Isaya 63:1-19

  • Kisasi cha Yehova dhidi ya mataifa (1-6)

  • Upendo mshikamanifu wa Yehova nyakati za zamani (7-14)

  • Sala ya toba (15-19)

63  Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu,+Kutoka Bosra+ akiwa na mavazi yenye rangi zinazong’aa,*Huyu aliye na mavazi ya kifahari,Anayetembea kwa nguvu zake nyingi? “Ni mimi, Yule anayesema kwa uadilifu,Yule aliye na nguvu nyingi za kuokoa.”   Kwa nini mavazi yako ni mekundu,Na kwa nini mavazi yako ni kama ya mtu anayekanyaga shinikizo la divai?+   “Nimelikanyaga pipa la divai nikiwa peke yangu. Hakuna mtu yeyote kutoka katika mataifa aliyekuwa pamoja nami. Niliendelea kuwakanyaga kwa hasira yangu,Nami niliendelea kuwakanyaga kwa ghadhabu yangu.+ Mavazi yangu yalijaa madoa ya damu yao,Nami nimezichafua nguo zangu zote.   Kwa maana siku ya kisasi imo moyoni mwangu,+Na mwaka wa watu wangu waliokombolewa umefika.   Nilitazama, lakini hapakuwa na yeyote wa kunisaidia;Nilishangaa kwamba hakuna yeyote aliyenitegemeza. Basi mkono wangu ukaniletea wokovu,*+Na ghadhabu yangu mwenyewe ikanitegemeza.   Niliwakanyaga watu kwa hasira yangu,Niliwalewesha kwa ghadhabu yangu+Niliimwaga damu yao ardhini.”   Nitayataja matendo ya Yehova ya upendo mshikamanifu,Matendo ya Yehova yanayostahili sifa,Kwa sababu ya mambo yote ambayo Yehova ametutendea,+Mambo mengi mema ambayo ameitendea nyumba ya Israeli,Kulingana na rehema zake na upendo wake mshikamanifu ulio mwingi.   Kwa maana alisema: “Kwa hakika hawa ni watu wangu, wana ambao hawatakosa kuwa washikamanifu.”*+ Basi akawa Mwokozi wao.+   Katika taabu zao zote, yeye alitaabika.+ Na mjumbe wake binafsi* akawaokoa.+ Kwa upendo na huruma yake aliwakomboa,+Naye aliwainua na kuwabeba siku zote za zamani.+ 10  Lakini waliasi+ na kuihuzunisha roho yake takatifu.+ Naye akageuka na kuwa adui yao,+Naye akawapiga vita.+ 11  Nao wakazikumbuka siku za zamani,Siku za Musa mtumishi wake: “Yuko wapi Yule aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+ Yuko wapi Yule aliyetia ndani yake roho Yake takatifu,+ 12  Yule aliyeufanya mkono Wake mtukufu uende pamoja na mkono wa kulia wa Musa,+Yule aliyeyatenganisha maji mbele yao+Ili kujifanyia jina la milele,+ 13  Yule aliyewafanya watembee katika maji yenye mawimbi makubwa,*Hivi kwamba wakatembea bila kujikwaa,Kama farasi katika nchi iliyo wazi?* 14  Kama mifugo wanavyoteremka katika bonde tambarare,Ndivyo roho ya Yehova ilivyowapumzisha.”+ Hivyo ndivyo ulivyowaongoza watu wako,Ili ujijengee jina kuu.*+ 15  Tazama kutoka mbinguni uoneKutoka kwenye makao yako yaliyoinuliwa ya utakatifu na utukufu.* Iko wapi bidii yako na nguvu zako,Shauku ya huruma*+ na rehema yako?+ Zimeondolewa kwangu. 16  Kwa maana wewe ni Baba yetu;+Ingawa huenda Abrahamu asitujueNa huenda Israeli asitutambue,Wewe, Ee Yehova, ni Baba yetu. Mkombozi wetu wa zamani za kale ndilo jina lako.+ 17  Kwa nini, Ee Yehova, unaruhusu* tutangetange kutoka kwenye njia zako? Kwa nini unaruhusu* mioyo yetu iwe migumu ili tusikuogope?+ Rudi, kwa ajili ya watumishi wako,Makabila ya urithi wako.+ 18  Watu wako watakatifu waliimiliki kwa muda mfupi. Maadui wetu walipakanyaga-kanyaga mahali pako patakatifu.+ 19  Kwa muda mrefu sana tumekuwa kama watu ambao hukuwatawala kamwe,Kama watu ambao hawakuitwa kamwe kwa jina lako.

Maelezo ya Chini

Au labda, “nyekundu nyangavu.”
Au “ushindi.”
Au “ambao hawatakuwa waongo.”
Au “malaika wa uwepo wake.”
Au “maji yenye kina kirefu.”
Au “nyikani.”
Au “zuri.”
Au “uzuri.”
Tnn., “Msukosuko wa sehemu zako za ndani.”
Au “unatufanya.”
Tnn., “unafanya.”