Isaya 7:1-25

  • Ujumbe kwa Mfalme Ahazi (1-9)

    • Shear-yashubu (3)

  • Ishara ya Imanueli (10-17)

  • Matokeo ya kutokuwa waaminifu (18-25)

7  Sasa katika siku za Ahazi+ mwana wa Yothamu mwana wa Uzia, mfalme wa Yuda, Mfalme Resini wa Siria na Peka+ mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, walipanda ili kuja kupigana vita dhidi ya Yerusalemu, lakini alishindwa* kuliteka.+  Habari ikapelekwa kwa nyumba ya Daudi: “Siria imeungana na Efraimu.” Na moyo wa Ahazi na moyo wa watu wake ukaanza kutetemeka, kama miti ya msituni inavyotikiswa na upepo.  Kisha Yehova akamwambia Isaya: “Tafadhali ondoka, wewe na mwana wako Shear-yashubu,*+ uende kukutana na Ahazi, kwenye mwisho wa mfereji* wa kidimbwi cha juu+ karibu na barabara kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.  Umwambie, ‘Jitahidi kuwa mtulivu. Usiogope, na usivunjike moyo kwa sababu ya haya magogo mawili yanayotoa moshi, kwa sababu ya hasira kali ya Resini na Siria na mwana wa Remalia.+  Kwa maana Siria pamoja na Efraimu na mwana wa Remalia wamepanga njama ya kukudhuru, wakisema:  “Na tupande dhidi ya Yuda na kuirarua* na kuishinda* iwe yetu, nasi tumweke mwana wa Tabeeli kuwa mfalme wake.”+   “‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Haitafanikiwa,Wala haitatimia.   Kwa maana kichwa cha Siria ni Damasko,Na kichwa cha Damasko ni Resini. Katika muda wa miaka 65 tuEfraimu litavunjwa kabisa na halitakuwa taifa tena.+   Kichwa cha Efraimu ni Samaria,+Na kichwa cha Samaria ni mwana wa Remalia.+ Msipokuwa na imani thabiti,Hamtakuwa imara.”’” 10  Yehova akaendelea kumwambia Ahazi: 11  “Mwombe Yehova Mungu wako+ ishara; inaweza kuwa yenye kina kama Kaburi* au iwe juu kama anga.” 12  Lakini Ahazi akasema: “Sitaomba, wala sitamjaribu Yehova.” 13  Kisha Isaya akasema: “Tafadhali, sikilizeni, enyi nyumba ya Daudi. Je, haitoshi kwamba mnaijaribu subira ya wanadamu? Je, ni lazima pia muijaribu subira ya Mungu?+ 14  Kwa hiyo Yehova mwenyewe atawapa ishara: Tazama! Mwanamke kijana* atapata mimba naye atazaa mwana,+ na kumwita jina Imanueli.*+ 15  Atakula siagi na asali kufikia wakati atakapojua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema. 16  Kwa maana kabla ya mvulana huyo kujua jinsi ya kukataa lililo baya na kuchagua lililo jema, nchi ya wale wafalme wawili mnaowahofu itaachwa kabisa.+ 17  Yehova ataleta dhidi yako na dhidi ya watu wako na dhidi ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuonekana tangu Efraimu lilipojitenga na Yuda,+ kwa maana Yeye atamleta mfalme wa Ashuru.+ 18  “Siku hiyo Yehova atawapigia mluzi nzi kutoka katika vijito vya mbali vya Mto Nile wa Misri na nyuki kutoka katika nchi ya Ashuru, 19  nao wote watakuja na kutua kwenye mabonde yenye mteremko mkali,* kwenye mipasuko ya miamba, kwenye vichaka vyote vya miiba, na sehemu zote za kunyweshea. 20  “Siku hiyo, kwa kutumia wembe uliokodiwa kutoka eneo la ule Mto,* kwa kumtumia mfalme wa Ashuru,+ Yehova atanyoa kichwa na nywele za miguu, nao utafagilia mbali ndevu pia. 21  “Siku hiyo mtu atamhifadhi hai ng’ombe mchanga aliye kundini na kondoo wawili. 22  Na kwa sababu ya wingi wa maziwa, atakula siagi, kwa maana kila mtu anayebaki katika nchi atakula siagi na asali. 23  “Siku hiyo mahali popote palipokuwa na mizabibu 1,000 yenye thamani ya vipande 1,000 vya fedha, patakuwa na vichaka vya miiba na magugu peke yake. 24  Watu wataenda huko wakiwa na mishale na upinde, kwa sababu nchi yote itakuwa vichaka vya miiba na magugu. 25  Na milima yote iliyokuwa ikilimwa kwa jembe, hutaikaribia kwa kuogopa vichaka vya miiba na magugu; itakuwa mahali pa kulisha ng’ombe na mahali pa kukanyagwa na kondoo.”

Maelezo ya Chini

Au labda, “walishindwa.”
Maana yake “Ni Mabaki tu Watakaorudi.”
Au “mtaro wa maji.”
Au labda, “kuishambulia.”
Au “bomoa kuta zake.” Tnn., “kulipasua.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Mwanamwali.”
Maana yake “Mungu Yuko Pamoja Nasi.”
Au “makorongo.”
Yaani, Mto Efrati.