Kumbukumbu la Torati 16:1-22

  • Pasaka; Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu (1-8)

  • Sherehe ya Majuma (9-12)

  • Sherehe ya Vibanda (13-17)

  • Kuwaweka waamuzi (18-20)

  • Vitu vya ibada vilivyokatazwa (21, 22)

16  “Adhimisheni mwezi wa Abibu* na msherehekee Pasaka ya Yehova Mungu wenu,+ kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Yehova Mungu wenu aliwatoa nchini Misri wakati wa usiku.+  Nanyi mnapaswa kumtolea Yehova Mungu wenu dhabihu ya Pasaka+ kutoka katika kondoo wenu na ng’ombe wenu,+ mahali ambapo Yehova atachagua jina lake likae hapo.+  Hampaswi kula kitu chochote chenye chachu pamoja na dhabihu hiyo;+ kwa siku saba mnapaswa kula mikate isiyo na chachu, mikate ya mateso, kwa sababu mlitoka haraka katika nchi ya Misri.+ Fanyeni hivyo sikuzote za maisha yenu ili mkumbuke siku mliyotoka katika nchi ya Misri.+  Msipatikane na unga wowote uliokandwa wenye chachu katika nchi yenu yote kwa siku saba,+ wala nyama yoyote mtakayotoa dhabihu siku ya kwanza jioni haipaswi kubaki usiku kucha mpaka asubuhi.+  Hamtaruhusiwa kutoa dhabihu ya Pasaka katika jiji lolote tu kati ya majiji ambayo Yehova anawapa ninyi.  Bali mtafanya hivyo mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae hapo. Mnapaswa kutoa dhabihu ya Pasaka wakati wa jioni mara tu baada ya jua kutua,+ wakati uleule mliotoka Misri.  Mtaipika na kuila+ mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua,+ na asubuhi mtarudi kwenye mahema yenu.  Kwa siku sita mtakula mikate isiyo na chachu, na siku ya saba kutakuwa na kusanyiko takatifu kwa Yehova Mungu wenu. Hampaswi kufanya kazi yoyote.+  “Mtahesabu majuma saba. Mnapaswa kuanza kuhesabu majuma saba wakati mnapoanza kuvuna kwa mundu nafaka iliyo shambani.+ 10  Kisha mtafanya Sherehe ya Majuma kwa Yehova Mungu wenu+ kwa toleo la hiari linalotoka mkononi mwenu, kulingana na baraka ambazo Yehova Mungu wenu amewapa.+ 11  Nanyi mnapaswa kushangilia mbele za Yehova Mungu wenu, ninyi na wana wenu, mabinti wenu, watumwa wenu wa kiume, vijakazi wenu, Walawi walio ndani ya majiji* yenu, wakaaji wageni, mayatima, na wajane walio kati yenu, mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae.+ 12  Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa Misri,+ nanyi mshike na kutekeleza masharti haya. 13  “Mnapaswa kufanya Sherehe ya Vibanda*+ kwa siku saba mnapokusanya nafaka kutoka katika uwanja wenu wa kupuria na kutoka katika shinikizo lenu la mafuta na divai. 14  Shangilieni wakati wa sherehe yenu,+ ninyi na wana wenu, mabinti wenu, watumwa wenu wa kiume, vijakazi wenu, Walawi, wakaaji wageni, mayatima, na wajane walio ndani ya majiji yenu. 15  Kwa siku saba mtamfanyia Yehova Mungu wenu sherehe+ mahali ambapo Yehova atachagua, kwa kuwa Yehova Mungu wenu atabariki mazao yenu yote na kila jambo mnalofanya,+ nanyi mtakuwa na shangwe kwelikweli.+ 16  “Mara tatu kwa mwaka, wanaume wenu wote wanapaswa kwenda mbele za Yehova Mungu wenu mahali atakapochagua: katika Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu,+ Sherehe ya Majuma,+ na Sherehe ya Vibanda,*+ na hakuna yeyote kati yao anayepaswa kwenda mbele za Yehova mikono mitupu. 17  Zawadi ambayo kila mtu ataleta inapaswa kulingana na baraka ambazo Yehova Mungu wenu amempa.+ 18  “Mnapaswa kuwaweka waamuzi+ na maofisa kwa ajili ya kila kabila katika majiji yenu yote ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, nao lazima wawahukumu watu kwa hukumu ya uadilifu. 19  Msipotoshe haki,+ msipendelee,+ wala kukubali rushwa, kwa maana rushwa hupofusha macho ya wenye hekima+ na hupotosha maneno ya waadilifu. 20  Haki—mnapaswa kufuatia haki,+ ili mwendelee kuishi na kumiliki nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa ninyi. 21  “Msipande mti wa aina yoyote na kuufanya kuwa mti mtakatifu*+ karibu na madhabahu ya Yehova Mungu wenu ambayo mtajitengenezea. 22  “Wala hampaswi kujisimamishia nguzo takatifu,+ kitu ambacho Yehova Mungu wenu anachukia.

Maelezo ya Chini

Tnn., “malango.”
Au “Vibanda vya Muda.”
Au “Vibanda vya Muda.”
Angalia Kamusi.