juu ya milima, miguu ya yule anayeleta habari njema,+Anayetangaza amani,+Anayeleta habari njema za jambo bora,Anayetangaza wokovu,Anayeambia Sayuni: “Mungu wako amekuwa Mfalme!”+   Sikiliza! Walinzi wako wanapaza sauti. Wanapiga vigelegele kwa shangwe pamoja,Kwa maana wataona waziwazi* Yehova atakapokusanya Sayuni tena.   Changamkeni, pigeni pamoja vigelegele kwa shangwe, enyi magofu ya Yerusalemu,+Kwa maana Yehova amewafariji watu wake;+ amekomboa Yerusalemu.+ 10  Yehova ameufunua wazi mkono wake mtakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+Miisho yote ya dunia itayaona matendo ya wokovu ya* Mungu wetu.+ 11  Ondokeni, ondokeni, tokeni humo,+ msiguse kitu chochote kichafu!+ Tokeni kati yake,+ iweni safi,Ninyi mnaobeba vyombo vya Yehova.+ 12  Kwa maana hamtaondoka kwa wasiwasi,Wala hamtahitaji kukimbia,Kwa maana Yehova atawatangulia,+Na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi nyuma yenu.+ 13  Tazameni! Mtumishi wangu+ atatenda kwa ufahamu. Atainuliwa juu,Atainuliwa na kukwezwa sana.+ 14  Kama alivyotazamwa na wengi kwa mshangao—Kwa maana sura yake ilikuwa imeharibiwa kuliko ya mwanadamu mwingine yeyoteNa umbo lake lenye fahari kuliko la binadamu— 15  Ndivyo atakavyoyashtua mataifa mengi.+ Wafalme watafunga vinywa vyao* mbele yake,+Kwa sababu wataona mambo ambayo hawakuwa wameambiwaNa kufikiria mambo ambayo hawakuwa wamesikia.+

Maelezo ya Chini

Au “jicho kwa jicho.”
Au “itaona ushindi wa.”
Au “hawatakuwa na la kusema.”