Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kitabu cha Kumbukumbu la Torati

Sura

Muhtasari wa Yaliyomo

  • 1

    • Kuondoka Mlima Horebu (1-8)

    • Wakuu na waamuzi wawekwa (9-18)

    • Watu wakosa kutii kule Kadesh-barnea (19-46)

      • Waisraeli wakataa kuingia katika ile nchi (26-33)

      • Washindwa kuteka Kanaani (41-46)

  • 2

    • Kutangatanga nyikani kwa miaka 38 (1-23)

    • Wamshinda Mfalme Sihoni wa Heshboni (24-37)

  • 3

    • Wamshinda Mfalme Ogu wa Bashani (1-7)

    • Kugawanywa kwa nchi upande wa mashariki wa Yordani (8-20)

    • Yoshua aambiwa asiogope (21, 22)

    • Musa hataingia katika nchi hiyo (23-29)

  • 4

    • Waagizwa watii (1-14)

      • Msisahau matendo ya Mungu (9)

    • Yehova anataka aabudiwe yeye peke yake (15-31)

    • Hakuna Mungu mwingine ila Yehova (32-40)

    • Majiji ya makimbilio upande wa mashariki wa Yordani (41-43)

    • Wapewa Sheria (44-49)

  • 5

    • Agano la Yehova kule Horebu (1-5)

    • Amri Kumi zarudiwa (6-22)

    • Watu waogopa kwenye Mlima Sinai (23-33)

  • 6

    • Mpende Yehova kwa moyo wako wote (1-9)

      • “Sikilizeni, enyi Waisraeli” (4)

      • Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto (6, 7)

    • Msimsahau Yehova (10-15)

    • Msimjaribu Yehova (16-19)

    • Kiambieni kizazi kinachofuata (20-25)

  • 7

    • Mataifa saba yataangamizwa (1-6)

    • Sababu ya Waisraeli kuchaguliwa (7-11)

    • Utii utawaletea mafanikio wakati ujao (12-26)

  • 8

    • Baraka kutoka kwa Yehova zatajwa tena (1-9)

      • “Haishi kwa mkate tu” (3)

    • Msimsahau Yehova (10-20)

  • 9

    • Sababu ya Waisraeli kupewa ile nchi (1-6)

    • Waisraeli wamkasirisha Yehova mara nne (7-29)

      • Ndama wa dhahabu (7-14)

      • Musa aingilia kati (15-21, 25-29)

      • Wamkasirisha mara tatu zaidi (22)

  • 10

    • Mabamba mawili yatengenezwa tena (1-11)

    • Analotaka Yehova (12-22)

      • Mwogopeni na kumpenda Yehova (12)

  • 11

    • Mmeuona ukuu wa Yehova (1-7)

    • Nchi Iliyoahidiwa (8-12)

    • Thawabu za kutii (13-17)

    • Maneno ya Mungu yakaziwe katika mioyo (18-25)

    • “Baraka na laana” (26-32)

  • 12

    • Abuduni mahali ambapo Mungu amechagua (1-14)

    • Waruhusiwa kula nyama lakini si damu (15-28)

    • Msinaswe na miungu mingine (29-32)

  • 13

    • Jinsi ya kuwatendea waasi imani (1-18)

  • 14

    • Njia zisizofaa za kuomboleza (1, 2)

    • Vyakula safi na visivyo safi (3-21)

    • Sehemu ya kumi kwa ajili ya Yehova (22-29)

  • 15

    • Madeni yafutwa kila mwaka wa saba (1-6)

    • Kuwasaidia maskini (7-11)

    • Kuwaachilia huru watumwa kila mwaka wa saba (12-18)

      • Kutoboa sikio la mtumwa kwa msumari (16, 17)

    • Wazaliwa wa kwanza wa wanyama watakaswa (19-23)

  • 16

    • Pasaka; Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu (1-8)

    • Sherehe ya Majuma (9-12)

    • Sherehe ya Vibanda (13-17)

    • Kuwaweka waamuzi (18-20)

    • Vitu vya ibada vilivyokatazwa (21, 22)

  • 17

    • Dhabihu zisiwe na kasoro (1)

    • Kushughulikia uasi imani (2-7)

    • Kuamua kesi ngumu (8-13)

