Isaya 55:1-13

  • Mwaliko wa kula na kunywa bure (1-5)

  • Mtafuteni Yehova na neno lake linalotegemeka (6-13)

    • Njia za Mungu ziko juu kuliko njia za mwanadamu (8, 9)

    • Neno la Mungu hakika litafanikiwa (10, 11)

55  Njooni, ninyi nyote mlio na kiu,+ njooni kwenye maji!+ Ninyi msio na pesa, njooni, nunueni na mle! Naam, njooni, mnunue divai na maziwa+ bila pesa na bila gharama.+   Kwa nini mnaendelea kulipa pesa kwa ajili ya kitu ambacho si mkate,Na kwa nini mtumie mapato yenu* kwa ajili ya kitu ambacho hakishibishi? Nisikilizeni kwa makini, mle kilicho chema,+Nanyi mtafurahia sana vitu vyenye lishe kwelikweli.*+   Tegeni sikio na mje kwangu.+ Sikilizeni, nanyi mtaendelea* kuwa hai,Nami nitafanya agano la milele pamoja nanyi bila kusita+Kulingana na matendo ya upendo mshikamanifu kwa Daudi, ambayo ni ya uaminifu.*+   Tazameni! Nilimfanya awe shahidi+ kwa mataifa,Kiongozi+ na kamanda+ kwa mataifa.   Tazama! Utaliita taifa ambalo hulijui,Na watu wa taifa ambao hawajakujua watakukimbiliaKwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ Mtakatifu wa Israeli,Kwa sababu atakutukuza.+   Mtafuteni Yehova wakati bado anapatikana.+ Mwiteni maadamu yuko karibu.+   Mtu mwovu na aiache njia yake+Na mtu mbaya mawazo yake;Na arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+Kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.*+   “Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu,+Na njia zenu si njia zangu,” asema Yehova.   “Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,Ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenuNa mawazo yangu kuliko mawazo yenu.+ 10  Kwa maana kama mvua na theluji inavyomwagika kutoka mbinguniNayo hairudi huko mpaka iiloweshe dunia na kuifanya izae na kuchipuka,Na kumpa mbegu mpandaji na mkate yule anayekula, 11  Hivyo ndivyo neno langu linalotoka katika kinywa changu litakavyokuwa.*+ Halitarudi kwangu bila matokeo,+Bali hakika litatimiza jambo lolote linalonipendeza,*+Na hakika litafanikiwa katika yale ambayo nimelituma. 12  Kwa maana ninyi mtatoka nje kwa shangwe,+Nanyi mtarudishwa kwa amani.+ Milima na vilima vitachangamka mbele yenu kwa vigelegele vya shangwe,+Na miti yote ya msituni itapiga makofi.+ 13  Badala ya vichaka vya miiba, mberoshi utakua,+Na badala ya upupu unaowasha, mhadasi utakua. Na jambo hilo litamletea Yehova sifa,*+Ishara ya milele ambayo haitatoweka kamwe.”

Maelezo ya Chini

Au “pesa mlizopata kwa shida.”
Tnn., “mtafurahia sana unono.”
Au “yenye kuaminika; kutegemeka.”
Au “nafsi yenu itaendelea.”
Au “kwa hiari.”
Au “mapenzi yangu.”
Au “litathibitika kuwa.”
Au “litamjengea jina Yehova.”