Isaya 60:1-22

  • Utukufu wa Mungu wang’aa juu ya Sayuni (1-22)

    • Kama njiwa kwenye viota vyao (8)

    • Dhahabu badala ya shaba (17)

    • Mdogo atakuwa elfu (22)

60  “Inuka, Ee mwanamke,+ angaza nuru, kwa maana nuru yako imekuja. Utukufu wa Yehova unakuangazia.+   Kwa maana tazama! giza litaifunika duniaNa utusitusi mzito utayafunika mataifa;Lakini Yehova atakuangazia,Na utukufu wake utaonekana juu yako.   Mataifa yataenda kwenye nuru yako+Na wafalme+ kwenye fahari yako inayong’aa.*+   Inua macho yako utazame pande zote kukuzunguka! Wote wamekusanywa; wanakuja kwako. Wana wako wanaendelea kuja kutoka mbali sana,+Na mabinti wako wakiwa wametegemezwa viunoni.+   Wakati huo utaona na kung’aa,+Na moyo wako utadundadunda na kufurika,Kwa sababu utajiri wa bahari utaelekezwa kwako;Mali za mataifa zitakuja kwako.+   Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,*Ngamia dume wachanga wa Midiani na Efa.+ Wote kutoka Sheba—watakuja;Watabeba dhahabu na ubani. Watatangaza sifa za Yehova.+   Makundi yote ya Kedari+ yatakusanywa kwako. Kondoo dume wa Nebayothi+ watakutumikia. Watakuja kwenye madhabahu yangu wakiwa na kibali,+Nami nitairembesha nyumba yangu yenye utukufu.*+   Ni nani hawa wanaokuja wakiruka kama mawingu,Kama njiwa kwenye viota vyao?*   Kwa maana visiwa vitanitumaini;+Meli za Tarshishi zinaongoza,*Kuwaleta wana wako kutoka mbali sana,+Pamoja na fedha yao na dhahabu yao,Kwa sifa ya jina la Yehova Mungu wako na ya Mtakatifu wa Israeli,Kwa maana atakutukuza.*+ 10  Wageni watazijenga kuta zako,Na wafalme wao watakuhudumia,+Kwa maana nilikupiga kwa hasira yangu,Lakini kwa kibali changu* nitakuonyesha rehema.+ 11  Malango yako yatakuwa wazi daima;+Hayatafungwa mchana wala usiku,Ili kukuletea mali za mataifa,Na wafalme wao wataongoza.+ 12  Kwa maana taifa lolote na ufalme wowote ambao hautakutumikia utaangamia,Nayo mataifa yataharibiwa kabisa.+ 13  Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako,+Mberoshi, mtidhari, na mvinje pamoja,+Ili kuparembesha mahali pangu patakatifu;Nitapatukuza mahali pa miguu yangu.+ 14  Wana wa wale waliokukandamiza watakuja na kuinama chini mbele yako;Wote wanaokudharau watainama chini miguuni pako,Nao watalazimika kukuita jiji la Yehova,Sayuni la Mtakatifu wa Israeli.+ 15  Badala ya kuwa aliyeachwa na kuchukiwa, bila yeyote kupita ndani yako,+Nitakufanya uwe chanzo cha fahari ya milele,Chanzo cha shangwe kwa vizazi vyote.+ 16  Nawe kwa kweli utakunywa maziwa ya mataifa,+Utanyonya matiti ya wafalme;+Nawe hakika utajua kwamba mimi, Yehova, ni Mwokozi wako,Na Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mkombozi wako.+ 17  Badala ya shaba nitaleta dhahabu,Na badala ya chuma nitaleta fedha,Badala ya mbao, shaba,Na badala ya mawe, chuma;Nitaweka amani kuwa waangalizi wakoNa uadilifu kuwa watu wako wanaogawa kazi.+ 18  Ukatili hautasikiwa tena katika nchi yakoWala maangamizi na uharibifu katika mipaka yako.+ Nawe utaziita kuta zako Wokovu+ na malango yako Sifa. 19  Kwa maana jua halitakuwa tena nuru ya mchana kwako,Wala nuru ya mwezi haitakuangazia,Kwa maana Yehova atakuwa nuru ya milele kwako,+Na Mungu wako atakuwa urembo wako.+ 20  Jua lako halitatua tena,Wala mwezi wako hautafifia,Kwa maana Yehova atakuwa nuru yako ya milele,+Na siku zako za kuomboleza zitakuwa zimekwisha.+ 21  Na watu wako wote watakuwa waadilifu;Wataimiliki nchi milele. Wao ndio chipukizi nililopanda,Kazi ya mikono yangu,+ ili nirembeshwe.+ 22  Mdogo atakuwa elfuNa mnyonge atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaliharakisha jambo hilo kwa wakati wake.”

Maelezo ya Chini

Au “kwenye mwangaza wa mapambazuko yako.”
Tnn., “yatakufunika.”
Au “nyumba yangu ya urembo.”
Au “matundu katika nyumba ya ndege?”
Au “atakurembesha.”
Au “kama zilivyokuwa awali.”
Au “kwa nia yangu njema.”