Kumbukumbu la Torati 2:1-37

  • Kutangatanga nyikani kwa miaka 38 (1-23)

  • Wamshinda Mfalme Sihoni wa Heshboni (24-37)

2  “Kisha tukageuka na kwenda nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu, kama Yehova alivyoniambia,+ nasi tulizunguka-zunguka Mlima Seiri kwa siku nyingi.  Mwishowe Yehova akaniambia hivi:  ‘Mmeuzunguka-zunguka mlima huu kwa muda mrefu vya kutosha. Sasa geukeni mwelekee kaskazini.  Nawe uwaamuru watu hivi: “Mtapita karibu na mpaka wa ndugu zenu, wazao wa Esau,+ wanaokaa Seiri,+ nao watawaogopa ninyi,+ basi mnapaswa kuwa waangalifu sana.  Msizozane nao,* kwa sababu sitawapa sehemu yoyote ya nchi yao, hata mahali panapotoshea wayo wa mguu, kwa sababu nimempa Esau Mlima Seiri uwe miliki yake.+  Mnapaswa kuwalipa pesa kwa ajili ya chakula mtakachokula, nanyi mnapaswa kulipia maji mtakayokunywa.+  Kwa maana Yehova Mungu wenu amewabariki katika mambo yote mliyofanya. Anajua vizuri kabisa safari yenu katika nyika hii kubwa. Yehova Mungu wenu amekuwa pamoja nanyi kwa miaka hii 40, nanyi hamjakosa kitu chochote.”’+  Basi tuliwapita ndugu zetu, wazao wa Esau,+ wanaokaa Seiri, tukaepuka njia ya Araba, kutoka Elathi na kutoka Esion-geberi.+ “Kisha tukageuka na kupitia njia ya nyika ya Moabu.+  Ndipo Yehova akaniambia, ‘Msizozane wala kupigana na Wamoabu, kwa sababu sitawapa ninyi sehemu yoyote ya nchi yao ili mwimiliki kwa sababu nimewapa wazao wa Loti+ nchi ya Ari ili waimiliki. 10  (Waemi+ waliishi katika nchi hiyo zamani, walikuwa watu wenye nguvu na wengi sana na warefu kama Waanaki. 11  Warefaimu+ pia walionwa kama Waanaki,+ na Wamoabu walikuwa wakiwaita Waemi. 12  Awali, Wahori+ waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau walimiliki nchi yao, wakawaangamiza na kukaa humo badala yao,+ kama Waisraeli watakavyofanya katika nchi ambayo ni miliki yao, ambayo kwa hakika Yehova atawapa.) 13  Sasa nendeni mvuke Bonde* la Zeredi.’ Basi tukavuka Bonde la Zeredi.+ 14  Tulitembea kwa miaka 38 kutoka Kadesh-barnea mpaka tulipovuka Bonde la Zeredi, mpaka kizazi chote cha wanaume wa vita kilipoangamia kutoka kambini, kama Yehova alivyokuwa amewaapia.+ 15  Mkono wa Yehova uliwapinga ili kuwaangamiza kutoka kambini mpaka walipoisha.+ 16  “Mara tu wanaume wote wa vita walipokufa,+ 17  Yehova akazungumza nami tena, akaniambia, 18  ‘Leo mtapita karibu na eneo la Moabu, yaani, Ari. 19  Mtakapofika karibu na Waamoni, msiwachokoze wala kuzozana nao, kwa sababu sitawapa ninyi nchi yoyote ya Waamoni ili mwimiliki, kwa kuwa nimewapa wazao wa Loti waimiliki.+ 20  Nchi hiyo pia ilionwa kuwa nchi ya Warefaimu.+ (Warefaimu waliishi katika nchi hiyo zamani, na Waamoni walikuwa wakiwaita Wazamzumi. 21  Walikuwa watu wenye nguvu na wengi sana na warefu kama Waanaki;+ lakini Yehova aliwasaidia Waamoni kuwaangamiza, Waamoni wakawafukuza na kuishi humo badala yao. 22  Hivyo ndivyo alivyofanya kwa ajili ya wazao wa Esau, ambao sasa wanakaa Seiri,+ alipowaangamiza Wahori+ kutoka mbele yao, ili wamiliki nchi yao na kukaa humo badala yao mpaka leo. 23  Nao Waavi, walikuwa wakiishi katika vijiji vilivyofika Gaza,+ mpaka Wakaftori waliotoka Kaftori*+ walipokuja na kuwaangamiza na kukaa humo badala yao.) 24  “‘Ondokeni, mvuke Bonde* la Arnoni.+ Tazameni nimemtia mikononi mwenu Sihoni+ Mwamori, mfalme wa Heshboni. Basi anzeni kumiliki nchi yake, nanyi mpigane vita naye. 25  Siku ya leo nitaanza kuwafanya watu wote duniani* wanaosikia habari zenu wawahofu na kuwaogopa ninyi. Watakuwa na wasiwasi na kutetemeka* kwa sababu yenu.’+ 26  “Kisha kutoka katika nyika ya Kedemothi,+ niliwatuma wajumbe kwa Mfalme Sihoni wa Heshboni, ili wampe ujumbe huu wa amani:+ 27  ‘Niruhusu nipite katika nchi yako. Nitatembea barabarani tu, sitakwenda kulia wala kushoto.+ 28  Nitakula tu chakula na kunywa tu maji utakayoniuzia. Niruhusu tu nipite kwa miguu, 29  hivyo ndivyo wazao wa Esau wanaokaa Seiri na Wamoabu wanaokaa Ari walivyonifanyia, mpaka nitakapovuka Yordani na kuingia nchi ambayo Yehova Mungu wetu anatupa sisi.’ 30  Lakini Mfalme Sihoni wa Heshboni hakuturuhusu tupite, kwa sababu Yehova Mungu wenu alimwacha awe na roho ya ukaidi+ na moyo wake uwe mgumu, ili amtie mikononi mwenu kama ilivyo leo.+ 31  “Kisha Yehova akaniambia, ‘Angalieni, tayari nimeanza kumtia mikononi mwenu Sihoni pamoja na nchi yake. Anzeni kuimiliki nchi yake.’+ 32  Sihoni alipotoka na watu wake wote ili kupigana nasi kule Yahazi,+ 33  Yehova Mungu wetu alimtia mikononi mwetu, hivi kwamba tukamshinda yeye, wanawe, na watu wake wote. 34  Tuliteka majiji yake yote wakati huo na kuangamiza kila jiji, pamoja na wanaume, wanawake, na watoto. Hatukumwacha mtu yeyote akiwa hai.+ 35  Tulijichukulia tu mifugo pamoja na nyara za majiji tuliyokuwa tumeteka. 36  Kuanzia Aroeri,+ jiji lililo kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni (pamoja na jiji lililo bondeni), mpaka Gileadi, hakuna mji wowote ambao hatungeweza kuuteka. Yehova Mungu wetu aliitia yote mikononi mwetu.+ 37  Hata hivyo, hamkukaribia nchi ya Waamoni,+ ukingo wote wa Bonde* la Yaboki+ na majiji yaliyo kwenye eneo lenye milima, wala eneo lingine lolote tulilokatazwa na Yehova Mungu wetu.

Maelezo ya Chini

Au “Msiwachokoze.”
Au “Korongo.”
Yaani, Krete.
Au “Korongo.”
Tnn., “walio chini ya mbingu.”
Au “watakuwa na uchungu kama wa kuzaa.”
Au “Korongo.”
Au “Korongo.”