Kumbukumbu la Torati 26:1-19

  • Kutoa mavuno ya kwanza (1-11)

  • Sehemu ya kumi iliyotolewa mara ya pili (12-15)

  • Waisraeli ni mali ya pekee ya Yehova (16-19)

26  “Mwishowe mtakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa kuwa urithi wenu, nanyi mmeimiliki na mnaishi ndani yake,  mtachukua baadhi ya mavuno ya kwanza ya mazao* yote ya ardhi, mtakayokusanya katika nchi yenu ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, na kuyatia katika kikapu na kwenda mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae hapo.+  Mtaenda kwa kuhani atakayekuwa akihudumu wakati huo na kumwambia, ‘Leo nimekuja kumjulisha Yehova Mungu wako kwamba nimeingia katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zetu kwamba atatupa sisi.’+  “Kisha kuhani atachukua kikapu hicho kutoka mkononi mwako na kukiweka mbele ya madhabahu ya Yehova Mungu wako.  Halafu utatangaza hivi mbele za Yehova Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Mwaramu aliyekuwa akitangatanga,*+ akashuka kwenda Misri+ na kukaa huko akiwa mgeni, akiwa na watu wachache wa familia yake.+ Lakini huko akawa taifa kubwa, lenye nguvu na lenye watu wengi.+  Na Wamisri wakatutesa na kutukandamiza na kututumikisha kikatili.+  Basi tukaanza kumlilia Yehova, Mungu wa mababu zetu, naye Yehova akasikia sauti yetu na kutazama mateso yetu na taabu yetu na kukandamizwa kwetu.+  Mwishowe Yehova akatutoa Misri kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa+ na kwa matendo yanayotisha na kwa ishara na miujiza.+  Kisha akatuleta mahali hapa na kutupatia nchi hii, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 10  Sasa nimeleta mavuno ya kwanza ya mazao ya ardhi ambayo Yehova amenipa.’+ “Ni lazima ukiweke kikapu hicho mbele za Yehova Mungu wako na kuinama mbele za Yehova Mungu wako. 11  Kisha utashangilia kwa sababu ya vitu vyote vyema ambavyo Yehova Mungu wako amekupa wewe na nyumba yako, wewe na Mlawi na mkaaji mgeni aliye miongoni mwenu.+ 12  “Baada ya kutoa sehemu yote ya kumi+ ya mazao yako katika mwaka wa tatu, mwaka wa sehemu ya kumi, utampa sehemu hiyo Mlawi, mkaaji mgeni, yatima, na mjane, nao watakula na kushiba katika majiji*+ yenu. 13  Kisha utasema hivi mbele za Yehova Mungu wako: ‘Nimeondoa sehemu takatifu kutoka katika nyumba yangu na kumpa Mlawi, mkaaji mgeni, yatima, na mjane,+ kama ulivyoniamuru. Sijavunja wala kupuuza amri zako. 14  Sikuila nikiomboleza wala kutoa kisehemu chochote nikiwa mchafu au kutoa kisehemu chochote kwa ajili ya wafu. Nimetii sauti ya Yehova Mungu wangu na kufanya mambo yote uliyoniamuru. 15  Sasa tazama chini kutoka katika makao yako matakatifu, mbinguni, na kuwabariki watu wako Waisraeli na nchi ambayo umetupatia,+ kama ulivyowaapia mababu zetu,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.’+ 16  “Siku ya leo Yehova Mungu wako anakuamuru utekeleze masharti haya na sheria hizi.* Ni lazima uzishike na kuzitekeleza kwa moyo wako wote+ na nafsi* yako yote. 17  Leo Yehova amewatangazia kwamba atakuwa Mungu wenu mnapotembea katika njia zake na kushika masharti yake,+ amri zake,+ na sheria zake,*+ na mnaposikiliza sauti yake. 18  Na leo mmemtangazia Yehova kwamba mtakuwa watu wake, mali yake ya pekee,*+ kama alivyowaahidi, na kwamba mtashika amri zake zote 19  na kwamba atawakweza juu ya mataifa mengine yote ambayo ameyatokeza,+ akiwapa sifa na umaarufu na utukufu mnapothibitisha kwamba ninyi ni taifa takatifu kwa Yehova Mungu wenu,+ kama alivyoahidi.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “matunda.”
Au labda, “akiangamia.”
Tnn., “malango.”
Tnn., “maamuzi haya ya hukumu.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “maamuzi yake ya hukumu.”
Au “mali yake anayothamini sana.”