Isaya 56:1-12

  • Baraka kwa wageni na matowashi (1-8)

    • Nyumba ya sala kwa ajili ya wote (7)

  • Walinzi vipofu, mbwa walio bubu (9-12)

56  Yehova anasema hivi: “Tekelezeni haki,+ na mtende uadilifu,Kwa maana wokovu wangu utakuja hivi karibuniNa uadilifu wangu utafunuliwa.+   Mwenye furaha ni mtu anayefanya jambo hiliNa mwana wa mtu anayeendelea kulishika kabisa,Anayeishika Sabato na asiyeitia unajisi+Na ambaye anauzuia mkono wake usitende uovu wowote.   Mgeni anayejiunga na Yehova+ asiseme,‘Bila shaka Yehova atanitenga na watu wake.’ Naye towashi asiseme, ‘Tazama! Mimi ni mti uliokauka.’”  Kwa maana mimi Yehova ninawaambia hivi matowashi wanaozishika sabato zangu na kuchagua mambo yanayonipendeza na kulishika kabisa agano langu:   “Nitawapa mnara wa ukumbusho na jina katika nyumba yangu na katika kuta zangu,Jambo bora kuliko wana na mabinti. Nitawapa jina linalodumu milele,Ambalo halitaangamia.   Na wageni wanaojiunga nami Yehova ili kunihudumia,Kulipenda jina langu mimi Yehova+Na kuwa watumishi wangu,Wote wanaoishika Sabato na wasioitia unajisiNa wanaolishika kabisa agano langu,   Nitawaleta pia kwenye mlima wangu mtakatifu+Na kuwafanya washangilie ndani ya nyumba yangu ya sala. Dhabihu zao nzima za kuteketezwa na matoleo yao yatakubaliwa kwenye madhabahu yangu. Kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote.”+  Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, anayewakusanya waliotawanyika wa Israeli,+ anasema hivi: “Nitawakusanya wengine wajiunge naye mbali na wale ambao tayari wamekusanywa.”+   Ninyi nyote wanyama wa mwituni, njooni mle,Ninyi nyote wanyama wa mwituni mlio msituni.+ 10  Walinzi wake ni vipofu,+ hakuna hata mmoja ambaye ameona.+ Wote ni mbwa walio bubu, wasioweza kubweka.+ Wanahemahema na kulala chini; wanapenda kulala. 11  Wao ni mbwa walafi;*Hawashibi kamwe. Wao ni wachungaji wasio na uelewaji.+ Wote wamefuata njia yao wenyewe;Kila mmoja wao anatafuta faida isiyo ya haki na kusema: 12  “Njooni, acheni nichukue divai,Na acheni tunywe kileo kingi.+ Na kesho itakuwa kama leo, itakuwa bora hata zaidi!”

Maelezo ya Chini

Au “wenye nafsi yenye nguvu.”