Kumbukumbu la Torati 13:1-18

  • Jinsi ya kuwatendea waasi imani (1-18)

13  “Ikiwa nabii au mtu anayebashiri kupitia ndoto atatokea miongoni mwenu na kuwapa ishara au dalili ya ajabu,  kisha ishara au dalili hiyo aliyowaambia itimie wakati anaposema, ‘Acheni tuifuate miungu mingine, miungu msiyoijua, na acheni tuiabudu,’  hampaswi kusikiliza maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue ikiwa mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+  Mnapaswa kumfuata Yehova Mungu wenu, mnapaswa kumwogopa yeye, mnapaswa kushika amri zake, mnapaswa kuisikiliza sauti yake; yeye ndiye mnayepaswa kumtumikia, nanyi mnapaswa kushikamana naye kabisa.+  Lakini nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto anapaswa kuuawa,+ kwa sababu aliwachochea mmwasi Yehova Mungu wenu—aliyewatoa nchini Misri na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa—ili mtoke katika njia ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mtembee. Nanyi lazima mwondoe kilicho kiovu kutoka miongoni mwenu.+  “Ikiwa ndugu yako, mwana wa mama yako, au mwana wako au binti yako au mke wako mpendwa au rafiki yako wa karibu sana* atajaribu kukushawishi kwa siri, akisema, ‘Twende tukaabudu miungu mingine,’+ miungu ambayo wewe wala mababu zako hamwijui,  kutoka miongoni mwa miungu ya mataifa yanayowazunguka, yaliyo karibu nanyi au mbali nanyi, kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho mwingine wa nchi,  usikubali ushawishi wake wala kumsikiliza,+ wala usimsikitikie wala kumhurumia wala kumlinda;  badala yake, ni lazima umuue.+ Mkono wako unapaswa kuwa wa kwanza kumuua, kisha mikono ya watu wote itafuata.+ 10  Nawe lazima umuue kwa kumpiga mawe,+ kwa sababu alijaribu kukugeuza umwache Yehova Mungu wako, aliyekutoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa. 11  Hivyo, Waisraeli wote watasikia na kuogopa, na kamwe hawatafanya tena jambo lolote baya kama hilo miongoni mwenu.+ 12  “Ikiwa mtasikia ikisemwa hivi katika mojawapo ya majiji yenu ambayo Yehova Mungu wenu anawapa mkae humo: 13  ‘Watu wasiofaa kitu wametokea miongoni mwenu ili kuwapotosha wakaaji wa jiji lao, wakisema, “Twendeni tukaabudu miungu mingine,” miungu ambayo hamwijui,’ 14  mnapaswa kupeleleza jambo hilo, kufanya uchunguzi kamili na kuuliza kwa makini;+ na ikithibitishwa ni kweli kwamba jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa miongoni mwenu, 15  ni lazima muwaangamize kwa upanga wakaaji wa jiji hilo.+ Mtawaangamiza+ kwa upanga watu wa jiji hilo pamoja na kila kitu kilichomo, kutia ndani mifugo yao. 16  Kisha mtakusanya nyara zote za jiji hilo katikati ya uwanja wa jiji na kuliteketeza jiji hilo kwa moto, na nyara hizo zitakuwa dhabihu nzima ya kuteketezwa kwa Yehova Mungu wenu. Nalo litabaki rundo la magofu milele. Halipaswi kamwe kujengwa tena. 17  Mikono yenu haipaswi kuchukua kitu chochote kinachopaswa kuharibiwa,*+ ili Yehova aache hasira yake kali na kuwaonyesha rehema na huruma na kuwafanya mwongezeke, kama alivyowaapia mababu zenu.+ 18  Kwa maana mnapaswa kumtii* Yehova Mungu wenu kwa kushika amri zake zote ambazo ninawaamuru leo, na hivyo kufanya yaliyo sawa machoni pa Yehova Mungu wenu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “rafiki yako ambaye ni kama nafsi yako mwenyewe.”
Au “kilichofanywa kitakatifu kwa kupigwa marufuku.”
Au “kusikiliza sauti ya.”