Isaya 65:1-25

  • Hukumu ya Yehova dhidi ya wanaoabudu sanamu (1-16)

    • Mungu wa Bahati Njema na Mungu wa Majaliwa (11)

    • “Watumishi wangu watakula” (13)

  • Mbingu mpya na dunia mpya (17-25)

    • Kujenga nyumba; kupanda mashamba ya mizabibu (21)

    • Hakuna atakayefanya kazi ngumu bure (23)

65  “Nimeruhusu wale ambao hawakuuliza kunihusu wanitafute;Nimeruhusu wale ambao hawakunitafuta wanipate.+ Nililiambia taifa ambalo halikuwa linaliitia jina langu, ‘Nipo hapa, nipo hapa!’+   Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wakaidi,+Wale wanaotembea katika njia isiyo nzuri,+Wanaofuata mawazo yao wenyewe;+   Watu wanaonikasirisha daima mbele za uso wangu,+Wanaotoa dhabihu katika bustani+ na kufukiza moshi wa dhabihu kwenye matofali.   Wanaketi kati ya makaburi,+Nao wanakaa usiku kucha mafichoni,*Wakila nyama ya nguruwe,+Na mchuzi wa vitu vichafu* umo katika vyombo vyao.+   Wanasema, ‘Kaa peke yako; usinikaribie,Kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe.’* Hawa ni moshi katika mianzi ya pua yangu, moto unaowaka mchana kutwa.   Tazama! Imeandikwa mbele zangu;Sitasimama tuli,Lakini nitawalipa,+Nitawalipa kikamili*   Kwa ajili ya makosa yao na kwa ajili ya makosa ya mababu zao pia,”+ asema Yehova. “Kwa sababu wamefukiza moshi wa dhabihu juu ya milimaNao wamenishutumu juu ya vilima,+Kwanza nitawapimia malipo yao kamili.”*   Yehova anasema hivi: “Kama divai mpya inapopatikana katika kishada cha zabibuKisha mtu anasema, ‘Usikiharibu, kwa sababu kuna kitu kizuri* ndani yake,’ Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;Sitawaangamiza wote.+   Nitatoa uzao* katika YakoboNa katika Yuda mrithi wa milima yangu;+Watu wangu niliowachagua wataumiliki,Na watumishi wangu watakaa huko.+ 10  Sharoni+ itakuwa malisho ya kondooNa Bonde la* Akori+ mahali pa kupumzika pa ng’ombe,Kwa ajili ya watu wangu wanaonitafuta. 11  Lakini ninyi ni kati ya wale wanaomwacha Yehova,+Wanaousahau mlima wangu mtakatifu,+Wanaoandaa meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Njema,Na wale wanaovijaza vikombe divai iliyochanganywa kwa ajili ya mungu wa Majaliwa. 12  Basi nitawaamulia muuawe kwa upanga,+Nanyi nyote mtainama chini ili mchinjwe,+Kwa sababu niliita, lakini hamkuitika,Nilizungumza lakini hamkusikiliza;+Mliendelea kutenda maovu machoni pangu,Nanyi mkachagua mambo yaliyonichukiza.”+ 13  Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Tazama! Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mtakuwa na njaa.+ Tazama! Watumishi wangu watakunywa,+ lakini ninyi mtakuwa na kiu. Tazama! Watumishi wangu watashangilia,+ lakini ninyi mtaona aibu.+ 14  Tazama! Watumishi wangu watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya hali nzuri ya moyo,Lakini ninyi mtalia kwa sababu ya maumivu ya moyoNanyi mtaomboleza kwa sababu ya roho iliyovunjika. 15  Mtaacha jina ambalo watu wangu niliowachagua watalitumia kama laana,Na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atamuua kila mmoja wenu,Lakini atawaita watumishi wake mwenyewe kwa jina lingine;+ 16  Ili kila mtu anayejitafutia baraka dunianiAbarikiwe na Mungu wa kweli,*Na yeyote anayeapa kiapo dunianiAape kwa Mungu wa kweli;*+Kwa maana taabu za zamani zitasahauliwa;*Zitafichwa kutoka machoni pangu.+ 17  Kwa maana, tazama! ninaumba mbingu mpya na dunia mpya;+Na mambo ya zamani hayataingia tena akilini,*Wala hayataingia tena moyoni.+ 18  Basi furahini na kushangilia milele kwa sababu ya vitu ninavyoumba. Kwa maana tazama! ninaumba Yerusalemu kuwa sababu ya shangweNa watu wake kuwa sababu ya furaha.+ 19  Nami nitashangilia kwa sababu ya Yerusalemu na kufurahi kwa sababu ya watu wangu;+Sauti ya kulia na ya maombolezo kwa sababu ya taabu haitasikika tena ndani yake.”+ 20  “Hakutakuwemo tena ndani yake mtoto mchanga anayeishi siku chache tu,Wala mzee asiyetimiza siku zake. Kwa maana mtu anayekufa akiwa na miaka mia moja ataonwa kuwa mvulana tu,Na mtenda dhambi atalaaniwa, hata ingawa ana umri wa miaka mia moja.* 21  Watajenga nyumba na kuishi ndani yake,+Nao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 22  Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake,Wala hawatapanda na watu wengine wale. Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za mti,+Na watu wangu niliowachagua watafurahia kikamili kazi ya mikono yao. 23  Hawatafanya kazi* ya bure,+Wala hawatazaa watoto ili wataabike,Kwa sababu wao ni uzao wa* watu waliobarikiwa na Yehova,+Na wazao wao pamoja nao.+ 24  Hata kabla hawajaita, nitajibu;Wakiwa bado wanasema, nitasikia. 25  Mbwamwitu na mwanakondoo watalisha pamoja,Simba atakula majani kama ng’ombe dume,+Na chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Hawatadhuru wala kusababisha uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu,”+ asema Yehova.

Maelezo ya Chini

Au labda, “katika vibanda vya kukesha.”
Au “visivyo safi.”
Au labda, “Kwa maana nitakupa utakatifu wangu.”
Tnn., “katika vifua vyao.”
Tnn., “katika vifua vyao.”
Tnn., “kina baraka.”
Tnn., “mbegu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Au “uaminifu.” Tnn., “Amina.”
Au “uaminifu.” Tnn., “Amina.”
Au “matatizo ya zamani yatasahauliwa.”
Au “hayatakumbukwa.”
Au labda, “Na mtu yeyote asiyetimiza miaka mia moja ataonwa kuwa amelaaniwa.”
Au “kazi ngumu.”
Tnn., “mbegu ya.”