    • Maagizo kwa ajili ya mfalme atakayetawala (14-20)

      • Mfalme aandike nakala ya Sheria (18)

  • 18

    • Fungu la makuhani na Walawi (1-8)

    • Mazoea ya kuwasiliana na roho waovu yakatazwa (9-14)

    • Nabii kama Musa (15-19)

    • Jinsi ya kuwatambua manabii wa uwongo (20-22)

  • 19

    • Hatia ya damu na majiji ya makimbilio (1-13)

    • Alama za mipaka zisisogezwe (14)

    • Mashahidi mahakamani (15-21)

      • Mashahidi wawili au watatu wahitajika (15)

  • 20

    • Sheria za vita (1-20)

      • Wale ambao hawakuruhusiwa kwenda vitani (5-9)

  • 21

    • Mauaji yaliyofanywa na watu wasiojulikana (1-9)

    • Kuoa wanawake mateka (10-14)

    • Haki ya mzaliwa wa kwanza (15-17)

    • Mwana mkaidi (18-21)

    • Mtu aliyetundikwa mtini amelaaniwa (22, 23)

  • 22

    • Kuheshimu wanyama wa jirani (1-4)

    • Kuvaa nguo za watu wa jinsia tofauti (5)

    • Kuwatendea wanyama kwa fadhili (6, 7)

    • Ukuta unaozunguka ukingo wa paa (8)

    • Michanganyiko isiyofaa (9-11)

    • Vishada vya nguo (12)

    • Sheria kuhusu kukiuka maadili ya ngono (13-30)

  • 23

    • Wasioruhusiwa katika kutaniko la Mungu (1-8)

    • Usafi wa kambi (9-14)

    • Watumwa waliokimbia (15, 16)

    • Ukahaba wakatazwa (17, 18)

    • Riba na nadhiri (19-23)

    • Vitu ambavyo wapita njia wanaruhusiwa kula (24, 25)

  • 24

    • Ndoa na talaka (1-5)

    • Kuheshimu uhai (6-9)

    • Kuwajali maskini (10-18)

    • Sheria kuhusu kuokota masalio (19-22)

  • 25

    • Sheria kuhusu kumpiga mtu viboko (1-3)

    • Usimfunge kinywa ng’ombe dume anapopura (4)

    • Ndoa ya ndugu mkwe (5-10)

    • Kumkamata mtu sehemu zisizofaa anapopigana (11, 12)

    • Mizani na vipimo sahihi (13-16)

    • Waamaleki wataangamizwa (17-19)

  • 26

    • Kutoa mavuno ya kwanza (1-11)

    • Sehemu ya kumi iliyotolewa mara ya pili (12-15)

    • Waisraeli ni mali ya pekee ya Yehova (16-19)

  • 27

    • Sheria itaandikwa kwenye mawe (1-10)

    • Kwenye Mlima Ebali na Mlima Gerizimu (11-14)

    • Laana zatangazwa (15-26)

  • 28

    • Baraka za kutii (1-14)

    • Laana za kutotii (15-68)

  • 29

    • Agano pamoja na Waisraeli kule Moabu (1-13)

    • Onyo kuhusu kutotii (14-29)

      • Mambo yaliyofichwa, mambo yaliyofunuliwa (29)

  • 30

    • Kumrudia Yehova (1-10)

    • Amri za Yehova si ngumu sana (11-14)

    • Kuchagua kati ya uzima na kifo (15-20)

  • 31

    • Musa akaribia kufa (1-8)

    • Sheria yasomwa hadharani (9-13)

    • Yoshua awekwa kuwa kiongozi (14, 15)

    • Uasi wa Waisraeli watabiriwa (16-30)

      • Wimbo wa kuwafundisha Waisraeli (19, 22, 30)

  • 32

    • Wimbo wa Musa (1-47)

      • Yehova ni Mwamba (4)

      • Waisraeli wamsahau Mwamba wao (18)

      • “Kisasi ni changu” (35)

      • “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake” (43)

    • Musa atafia juu ya Mlima Nebo (48-52)

  • 33

    • Musa ayabariki makabila (1-29)

      • ‘Mikono ya milele’ ya Yehova (27)

  • 34

    • Yehova amwonyesha Musa ile nchi (1-4)

    • Kifo cha Musa (5-12)