Isaya 66:1-24

  • Ibada ya kweli na ibada ya uwongo (1-6)

  • Sayuni na wanawe (7-17)

  • Watu wakusanyika Yerusalemu ili kuabudu (18-24)

66  Yehova anasema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha ufalme, na dunia ni kiti cha miguu yangu.+ Hivyo basi, iko wapi nyumba mnayoweza kunijengea,+Na pako wapi mahali pangu pa kupumzikia?”+   “Sasa mkono wangu mwenyewe uliumba vitu hivi vyote,Na vitu vyote vilikuja kuwapo kwa njia hiyo,” asema Yehova.+ “Basi, nitamtazama huyu,Yule aliye mnyenyekevu na aliyevunjika rohoni na anayelitetemekea* neno langu.+   Anayemchinja ng’ombe dume ni kama yule anayemuua mwanadamu.+ Anayemchinja kondoo ni kama yule anayevunja shingo ya mbwa.+ Anayetoa zawadi—kama damu ya nguruwe!+ Anayetoa toleo la ubani la ukumbusho+ ni kama yule anayebariki kwa maneno ya uchawi.*+ Wamechagua njia zao wenyewe,Nao wanapenda* mambo yanayochukiza.   Basi nitachagua njia za kuwaadhibu,+Nami nitawaletea mambo yaleyale wanayoogopa sana. Kwa sababu nilipoita, hakuna aliyejibu;Nilipozungumza, hakuna aliyesikiliza.+ Waliendelea kutenda maovu machoni pangu,Nao wakachagua kufanya mambo yaliyonichukiza.”+   Sikieni neno la Yehova, ninyi mnaolitetemekea* neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia na kuwatenga kwa sababu ya jina langu, walisema, ‘Yehova na atukuzwe!’+ Lakini atatokea na kuwaletea shangwe,Nao ndio watakaoaibishwa.”+   Kuna sauti ya ghasia kutoka jijini, sauti kutoka hekaluni! Ni sauti ya Yehova akiwalipa maadui wake kile wanachostahili.   Kabla hajawa na uchungu wa kuzaa, alizaa.+ Kabla ya kushikwa na uchungu wa kuzaa, alijifungua mtoto wa kiume.   Ni nani amewahi kusikia jambo kama hilo? Ni nani ameona mambo kama hayo? Je, nchi itazaliwa katika siku moja? Au, je, taifa lote litazaliwa mara moja? Hata hivyo, mara tu Sayuni aliposhikwa na uchungu wa kuzaa, aliwazaa wanawe.   “Je, nimfanye mtoto akaribie kuzaliwa kisha nifanye asizaliwe?” asema Yehova. “Au, je, nisababishe afikie hatua ya kuzaliwa kisha nifunge tumbo la uzazi?” asema Mungu wako. 10  Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi pamoja naye,+ ninyi nyote mnaompenda.+ Furahini sana pamoja naye, ninyi nyote mnaomwombolezea, 11  Kwa maana mtanyonya na kushiba kabisa maziwa ya titi lake la faraja,Nanyi mtakunywa sana na kufurahia utukufu wake mwingi. 12  Kwa maana Yehova anasema hivi: “Tazama, ninampa amani kama mto+Na utukufu wa mataifa kama mto unaofurika.+ Mtanyonya na kubebwa kiunoni,Nanyi mtachezeshwa kwenye magoti yake. 13  Kama mama anavyomfariji mwanawe,Ndivyo nitakavyoendelea kuwafariji;+Nanyi mtafarijiwa kwa sababu ya Yerusalemu.+ 14  Mtaona jambo hilo, na moyo wenu utashangilia,Mifupa yenu itanawiri kama majani mabichi. Na mkono wa Yehova utajulikana* kwa watumishi wake,Lakini atawashutumu maadui wake.”+ 15  “Kwa maana Yehova atakuja kama moto,+Na magari yake ya vita kama upepo wa dhoruba,+Ili kulipa kwa hasira kali,Ili kukemea kwa miali ya moto.+ 16  Kwa maana Yehova atatekeleza hukumu kwa moto,Naam, kwa upanga wake, dhidi ya wote wenye mwili;*Na watakaouawa na Yehova watakuwa wengi. 17  “Wale wanaojitakasa na kujisafisha ili waingie kwenye bustani*+ wakimfuata yule aliye katikati, wale wanaokula nyama ya nguruwe+ na vitu vinavyochukiza na panya,+ wote watafikia mwisho wao pamoja,” asema Yehova. 18  “Kwa kuwa ninajua kazi zao na mawazo yao, ninakuja kuwakusanya watu wa mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.” 19  “Nitaweka ishara miongoni mwao, nami nitawapeleka baadhi ya wale wanaoponyoka waende kwa mataifa—waende Tarshishi,+ Pulu, na Ludi,+ wale wanaouvuta upinde, waende Tubali na Yavani,+ na kwenye visiwa vilivyo mbali sana—mataifa ambayo hayajasikia habari kunihusu wala kuuona utukufu wangu; nao watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.+ 20  Watawaleta ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote+ wawe zawadi kwa Yehova, wakiwa juu ya farasi, ndani ya magari ya vita, ndani ya magari ya kukokotwa yaliyofunikwa, juu ya nyumbu, juu ya ngamia wenye kasi, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu, Yerusalemu,” asema Yehova, “kama watu wa Israeli wanavyoleta zawadi zao ndani ya nyumba ya Yehova zikiwa katika chombo safi.” 21  “Pia nitawachukua baadhi yao wawe makuhani na Walawi,” asema Yehova. 22  “Kwa maana kama vile mbingu mpya na dunia mpya+ ninazoumba zitakavyoendelea kusimama mbele zangu,” asema Yehova, “ndivyo uzao wenu* na jina lenu litakavyoendelea kudumu.”+ 23  “Na kutoka mwezi mpya mpaka mwezi mpya na kutoka sabato mpaka sabato,Wote wenye mwili* wataingia ili kuinama chini* mbele zangu,”+ asema Yehova. 24  “Nao watatoka nje na kuzitazama maiti za watu walioniasi;Kwa maana funza walio juu yao hawatakufa,Na moto wao hautazimwa,+Nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa watu wote.”*

Maelezo ya Chini

Au “anayelihangaikia.”
Au labda, “yule anayeisifu sanamu.”
Au “Na nafsi zao zinapenda.”
Au “mnaolihangaikia.”
Au “nguvu za Yehova zitajulikana.”
Au “wanadamu wote.”
Yaani, bustani za pekee zilizotumiwa kwa ajili ya ibada ya sanamu.
Tnn., “mbegu yenu.”
Au “Wanadamu wote.”
Au “kuabudu.”
Tnn., “wote wenye mwili.”