Kumbukumbu la Torati 31:1-30

  • Musa akaribia kufa (1-8)

  • Sheria yasomwa hadharani (9-13)

  • Yoshua awekwa kuwa kiongozi (14, 15)

  • Uasi wa Waisraeli watabiriwa (16-30)

    • Wimbo wa kuwafundisha Waisraeli (19, 22, 30)

31  Ndipo Musa akatoka na kuwaambia Waisraeli wote maneno haya:  “Leo nina umri wa miaka 120.+ Siwezi tena kuwaongoza,* kwa sababu Yehova ameniambia, ‘Hutavuka mto huu wa Yordani.’+  Yehova Mungu wenu ndiye anayevuka mbele yenu, naye mwenyewe atayaangamiza mataifa haya kutoka mbele yenu, nanyi mtayafukuza.+ Yoshua ndiye atakayewaongoza kuvuka,+ kama Yehova alivyosema.  Yehova atayatendea kama alivyowatendea Sihoni+ na Ogu,+ wafalme wa Waamori, na nchi yao, alipowaangamiza.+  Yehova atawashinda kwa niaba yenu, mtawatendea kulingana na amri yote ambayo nimewapa.+  Iweni jasiri na imara.+ Msiogope wala msiwe na hofu mbele yao,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu ndiye anayepiga mwendo pamoja nanyi. Hatawatupa wala kuwaacha.”+  Kisha Musa akamwita Yoshua na kumwambia hivi mbele ya Waisraeli wote: “Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaingiza watu hawa katika nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zao kwamba atawapa, nawe utawapa iwe urithi wao.+  Yehova ndiye anayepiga mwendo mbele yako, naye ataendelea kuwa pamoja nawe.+ Hatakutupa wala kukuacha. Usiogope wala usihofu.”+  Ndipo Musa akaandika Sheria hii+ na kuwapa makuhani, Walawi, ambao wanabeba sanduku la agano la Yehova, na wazee wote wa Israeli. 10  Musa akawaamuru hivi: “Mwishoni mwa kila miaka saba, wakati uliowekwa katika mwaka wa kufuta madeni,+ wakati wa Sherehe ya Vibanda,*+ 11  Waisraeli wote wanapokuja mbele za Yehova+ Mungu wao mahali anapochagua, unapaswa kuisoma Sheria hii mbele ya Waisraeli wote ili waisikie.+ 12  Wakusanye watu pamoja,+ wanaume, wanawake, watoto,* na mkaaji mgeni aliye katika majiji* yenu, ili wasikilize na kujifunza kumhusu Yehova Mungu wenu na kumwogopa yeye na kuwa waangalifu kutekeleza maneno yote ya Sheria hii. 13  Ndipo wana wao ambao hawajui Sheria hii watasikiliza+ na kujifunza kumwogopa Yehova Mungu wenu sikuzote ambazo mtaishi katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.”+ 14  Kisha Yehova akamwambia Musa, “Tazama! Wakati wako wa kufa umekaribia.+ Mwite Yoshua, nanyi mwende* kwenye hema la mkutano, ili nimweke yeye kuwa kiongozi.”+ Basi Musa na Yoshua wakaenda na kusimama kwenye hema la mkutano. 15  Ndipo Yehova akatokea pale hemani katika nguzo ya wingu, na nguzo hiyo ya wingu ikasimama karibu na mlango wa hema.+ 16  Sasa Yehova akamwambia Musa hivi: “Tazama! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na miungu ya kigeni inayowazunguka katika nchi wanayoenda.+ Wataniacha na kuvunja agano langu+ ambalo nimefanya pamoja nao.+ 17  Wakati huo hasira yangu itawaka dhidi yao,+ nami nitawaacha+ na kuuficha uso wangu wasiuone+ mpaka watakapoangamia. Kisha baada ya kupatwa na misiba na mateso mengi,+ watasema, ‘Je, hatujapatwa na misiba hii kwa sababu Mungu wetu hayuko miongoni mwetu?’+ 18  Lakini nitaendelea kuuficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yote waliyotenda kwa kuigeukia miungu mingine.+ 19  “Sasa jiandikieni wimbo huu+ na kuwafundisha Waisraeli.+ Hakikisheni kwamba wanajifunza wimbo huu* ili uwe ushahidi wangu dhidi ya Waisraeli.+ 20  Nitakapowaleta katika nchi ambayo niliwaapia mababu zao+—nchi inayotiririka maziwa na asali+—nao wale na kushiba na kufanikiwa,*+ wataigeukia miungu mingine na kuiabudu na kunidharau na kulivunja agano langu.+ 21  Watakapopatwa na misiba na mateso mengi,+ wimbo huu utakuwa ushahidi kwao (kwa sababu wazao wao hawapaswi kuusahau), kwa sababu tayari ninajua mwelekeo ambao wamesitawisha+ hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaapia.” 22  Basi Musa akaandika wimbo huu siku hiyo na kuwafundisha Waisraeli kuuimba. 23  Kisha akamweka* Yoshua+ mwana wa Nuni kuwa kiongozi na kusema: “Uwe jasiri na imara,+ kwa sababu ni wewe utakayewaingiza Waisraeli katika nchi ambayo nimewaapia,+ nami nitaendelea kuwa pamoja nawe.” 24  Mara tu Musa alipomaliza kuandika maneno yote ya Sheria hii katika kitabu,+ 25  Musa akawaamuru hivi Walawi wanaobeba sanduku la agano la Yehova: 26  “Chukueni kitabu hiki cha Sheria+ mkiweke kando ya sanduku+ la agano la Yehova Mungu wenu, nacho kitakuwa ushahidi dhidi yenu mahali hapo. 27  Kwa maana mimi mwenyewe najua vizuri uasi wenu+ na ukaidi wenu.*+ Ikiwa mmekuwa mkimwasi sana Yehova ningali hai pamoja nanyi, basi mtamwasi kadiri gani nikifa? 28  Nikusanyieni wazee wote wa makabila yenu na maofisa wenu, acheni niwaambie maneno haya wasikie, na acheni nichukue mbingu na dunia ziwe mashahidi dhidi yao.+ 29  Kwa maana najua vizuri kwamba baada ya kifo changu hakika mtatenda maovu+ na kuacha njia ambayo nimewaamuru ninyi. Na bila shaka mtapatwa na msiba+ siku zijazo, kwa sababu mtatenda maovu machoni pa Yehova, nanyi mtamkasirisha kwa kazi za mikono yenu.” 30  Kisha mbele ya Waisraeli wote, Musa akasema maneno ya wimbo huu kuanzia mwanzo mpaka mwisho:+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoka nje na kuingia ndani.”
Au “Vibanda vya Muda.”
Tnn., “watoto wachanga.”
Tnn., “malango.”
Au “mchukue nafasi zenu.”
Tnn., “kulala na baba zako.”
Tnn., “Utieni katika vinywa vyao.”
Tnn., “kunenepa.”
Inaonekana ni Mungu.
Tnn., “shingo yenu ngumu.”