Isaya 62:1-12

  • Jina jipya la Sayuni (1-12)

62  Sitanyamaza kwa ajili ya Sayuni,+Nami sitatulia kwa ajili ya YerusalemuMpaka uadilifu wake ung’ae kama mwangaza mkali+Na wokovu wake uwake kama mwenge.+   “Mataifa yatauona uadilifu wako, ewe mwanamke,+Na wafalme wote utukufu wako.+ Nawe utaitwa kwa jina jipya,+Ambalo kinywa cha Yehova mwenyewe kitalichagua.   Utakuwa taji la urembo mkononi mwa Yehova,Kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.   Hutaitwa tena mwanamke aliyeachwa,+Na nchi yako haitaitwa tena ukiwa.+ Lakini utaitwa Furaha Yangu Imo Ndani Yake,+Na nchi yako itaitwa Aliyeolewa. Kwa maana Yehova atafurahishwa nawe,Na nchi yako itakuwa kama aliyeolewa.   Kwa maana kama kijana wa kiume anavyomwoa msichana bikira,Ndivyo wana wako watakavyokuoa. Kama bwana harusi anavyomfurahia bibi harusiNdivyo Mungu wako atakavyokufurahia.+   Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu. Hawapaswi kukaa kimya daima, mchana kutwa na usiku kucha. Ninyi mnaomtaja Yehova,Msipumzike,   Na msiache kamwe apumzike mpaka aliimarishe kabisa Yerusalemu,Naam, mpaka alifanye kuwa sifa ya dunia.”+   Yehova ameapa kiapo kwa mkono wake wa kuume, kwa mkono wake wenye nguvu: “Sitawapa tena maadui wako nafaka yako iwe chakula chao,Wala wageni hawatakunywa divai yako mpya, ambayo umetaabika kuipata.+   Lakini wale wanaoikusanya wataila nao watamsifu Yehova;Na wale wanaoikusanya watainywa katika nyua zangu takatifu.”+ 10  Piteni humo, piteni katika malango. Watayarishieni watu njia.+ Tengenezeni, tengenezeni barabara kuu. Ondoeni mawe juu yake.+ Inueni ishara* kwa ajili ya watu.+ 11  Tazama! Yehova ametangaza mpaka kwenye miisho ya dunia: “Mwambieni binti ya Sayuni,‘Tazama! Wokovu wako unakuja.+ Tazama! Anakuja na thawabu yake,Na malipo anayotoa yako mbele zake.’”+ 12  Wataitwa watu watakatifu, wale waliokombolewa na Yehova,+Nawe utaitwa Aliyetafutwa, Jiji Ambalo Halikuachwa.+

Maelezo ya Chini

Au “nguzo ya ishara.”