Kumbukumbu la Torati 14:1-29

  • Njia zisizofaa za kuomboleza (1, 2)

  • Vyakula safi na visivyo safi (3-21)

  • Sehemu ya kumi kwa ajili ya Yehova (22-29)

14  “Ninyi ni wana wa Yehova Mungu wenu. Msijikatekate+ wala kunyoa upara kwenye mapaji ya nyuso zenu* kwa ajili ya mtu aliyekufa.+  Kwa maana ninyi ni watu watakatifu+ kwa Yehova Mungu wenu, na Yehova amewachagua ninyi muwe watu wake, mali yake ya pekee,* kutoka kati ya mataifa yote duniani.+  “Msile kitu chochote kinachochukiza.+  Hawa ndio wanyama mnaoweza kula:+ ng’ombe, kondoo, mbuzi,  paa, swala, kulungu, mbuzi mwitu, mbawala, kondoo mwitu, na kondoo wa mlimani.  Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizopasuka na zilizogawanyika mara mbili na ambaye anacheua.  Lakini hampaswi kuwala wanyama wafuatao wanaocheua au wenye kwato zilizogawanyika: ngamia, sungura, na wibari, kwa sababu wanacheua lakini kwato zao hazijapasuka. Wao si safi kwenu.+  Pia, msimle nguruwe kwa sababu ana kwato zilizopasuka lakini hacheui. Yeye si safi kwenu. Msile kamwe nyama yao wala kugusa mizoga yao.  “Kati ya viumbe wote wanaoishi ndani ya maji, mnaweza kula wafuatao: Mnaweza kumla kiumbe yeyote mwenye mapezi na magamba.+ 10  Lakini hampaswi kumla kiumbe yeyote ambaye hana mapezi na magamba. Yeye si safi kwenu. 11  “Mnaweza kumla ndege yeyote aliye safi. 12  Lakini hampaswi kuwala ndege wafuatao: tai, furukombe, tumbusi mweusi,*+ 13  mwewe mwekundu, mwewe mweusi, kila aina ya ndege mbua, 14  kila aina ya kunguru, 15  mbuni, bundi, shakwe, kila aina ya kipanga, 16  bundi mdogo, bundi mwenye masikio marefu, batamaji, 17  mwari, tumbusi, mnandi, 18  korongo, kila aina ya kulastara, hudihudi, na popo. 19  Pia, kila kiumbe* mwenye mabawa anayeishi katika makundi makubwa si safi kwenu. Hawapaswi kuliwa. 20  Mnaweza kumla kiumbe yeyote safi anayeruka. 21  “Msimle mnyama yeyote aliyepatikana amekufa.+ Mnaweza kumpa mkaaji mgeni aliye ndani ya majiji yenu,* naye anaweza kumla, au mnyama huyo anaweza kuuzwa kwa mgeni. Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu. “Msimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.+ 22  “Ni lazima mtoe sehemu ya kumi ya mazao ya shambani yanayotokana na mbegu zenu mwaka baada ya mwaka.+ 23  Mtakula sehemu ya kumi ya nafaka yenu, divai yenu mpya, mafuta yenu, na wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe wenu na kondoo wenu mbele za Yehova Mungu wenu mahali ambapo atachagua jina lake likae hapo,+ ili mjifunze kumwogopa Yehova Mungu wenu sikuzote.+ 24  “Lakini ikiwa safari ni ndefu sana kwenu na hivyo hamwezi kupeleka vitu hivyo mahali ambapo Yehova Mungu wenu amechagua jina lake likae hapo,+ kwa sababu ni mbali sana (kwa sababu Yehova Mungu wenu atawabariki), 25  basi mnaweza kubadilisha vitu hivyo kwa pesa, na mbebe pesa hizo mikononi mwenu na kwenda mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua. 26  Kisha mnaweza kutumia pesa hizo kununua chochote mnachotamani, iwe ni ng’ombe, kondoo, mbuzi, divai na vinywaji vingine vyenye kileo, na kitu chochote mpendacho; nanyi mtakula huko mbele za Yehova Mungu wenu na kushangilia, ninyi na familia zenu.+ 27  Na msimpuuze Mlawi yeyote aliye ndani ya majiji yenu,+ kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+ 28  “Mwishoni mwa kila miaka mitatu mnapaswa kuleta sehemu yote ya kumi ya mazao yenu ya mwaka huo na kuyahifadhi ndani ya majiji yenu.+ 29  Kisha Mlawi, ambaye hana fungu wala urithi kati yenu, mkaaji mgeni, yatima, na mjane aliye ndani ya majiji yenu atakuja kula na kushiba,+ ili Yehova Mungu wenu awabariki katika mambo yote mnayofanya.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutia (kunyoa) upara katikati ya macho yenu.”
Au “mali yake anayothamini sana.”
Au “tai mla mizoga.”
Au “mdudu.”
Tnn., “malango.”