Isaya 57:1-21

  • Mtu mwadilifu na watu washikamanifu waangamia (1, 2)

  • Ukahaba wa kiroho wa Israeli wafunuliwa (3-13)

  • Faraja kwa watu wa hali ya chini (14-21)

    • Waovu ni kama bahari iliyochafuka (20)

    • Hakuna amani kwa waovu (21)

57  Mwadilifu ameangamia,Lakini hakuna yeyote anayetia jambo hilo moyoni. Watu washikamanifu wanaondolewa,*+Na hakuna mtu anayetambua kwamba mwadilifu ameondolewaKwa sababu ya* msiba.   Yeye huingia katika amani. Wanapumzika vitandani mwao,* wote wanaotembea kwa unyoofu.   “Lakini ninyi karibieni,Enyi wana wa mwanamke mlozi,Ninyi watoto wa mzinzi na kahaba:   Mnamkejeli nani? Ni nani mnayemfungulia kinywa wazi na kumtolea ulimi? Je, ninyi si watoto wa ukosaji,Watoto wa udanganyifu,+   Wale wanaowaka tamaa kati ya miti mikubwa,+Chini ya kila mti wenye majani mengi,+Wanaowachinja watoto kwenye mabonde,*+Chini ya mipasuko ya majabali?   Mawe laini ya bondeni* ndilo fungu lako. Naam, hayo ndiyo fungu lako.+ Hata unayamiminia matoleo ya kinywaji na kutoa zawadi juu yake.+ Je, niridhike* na mambo hayo?   Ulikitayarisha kitanda chako juu ya mlima mrefu ulioinuka,+Nawe ukapanda huko ili kutoa dhabihu.+   Uliweka ukumbusho wako nyuma ya mlango na nyuma ya mwimo wa mlango. Uliniacha nawe ukajifunua;Ulipanda huko na kukipanua kitanda chako. Nawe ukafanya agano pamoja nao. Ulipenda kulala nao kitandani mwao,+Nawe ulikitazama kiungo cha kiume.*   Ulishuka kwa Meleki* ukiwa na mafutaNa ukiwa na manukato mengi. Uliwatuma wajumbe wako mbali,Hivi kwamba ukashuka Kaburini.* 10  Umejitaabisha ukifuata njia zako nyingi,Lakini hukusema, ‘Hakuna matumaini!’ Ulipata nguvu mpya. Ndiyo sababu hukati tamaa.* 11  Ulimhofu na kumwogopa naniHivi kwamba ukaanza kusema uwongo?+ Hukunikumbuka mimi.+ Hukutia jambo lolote moyoni mwako.+ Je, sijakaa kimya na kujiondoa?*+ Kwa hiyo hukuniogopa mimi. 12  Nitatangaza ‘uadilifu’ wako+ na kazi zako,+Nazo hazitakunufaisha.+ 13  Unapolilia msaada,Sanamu ulizojikusanyia hazitakuokoa.+ Upepo utazipeperusha zote mbali sana,Zitapeperushwa na pumzi tu,Lakini yule anayenikimbilia atairithi nchiNaye ataumiliki mlima wangu mtakatifu.+ 14  Itasemwa, ‘Tengenezeni, tengenezeni barabara! Tayarisheni njia!+ Ondoeni kizuizi chochote katika njia ya watu wangu.’” 15  Kwa maana Yule Aliye Juu na Aliyetukuka Sana,Anayeishi* milele+ na ambaye jina lake ni takatifu+ anasema hivi: “Ninaishi mahali palipo juu na patakatifu,+Lakini ninaishi pia na wale waliopondwa na wenye roho ya unyenyekevu,Ili kuihuisha roho ya watu wa hali ya chiniNa kuuhuisha moyo wa wale wanaopondwa.+ 16  Kwa maana sitawapinga mileleWala kuwa na hasira daima;+Kwa sababu roho ya mwanadamu itadhoofika kwa sababu yangu,+Hata viumbe wanaopumua ambao niliwaumba. 17  Nilikasirika kwa sababu alitenda dhambi kwa kufuatilia faida isiyo ya haki,+Basi nikampiga, nikauficha uso wangu, nami nikashikwa na hasira. Lakini aliendelea kuwa mwasi+ akifuata njia ya moyo wake. 18  Nimeziona njia zake,Lakini nitamponya+ na kumwongoza+Na kumrudishia* faraja yeye+ na watu wake wanaoomboleza.”+ 19  “Ninaumba matunda ya midomo. Yule aliye mbali sana atapewa amani ya kudumu na pia yule aliye karibu,”+ asema Yehova,“Nami nitamponya.” 20  “Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka ambayo haiwezi kutulia,Na maji yake yanaendelea kurusharusha juu magugu ya baharini na matope. 21  Hakuna amani kwa waovu,”+ asema Mungu wangu.

Maelezo ya Chini

Au labda, “Kutokana na.”
Yaani, katika kifo.
Yaani, kaburini.
Au “makorongo.”
Au “Je, nijifariji.”
Au “korongoni.”
Huenda maneno hayo yanarejelea ibada ya sanamu.
Au labda, “mfalme.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “huchoki.”
Au “kuficha mambo.”
Au “Anayekaa.”
Au “kufidia kwa kumpa.”