Isaya 8:1-22

  • Usiogope⁠—“Mungu yuko pamoja nasi!” (9-17)

  • Isaya na watoto wake ni kama ishara (18)

  • Tafuteni habari katika sheria, si kwa roho waovu (19-22)

8  Yehova akaniambia: “Chukua bamba kubwa+ na uandike juu yake kwa kalamu ya kawaida,* ‘Maher-shalal-hash-bazi.’*  Nami nihakikishe kwamba limethibitishwa kwa maandishi* na mashahidi waaminifu, kuhani Uria+ na Zekaria mwana wa Yeberekia.”  Ndipo nikalala na* yule nabii wa kike,* naye akapata mimba na baada ya muda akazaa mwana.+ Kisha Yehova akaniambia: “Mwite jina Maher-shalal-hash-bazi,  kwa maana kabla mvulana huyo hajajua jinsi ya kuita, ‘Baba yangu!’ na ‘Mama yangu!’ mali za Damasko na nyara za Samaria zitachukuliwa mbele ya mfalme wa Ashuru.”+  Yehova akaniambia tena:   “Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya Shiloa* yanayotiririka polepole+Nao wanamshangilia Resini na mwana wa Remalia,+   Kwa hiyo tazama! Yehova ataleta dhidi yaoMaji yenye nguvu na yaliyo mengi ya ule Mto,*Mfalme wa Ashuru+ na utukufu wake wote. Atakuja juu ya sakafu zake zote za vijitoNa kufurika kwenye kingo zake zote   Na kupita katika nchi yote ya Yuda. Atafurika na kuvuka, na kufika shingoni;+Mabawa yake yaliyonyooshwa yatajaza upana wa nchi yako,Ewe Imanueli!”*+   Sababisheni madhara, enyi watu, lakini mtavunjwa vipandevipande. Sikilizeni, nyote mnaotoka sehemu za mbali za dunia! Jitayarisheni kwa ajili ya vita,* lakini mtavunjwa vipandevipande!+ Jitayarisheni kwa ajili ya vita, lakini mtavunjwa vipandevipande! 10  Fanyeni mpango, lakini utavunjwa! Semeni mnachotaka, lakini hakitafanikiwa,Kwa maana Mungu yuko pamoja nasi!*+ 11  Kwa mkono wake wenye nguvu ulio juu yangu, Yehova aliniambia hivi ili kunionya nisifuate njia ya watu hawa: 12  “Usikiite njama kitu ambacho watu hawa wanakiita njama! Usiogope kitu wanachoogopa;Usitetemeshwe nacho. 13  Yehova wa majeshi—Yeye ndiye mnayepaswa kumwona kuwa mtakatifu,+Yeye ndiye mnayepaswa kumwogopa,Na Yeye ndiye anayepaswa kuwatetemesha ninyi.”+ 14  Atakuwa kama mahali patakatifu,Lakini kama jiwe la kujigonga juu yakeNa kama mwamba wa kujikwaa juu yake+Kwa nyumba zote mbili za Israeli,Kama mtego na kama kitu kinachonasaKwa wakaaji wa Yerusalemu. 15  Wengi wao watajikwaa na kuanguka na kuvunjwa;Watanaswa na kukamatwa. 16  Funga ule uthibitisho ulioandikwa,*Tia muhuri sheria* kati ya wanafunzi wangu! 17  Nitaendelea kumtarajia* Yehova,+ ambaye anauficha uso wake kutoka kwa nyumba ya Yakobo,+ nami nitamtumainia. 18  Tazama! Mimi na watoto ambao Yehova amenipa+ ni kama ishara+ na kama miujiza katika Israeli kutoka kwa Yehova wa majeshi, anayekaa kwenye Mlima Sayuni. 19  Nao wakiwaambia: “Tafuteni habari kutoka kwa wale wanaowasiliana na roho au wabashiri wanaonong’oneza na kutoa sauti za chini,” je, watu hawapaswi kutafuta habari kutoka kwa Mungu wao? Je, wanapaswa kutafuta habari kutoka kwa wafu kwa ajili ya walio hai?+ 20  Badala yake, wanapaswa kutafuta habari katika sheria na uthibitisho ulioandikwa!* Wasiposema kulingana na neno hili, hawana nuru.*+ 21  Na kila mtu atapita katika nchi akiteseka na akiwa na njaa;+ na kwa sababu ana njaa na ghadhabu, atamtukana mfalme wake na Mungu wake huku akitazama juu. 22  Kisha ataiangalia dunia na kuona taabu na giza peke yake, gizagiza na nyakati ngumu, na utusitusi bila mwangaza.

Maelezo ya Chini

Huenda jina hili linamaanisha “Kuharakisha Kwenda Kwenye Nyara, Kuja Upesi Kwenye Nyara.”
Tnn., “kalamu ya mwanadamu anayeweza kufa.”
Au “limeshuhudiwa.”
Tnn., “nikamkaribia.”
Yaani, mke wa Isaya.
Shiloa ulikuwa mfereji wa maji.
Yaani, Mto Efrati.
Angalia Isa Isa 7:14.
Au “Jifungeni viuno.”
Katika Kiebrania maana ya neno Imanueli ni “Mungu yuko pamoja nasi.” Angalia Isa 7:14; 8:8.
Au “ushahidi.”
Au “mafundisho.”
Au “kumsubiri kwa hamu.”
Au “ushahidi.”
Tnn., “mapambazuko.”