Isaya 6:1-13

  • Maono ya Yehova katika hekalu lake (1-4)

    • “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova” (3)

  • Midomo ya Isaya yasafishwa (5-7)

  • Isaya atumwa (8-10)

    • “Mimi hapa! Nitume mimi!” (8)

  • “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” (11-13)

6  Katika mwaka ambao Mfalme Uzia alikufa,+ nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti cha ufalme kilicho juu na kilichoinuliwa,+ na pindo za kanzu yake zilijaa hekaluni.  Maserafi walikuwa wamesimama juu yake; kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita. Kila mmoja aliufunika uso wake kwa mabawa mawili na alifunika miguu yake kwa mawili, na kila mmoja wao aliruka huku na huku kwa mawili.   Na kila mmoja alimwambia mwenzake: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova wa majeshi.+ Dunia yote imejaa utukufu wake.”  Na viegemeo vya milango vikatetemeka kwa sababu ya ile sauti kubwa,* na nyumba ikajaa moshi.+   Kisha nikasema: “Ole wangu! Kwa maana ni kama nimekufa,*Kwa maana mimi ni mtu asiye na midomo safi,Nami ninaishi kati ya watu wasio na midomo safi;+Kwa maana macho yangu yamemwona Mfalme, Yehova wa majeshi mwenyewe!”  Ndipo mmoja wa maserafi akaruka kunijia, na mkononi mwake alikuwa na kaa linalowaka+ alilokuwa amechukua kwa koleo kutoka kwenye madhabahu.+  Akakigusa kinywa changu na kusema: “Tazama! Hili limeigusa midomo yako. Hatia yako imeondolewa,Na dhambi yako imefunikwa.”  Kisha nikasikia sauti ya Yehova ikiuliza: “Nimtume nani, na ni nani atakayeenda kwa ajili yetu?”+ Nami nikasema: “Mimi hapa! Nitume mimi!”+   Ndipo akasema, “Nenda, uwaambie hivi watu hawa: ‘Mtasikia tena na tena,Lakini hamtaelewa;Mtaona tena na tena,Lakini hamtapata ujuzi wowote.’+ 10  Ufanye moyo wa watu hawa uwe mgumu,+Yafanye masikio yao yawe mazito,+Na uyafunge kabisa macho yao,Ili wasione kwa macho yaoNa wasisikie kwa masikio yao,Ili moyo wao usieleweNao wasigeuke na kuponywa.” 11  Ndipo nikauliza: “Ni mpaka lini, Ee Yehova?” Kisha akasema: “Mpaka majiji yabomoke yawe magofu bila mkaajiNa nyumba zisiwe na watuNa nchi iharibiwe na kubaki ukiwa;+ 12  Mpaka Yehova awaondoe watu na kuwapeleka mbali+Na hali ya ukiwa ya nchi ienee sana. 13  “Lakini bado kutakuwa na sehemu ya kumi ndani yake, nayo itateketezwa tena, kama mti mkubwa na kama mwaloni, ambayo inapokatwa huacha kisiki; mbegu takatifu itakuwa* kisiki chake.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “sauti ya yule aliyekuwa akiita.”
Tnn., “nimenyamazishwa.”
Au “uzao mtakatifu utakuwa.”