Isaya 54:1-17

  • Sayuni aliye tasa atapata wana wengi (1-17)

    • Yehova ni mume wa Sayuni (5)

    • Wana wa Sayuni watafundishwa na Yehova (13)

    • Silaha dhidi ya Sayuni zitashindwa (17)

54  “Piga vigelegele kwa shangwe, wewe mwanamke tasa ambaye hujazaa!+ Changamka na upaze sauti kwa shangwe,+ wewe ambaye hukuwahi kupata uchungu wa kuzaa,+Kwa maana wana* wa aliye ukiwa ni wengiKuliko wana wa mwanamke aliye na mume,”*+ asema Yehova.   “Pafanye mahali pa hema lako pawe na nafasi kubwa zaidi.+ Vitandaze vitambaa vya hema lako tukufu la ibada. Usizuie, refusha kamba za hema lako,Na uviimarishe vigingi vya hema lako.+   Kwa maana utaenea kulia na kushoto. Uzao wako utayamiliki mataifa,Nao watakaa katika majiji yaliyoachwa ukiwa.+   Usiogope,+ kwa maana hutaaibishwa;+Usifedheheke, kwa maana hutakatishwa tamaa. Kwa maana utaisahau aibu ya ujana wako,Nawe hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.”   “Kwa maana Muumba*+ wako Mkuu ni kama mume* wako,+Yehova wa majeshi ndilo jina lake,Na Mtakatifu wa Israeli ni Mkombozi wako.+ Ataitwa Mungu wa dunia yote.+   Kwa maana Yehova alikuita kana kwamba wewe ni mke aliyeachwa na aliye na huzuni,*+Kama mke aliyeolewa wakati wa ujana kisha akakataliwa,” asema Mungu wako.   “Kwa maana nilikuacha kwa muda mfupi,Lakini nitakukusanya tena kwa rehema nyingi.+   Kwa furiko la hasira niliuficha uso wangu kutoka kwako kwa muda mfupi,+Lakini nitakuonyesha rehema kwa upendo mshikamanifu wa milele,”+ asema Mkombozi+ wako, Yehova.   “Jambo hili kwangu ni kama siku za Noa.+ Kama nilivyoapa kwamba maji ya Noa hayataifunika tena dunia,+Ndivyo ninavyoapa kwamba sitawaka hasira tena kukuelekea wewe wala kukukemea.+ 10  Kwa maana huenda milima ikaondolewaNa huenda vilima vikatikiswa,Lakini upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwako,+Wala agano langu la amani halitatikiswa,”+ asema Yehova, Yule anayekuonyesha rehema.+ 11  “Ee mwanamke uliyeteseka,+ uliyerushwa na dhoruba, ambaye hajafarijiwa,+Ninayaweka mawe yako kwa saruji ngumuNa msingi wako kwa yakuti.+ 12  Nitatengeneza minara yako kwa zabarijadi,Na malango yako kwa mawe yanayong’aa,*Na mipaka yako yote kwa mawe yenye thamani. 13  Na wana* wako wote watafundishwa na Yehova,+Na amani ya wana* wako itakuwa nyingi.+ 14  Utaimarishwa kabisa katika uadilifu.+ Utakuwa mbali sana na ukandamizaji,+Hutaogopa chochote na hutakuwa na sababu yoyote ya kuhofu,Kwa maana haitakukaribia.+ 15  Mtu yeyote akikushambulia,Haitakuwa kwa maagizo yangu. Yeyote anayekushambulia ataanguka kwa sababu yako.”+ 16  “Tazama! Mimi mwenyewe nilimuumba fundi,Anayefukuta moto wa makaa,Naye hutengeneza silaha kwa kazi yake. Mimi mwenyewe pia nilimuumba yule mtu mharibifu ili alete uharibifu.+ 17  Hakuna silaha yoyote itakayotokezwa dhidi yako itakayofanikiwa,+Nawe utauhukumu ulimi wowote utakaoinuka dhidi yako katika hukumu. Huu ndio urithi wa watumishi wa Yehova,Na uadilifu wao unatoka kwangu,” asema Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “bwana mkubwa.”
Au “watoto.”
Au “bwana mkubwa.”
Au “Mtengenezaji.”
Tnn., “aliyeumizwa rohoni.”
Au “mawe ya moto.”
Au “watoto.”
Au “watoto.”