Isaya 64:1-12

  • Sala ya toba yaendelea (1-12)

    • Yehova “Mfinyanzi wetu” (8)

64  Laiti ungezipasua mbingu ushuke chini,Ili milima itetemeke kwa sababu yako,   Kama moto unavyoteketeza vichaka,Na moto huo unachemsha maji,Basi jina lako litajulikana kwa maadui wako,Na mataifa yatatetemeka mbele zako!   Ulipofanya mambo yanayoogopesha ambayo hatungeweza kuyatazamia,+Ulishuka, nayo milima ikatetemeka mbele zako.+   Tangu zamani hakuna mtu aliyesikia wala kutega sikio,Wala hakuna jicho lililomwona Mungu, isipokuwa wewe,Yule anayetenda kwa ajili ya wale wanaoendelea kumtarajia.*+   Umekutana na wale wanaoshangilia kutenda mambo yanayofaa,+Wale wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Tazama! Ulikuwa na ghadhabu, huku sisi tukiendelea kutenda dhambi,+Tulifanya hivyo kwa muda mrefu. Je, sasa tuokolewe?   Na sisi sote tumekuwa kama mtu asiye safi,Na matendo yetu yote ya uadilifu ni kama kitambaa cha hedhi.+ Sisi sote tutanyauka kama jani,Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.   Hakuna yeyote anayeliitia jina lako,Hakuna yeyote anayejichochea kukushika,Kwa maana umeuficha uso wako kutoka kwetu,+Nawe unatufanya tudhoofike* kwa sababu ya* kosa letu.   Lakini sasa, Ee Yehova, wewe ni Baba yetu.+ Sisi ni udongo, nawe ni Mfinyanzi wetu;*+Sisi sote ni kazi ya mkono wako.   Usiwe na ghadhabu nyingi, Ee Yehova,+Nawe usilikumbuke kosa letu milele. Tafadhali, tutazame, kwa maana sisi sote ni watu wako. 10  Majiji yako matakatifu yamekuwa nyika. Sayuni imekuwa nyika,Yerusalemu limekuwa ukiwa.+ 11  Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*Ambamo mababu zetu walikusifu,Imeteketezwa kwa moto,+Na vitu vyote tulivyovithamini sana vimeharibiwa. 12  Baada ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova? Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke kupita kiasi?+

Maelezo ya Chini

Au “kumngojea kwa subira.”
Tnn., “kwa mkono wa.”
Tnn., “tuyeyuke.”
Au “Muumba wetu.”
Au “Hekalu letu la.”
Au “uzuri.”