Isaya 58:1-14

  • Kufunga kwa kweli na kwa uwongo (1-12)

  • Kushika Sabato kwa furaha (13, 14)

58  “Ita kwa sauti yote kutoka kooni; usijizuie! Paza sauti yako kama pembe. Watangazie watu wangu uasi wao,+Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.   Wananitafuta siku baada ya siku,Nao wanafurahia kuzijua njia zangu,Kana kwamba walikuwa taifa lililotenda uadilifuNa ambalo halikuacha haki ya Mungu wao.+ Wananiomba hukumu za uadilifu,Wakifurahia kumkaribia Mungu:+   ‘Kwa nini huoni, tunapofunga?+ Na kwa nini hutambui tunapojitesa?’*+ Kwa sababu siku mnayofunga mnafuatia mapendezi yenu wenyewe,*Nanyi mnawakandamiza wafanyakazi wenu.+   Kufunga kwenu huishia kwenye ugomvi na vita,Nanyi mnashambulia kwa ngumi ya uovu. Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na sauti yenu isikiwe mbinguni.   Je, kufunga ambako ninachagua kunapaswa kuwa hivi,Siku ya mtu kujitesa,*Kuinamisha chini kichwa chake kama utete,Na kufanya nguo za magunia na majivu yawe kitanda chake? Je, huko ndiko unakoita kufunga na siku inayompendeza Yehova?   Hapana, huku ndiko kufunga ambako ninachagua: Kuondoa pingu za uovu,Kufungua vifungo vya nira,+Kuwaachilia huru waliokandamizwa,+Na kuivunja kila nira mara mbili;   Ni kumgawia aliye na njaa mkate wako,+Kuwaleta maskini na wasio na makao nyumbani mwako,Kumvisha aliye uchi unapokutana naye,+Na kutowageuzia mgongo watu wako wa ukoo.   Ndipo nuru yako itakapochomoza kama mapambazuko,+Na uponyaji wako utatokea upesi. Uadilifu wako utakutangulia,Na utukufu wa Yehova utakuwa ulinzi nyuma yako.+   Kisha utaita, na Yehova atakujibu;Utalilia msaada, naye atasema, ‘Mimi hapa!’ Ukiiondoa nira kati yakoUkiacha kunyoosha kidole chako na kuacha kuongea mambo yanayodhuru,+ 10  Ukimpa mwenye njaa kile ambacho wewe mwenyewe unatamani*+Na kuwashibisha wale wanaoteseka,*Ndipo nuru yako itakapong’aa hata gizani,Na giza lako litakuwa kama adhuhuri.+ 11  Yehova atakuongoza daimaNa kukushibisha* hata katika nchi iliyokauka;+Ataitia nguvu mifupa yako,Nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+Kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe. 12  Watajenga upya magofu ya kale kwa sababu yako,+Nawe utairudisha misingi ya vizazi vilivyopita.+ Utaitwa mrekebishaji wa kuta zilizobomoka,*+Mrekebishaji wa barabara zinazopita kwenye makao. 13  Ikiwa kwa sababu ya Sabato unaacha kufuatilia* mapendezi yako mwenyewe* katika siku yangu takatifu+Nawe uiite Sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, siku ya kutukuzwa,+Nawe uitukuze badala ya kufuatilia mapendezi yako mwenyewe na kusema maneno ya upuuzi, 14  Ndipo utakapopata furaha tele katika Yehova,Nami nitakufanya upande sehemu za juu za dunia.+ Nitakufanya ule kutokana na* urithi wa Yakobo babu yako,+Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hivyo.”

Maelezo ya Chini

Au “tunapozitesa nafsi zetu?”
Au “mambo mnayofurahia.”
Au “kuitesa nafsi yake.”
Au “kuzishibisha nafsi zinazoteseka.”
Au “tamaa za nafsi yako.”
Au “kuishibisha nafsi yako.”
Tnn., “wa mashimo yaliyo katika ukuta.”
Tnn., “unaugeuza mguu wako usifuatilie.”
Au “mambo unayofurahia.”
Au “ufurahie.”