Isaya 61:1-11

  • Atiwa mafuta ili kutangaza habari njema (1-11)

    • “Mwaka wa nia njema ya Yehova” (2)

    • “Miti mikubwa ya uadilifu” (3)

    • Watu wa nchi nyingine watasaidia (5)

    • “Makuhani wa Yehova” (6)

61  Roho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova iko juu yangu,+Kwa sababu Yehova alinitia mafuta niwatangazie wapole habari njema.+ Alinituma kuyafunga majeraha ya waliovunjika moyo,Kuwatangazia mateka uhuruNa kutangaza kwamba macho ya wafungwa yatafunguliwa kabisa,+   Kutangaza mwaka wa nia njema ya* YehovaNa siku ya kisasi ya Mungu wetu,+Kuwafariji wote wanaoomboleza,+   Kuwaandalia mahitaji wale wanaoombolezea Sayuni,Kuwapa vazi la kichwani badala ya majivu,Mafuta ya furaha badala ya maombolezo,Vazi la sifa badala ya roho iliyovunjika. Nao wataitwa miti mikubwa ya uadilifu,Bustani ya Yehova, ili kumtukuza.*+   Watajenga upya magofu ya kale;Watasimamisha sehemu zilizoachwa ukiwa za zamani,+Nao watajenga upya majiji yaliyoharibiwa,+Sehemu zilizoachwa ukiwa kizazi baada ya kizazi.+   “Wageni watakuja na kuichunga mifugo yenu,Nao watu wa nchi nyingine+ watakuwa wakulima wenu na watunzaji wa mizabibu yenu.+   Nanyi mtaitwa makuhani wa Yehova;+Watawaita wahudumu wa Mungu wetu. Mtakula mali za mataifa,+Nanyi mtajivunia utukufu* wao.   Badala ya aibu mtakuwa na fungu mara mbili,Na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya fungu lao. Naam, watamiliki fungu mara mbili katika nchi yao.+ Watakuwa na shangwe milele.+   Kwa maana mimi, Yehova, ninapenda haki;+Ninachukia unyang’anyi na ukosefu wa uadilifu.+ Nitawapa malipo yao kwa uaminifu,Nami nitafanya agano la milele pamoja nao.+   Uzao wao utajulikana* miongoni mwa mataifa+Na wazao wao miongoni mwa watu. Wote wanaowaona watawatambua,Kwamba wao ni uzao ambao* Yehova amebariki.”+ 10  Nitashangilia sana katika Yehova. Nafsi yangu yote itashangilia katika Mungu wangu.+ Kwa maana amenivisha mavazi ya wokovu;+Amenifunika kwa joho* la uadilifu,Kama bwana harusi anayevaa kilemba kama cha kuhani,+Na kama bibi harusi anayejipamba kwa mapambo yake. 11  Kwa maana kama dunia inavyochipusha mimeaNa kama bustani inavyochipusha vitu vilivyopandwa humo,Ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu YehovaAtakavyofanya uadilifu+ na sifa zichipuke+ mbele ya mataifa yote.

Maelezo ya Chini

Au “kibali cha.”
Au “kumrembesha.”
Au “utajiri.”
Tnn., “mbegu ambayo.”
Tnn., “Mbegu yao itajulikana.”
Au “joho lisilo na mikono.”