Kumbukumbu la Torati 10:1-22

  • Mabamba mawili yatengenezwa tena (1-11)

  • Analotaka Yehova (12-22)

    • Mwogopeni na kumpenda Yehova (12)

10  “Wakati huo Yehova aliniambia, ‘Jichongee mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza,+ upande uje kwangu mlimani; jitengenezee pia sanduku la mbao.  Nami nitaandika kwenye mabamba hayo maneno yaliyokuwa kwenye yale mabamba ya kwanza ambayo uliyavunja, na uweke mabamba hayo ndani ya sanduku hilo.’  Kwa hiyo nikatengeneza sanduku kwa mbao za mshita na kuchonga mabamba mawili ya mawe kama yale ya kwanza na kupanda juu mlimani nikiwa nimebeba mabamba hayo mawili mkononi mwangu.+  Kisha akaandika kwenye mabamba hayo maneno aliyoandika mwanzoni,+ zile Amri Kumi,*+ ambazo Yehova aliwaambia mlimani kutoka katika moto+ siku ya kusanyiko;*+ Yehova akanipa mabamba hayo.  Basi nikageuka na kushuka kutoka mlimani+ na kuyaweka mabamba hayo katika sanduku nililokuwa nimetengeneza, na yangali humo, kama Yehova alivyokuwa ameniamuru.  “Kisha Waisraeli wakaondoka Beerothi Bene-yaakani na kwenda Mosera. Haruni akafa na kuzikwa huko,+ na Eleazari mwana wake akaanza kutumikia akiwa kuhani baada yake.+  Kutoka huko wakaelekea Gudgoda, na kutoka Gudgoda wakaelekea Yotbata,+ nchi yenye vijito vingi vya maji.  “Wakati huo Yehova aliliteua kabila la Lawi+ ili libebe sanduku la agano la Yehova,+ lisimame mbele za Yehova ili kumhudumia, na kubariki katika jina lake,+ kama linavyofanya mpaka leo.  Ndio maana Lawi hana fungu wala urithi pamoja na ndugu zake. Yehova ndiye urithi wake, kama Yehova Mungu wako alivyokuwa amemwambia.+ 10  Mimi mwenyewe nilikaa mlimani siku 40, mchana na usiku,+ kama nilivyofanya mwanzoni, na Yehova alinisikiliza wakati huo pia.+ Yehova hakutaka kuwaangamiza. 11  Kisha Yehova akaniambia, ‘Tangulia mbele ya watu, na mjitayarishe kuondoka, ili waingie na kuimiliki nchi ambayo nimewaapia mababu zao kwamba nitawapa.’+ 12  “Sasa, enyi Waisraeli, Yehova Mungu wenu anataka mfanye nini?+ Hili tu ndilo analotaka: mmwogope Yehova Mungu wenu,+ mtembee katika njia zake zote,+ mumpende, na kumtumikia Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 13  na kushika amri na sheria za Yehova ninazowaamuru leo kwa faida yenu wenyewe.+ 14  Tazameni, mbingu, hata mbingu za mbingu* ni mali ya Yehova Mungu wenu, pamoja na dunia na vitu vyote vilivyomo.+ 15  Lakini Yehova aliwakaribia na kudhihirisha upendo wake kwa mababu zenu tu, naye amewachagua ninyi, wazao wao,+ kutoka kati ya mataifa yote, kama mlivyo leo. 16  Ni lazima sasa msafishe*+ mioyo yenu na kuacha ukaidi.*+ 17  Kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu wa miungu+ na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye nguvu, na mwenye kuogopesha, asiyempendelea yeyote+ na hakubali rushwa. 18  Hutekeleza haki kwa ajili ya yatima na mjane+ na kumpenda mkaaji mgeni,+ humpa chakula na mavazi. 19  Ni lazima ninyi pia mumpende mkaaji mgeni, kwa maana mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+ 20  “Mnapaswa kumwogopa Yehova Mungu wenu, na kumtumikia yeye,+ mnapaswa kushikamana naye, nanyi mnapaswa kuapa kwa jina lake. 21  Yeye Ndiye mnayepaswa kumsifu.+ Yeye ni Mungu wenu, ambaye amewafanyia mambo haya makuu na yenye kuogopesha mliyoyaona kwa macho yenu wenyewe.+ 22  Mababu zenu waliposhuka kwenda Misri walikuwa watu* 70,+ na sasa Yehova Mungu wenu amewafanya muwe wengi kama nyota za mbinguni.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “yale Maneno Kumi.”
Au “kukutanika.”
Angalia Kamusi.
Au “mbingu zilizo juu zaidi.”
Tnn., “mtahiri govi la.”
Au “mwache kufanya shingo zenu kuwa ngumu.”
Au “nafsi.”