Isaya 58:1-14
58 “Ita kwa sauti yote kutoka kooni; usijizuie!
Paza sauti yako kama pembe.
Watangazie watu wangu uasi wao,+Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.
2 Wananitafuta siku baada ya siku,Nao wanafurahia kuzijua njia zangu,Kana kwamba walikuwa taifa lililotenda uadilifuNa ambalo halikuacha haki ya Mungu wao.+
Wananiomba hukumu za uadilifu,Wakifurahia kumkaribia Mungu:+
3 ‘Kwa nini huoni, tunapofunga?+
Na kwa nini hutambui tunapojitesa?’*+
Kwa sababu siku mnayofunga mnafuatia mapendezi yenu wenyewe,*Nanyi mnawakandamiza wafanyakazi wenu.+
4 Kufunga kwenu huishia kwenye ugomvi na vita,Nanyi mnashambulia kwa ngumi ya uovu.
Hamwezi kufunga kama mnavyofanya leo na sauti yenu isikiwe mbinguni.
5 Je, kufunga ambako ninachagua kunapaswa kuwa hivi,Siku ya mtu kujitesa,*Kuinamisha chini kichwa chake kama utete,Na kufanya nguo za magunia na majivu yawe kitanda chake?
Je, huko ndiko unakoita kufunga na siku inayompendeza Yehova?
6 Hapana, huku ndiko kufunga ambako ninachagua:
Kuondoa pingu za uovu,Kufungua vifungo vya nira,+Kuwaachilia huru waliokandamizwa,+Na kuivunja kila nira mara mbili;
7 Ni kumgawia aliye na njaa mkate wako,+Kuwaleta maskini na wasio na makao nyumbani mwako,Kumvisha aliye uchi unapokutana naye,+Na kutowageuzia mgongo watu wako wa ukoo.
8 Ndipo nuru yako itakapochomoza kama mapambazuko,+Na uponyaji wako utatokea upesi.
Uadilifu wako utakutangulia,Na utukufu wa Yehova utakuwa ulinzi nyuma yako.+
9 Kisha utaita, na Yehova atakujibu;Utalilia msaada, naye atasema, ‘Mimi hapa!’
Ukiiondoa nira kati yakoUkiacha kunyoosha kidole chako na kuacha kuongea mambo yanayodhuru,+
10 Ukimpa mwenye njaa kile ambacho wewe mwenyewe unatamani*+Na kuwashibisha wale wanaoteseka,*Ndipo nuru yako itakapong’aa hata gizani,Na giza lako litakuwa kama adhuhuri.+
11 Yehova atakuongoza daimaNa kukushibisha* hata katika nchi iliyokauka;+Ataitia nguvu mifupa yako,Nawe utakuwa kama bustani iliyonyweshwa maji vizuri,+Kama chemchemi ambayo maji yake hayakauki kamwe.
12 Watajenga upya magofu ya kale kwa sababu yako,+Nawe utairudisha misingi ya vizazi vilivyopita.+
Utaitwa mrekebishaji wa kuta zilizobomoka,*+Mrekebishaji wa barabara zinazopita kwenye makao.
13 Ikiwa kwa sababu ya Sabato unaacha kufuatilia* mapendezi yako mwenyewe* katika siku yangu takatifu+Nawe uiite Sabato kuwa ni furaha tele, siku takatifu ya Yehova, siku ya kutukuzwa,+Nawe uitukuze badala ya kufuatilia mapendezi yako mwenyewe na kusema maneno ya upuuzi,
14 Ndipo utakapopata furaha tele katika Yehova,Nami nitakufanya upande sehemu za juu za dunia.+
Nitakufanya ule kutokana na* urithi wa Yakobo babu yako,+Kwa maana kinywa cha Yehova kimesema hivyo.”
Maelezo ya Chini
^ Au “tunapozitesa nafsi zetu?”
^ Au “mambo mnayofurahia.”
^ Au “kuitesa nafsi yake.”
^ Au “kuzishibisha nafsi zinazoteseka.”
^ Au “tamaa za nafsi yako.”
^ Au “kuishibisha nafsi yako.”
^ Tnn., “wa mashimo yaliyo katika ukuta.”
^ Tnn., “unaugeuza mguu wako usifuatilie.”
^ Au “mambo unayofurahia.”
^ Au “ufurahie.”