Isaya 53:1-12

  • Kuteseka, kufa, na kuzikwa kwa mtumishi wa Yehova (1-12)

    • Adharauliwa na kuepukwa (3)

    • Abeba magonjwa na maumivu (4)

    • “Kama kondoo machinjioni” (7)

    • Abeba dhambi za wengi (12)

53  Ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?*+ Na mkono wa Yehova,+ umefunuliwa kwa nani?+   Atapanda kama tawi+ mbele yake,* kama mzizi kutoka katika nchi iliyokauka. Hana umbo la kifahari, wala utukufu wowote;+Na tunapomwona, sura yake haituvutii.*   Alidharauliwa na kuepukwa na wanadamu,+Mtu aliyekusudiwa kupata* maumivu na aliyezoea magonjwa. Ilikuwa kana kwamba uso wake ulifichwa kutoka kwetu.* Alidharauliwa, nasi tulimwona kuwa asiye na maana.+   Kwa kweli yeye mwenyewe aliyabeba magonjwa yetu,+Na kujitwika maumivu yetu.+ Lakini tulimwona kama mtu aliyepata mapigo, aliyepigwa na Mungu na kuteswa.   Lakini alichomwa*+ kwa sababu ya makosa yetu;+Alipondwa kwa sababu ya dhambi zetu.+ Aliibeba adhabu ili tupate amani,+Na kwa sababu ya majeraha yake tuliponywa.+   Sisi sote tumetangatanga kama kondoo,+Kila mmoja ameifuata njia yake mwenyewe,Na Yehova amefanya dhambi yetu sote ikutane naye.+   Alikandamizwa+ na alikubali kuteswa,+Lakini hakuthubutu kufungua kinywa chake. Aliletwa kama kondoo machinjioni,+Kama kondoo jike aliye kimya mbele ya wanaomkata manyoya,Na hakuthubutu kufungua kinywa chake.+   Kwa sababu ya kizuizi* na hukumu alichukuliwa;Na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?* Kwa maana aliondolewa katika nchi ya walio hai;+Alipata pigo* kwa sababu ya makosa ya watu wangu.+   Naye alipewa kaburi* pamoja na waovu,+Na pamoja na matajiri* katika kifo chake,+Ingawa hakuwa amefanya kosa*Na hakukuwa na udanganyifu kinywani mwake.+ 10  Lakini yalikuwa mapenzi ya Yehova* kumponda, naye aliruhusu awe mgonjwa. Ukitoa uhai wake* uwe dhabihu ya hatia,+Atauona uzao wake,* ataongeza siku zake,+Na kupitia kwake mapenzi* ya Yehova yatafanikiwa.+ 11  Kwa sababu ya mateso* yake, ataona na kuridhika. Kupitia ujuzi wake, yule mwadilifu, mtumishi wangu,+Atawaletea watu wengi msimamo wa uadilifu,+Na dhambi zao atazibeba.+ 12  Kwa sababu hiyo nitampa fungu kati ya wengi,Naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,Kwa sababu aliumwaga uhai wake* mpaka kifo+Naye alihesabiwa miongoni mwa wakosaji;+Aliibeba dhambi ya watu wengi,+Naye aliwatetea wakosaji.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “jambo ambalo tulisikia?”
Maneno “mbele yake” huenda yanarejelea mtazamaji yeyote au Mungu.
Au “hana sura ya pekee hivi kwamba tumtamani.”
Au labda, “Alikuwa kama mtu ambaye watu waligeuza mbali nyuso zao ili wasimtazame.”
Au “aliyeelewa.”
Au “alichomwa kwa silaha.”
Au “Aliuawa.”
Au “njia yake ya maisha.”
Au “ukandamizaji.”
Au “Na mtu atatoa kaburi lake.”
Tnn., “mtu tajiri.”
Au “ukatili.”
Au “nafsi yake.”
Au “mapendezi.”
Tnn., “Ataiona mbegu yake.”
Au “Yehova alifurahia.”
Au “maumivu ya nafsi.”
Au “aliimwaga nafsi yake.”