Kumbukumbu la Torati 32:1-52

  • Wimbo wa Musa (1-47)

    • Yehova ni Mwamba (4)

    • Waisraeli wamsahau Mwamba wao (18)

    • “Kisasi ni changu” (35)

    • “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake” (43)

  • Musa atafia juu ya Mlima Nebo (48-52)

32  “Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema,Dunia na isikie maneno ya kinywa changu.   Mafundisho yangu yatanyesha kama mvua;Maneno yangu yatadondoka kama umande,Kama mvua ya rasharasha juu ya majaniNa kama manyunyu mengi juu ya mimea.   Kwa maana nitalitangaza jina la Yehova.+ Nitaongea kuhusu ukuu wa Mungu wetu!+   Yeye Mwamba, kazi zake ni kamilifu,+Kwa maana njia zake zote ni haki.+ Mungu wa uaminifu+ ambaye kamwe hana ukosefu wa haki;+Yeye ni mwadilifu na mnyoofu.+   Wao ndio wametenda kwa njia ya upotovu.+ Wao si watoto wake, kasoro ni yao wenyewe.+ Wao ni kizazi kilicho kombo na kilichopotoka!+   Je, hivi ndivyo mnavyopaswa kumtendea Yehova,+Enyi watu wajinga na wasio na hekima?+ Je, yeye si Baba yenu aliyewaumba,+Si Yeye aliyewaumba ninyi na kuwaimarisha kabisa?   Kumbukeni siku za zamani;Fikirieni miaka ya vizazi vilivyopita. Waulizeni baba zenu, nao watawaambia;+Wazee wenu, nao watawajulisha.   Aliye Juu Zaidi alipoyapa mataifa urithi wao,+Alipowatenganisha wana wa Adamu,*+Aliweka mpaka wa mataifa+Kulingana na idadi ya wana wa Israeli.+   Kwa maana watu wa Yehova ni fungu lake;+Yakobo ni urithi wake.+ 10  Alimpata katika nchi yenye nyika+Na katika jangwa tupu, lenye milio.+ Alimzunguka akimlinda, akamtunza,+Na kumlinda kama mboni ya jicho lake.+ 11  Kama tai anavyokitikisa kiota chake,Anavyopaa juu ya makinda yake,Akitandaza mabawa yake, na kuwachukua,Akiwabeba juu ya mabawa yake,+ 12  Yehova peke yake aliendelea kumwongoza;*+Hakuna mungu yeyote wa kigeni aliyekuwa pamoja naye.+ 13  Alimpitisha juu ya sehemu za juu za dunia,+Hivi kwamba akala mazao ya shambani.+ Alimlisha asali kutoka katika jabaliNa mafuta kutoka katika mwamba mgumu, 14  Siagi ya mifugo na maziwa ya kundi,Pamoja na kondoo bora,*Na kondoo dume wa Bashani, na mbuzi dume,Pamoja na ngano bora;*+Nawe ulikunywa divai kutoka katika damu* ya zabibu. 15  Yeshuruni* aliponenepa, alipiga teke kwa uasi. Umenenepa, una mafuta mengi mwilini, tumbo lako limenenepa.+ Basi akamwacha Mungu, aliyemuumba,+Na kumdharau Mwamba wa wokovu wake. 16  Kwa miungu ya kigeni walichochea hasira yake kali;+Walikuwa wakimkasirisha kwa mambo yanayochukiza.+ 17  Walikuwa wakiwatolea dhabihu roho waovu, wala si Mungu,+Miungu ambayo hawakuijua,Mipya iliyokuja hivi karibuni,Miungu ambayo mababu zenu hawakuijua. 18  Mlimsahau Mwamba,+ baba yenu aliyewazaa,Nanyi hamkumkumbuka Mungu aliyewazaa.+ 19  Yehova alipoona hilo, aliwakataa+Kwa sababu wanawe na mabinti zake walimkasirisha. 20  Kwa hiyo akasema, ‘Nitauficha uso wangu wasiuone;+Nitaona kitakachowapata. Kwa maana wao ni kizazi kilichopotoka,+Wana ambao hawana uaminifu.+ 21  Wamechochea hasira yangu kali* kwa kitu ambacho si mungu;+Wamenikasirisha kwa sanamu zao za ubatili.+ Kwa hiyo nitawachochea wawe na wivu kwa wale ambao si taifa;+Nitawakasirisha kwa kutumia taifa lenye ujinga.+ 22  Kwa maana hasira yangu imewasha moto+Ambao utateketeza mpaka kwenye kina cha Kaburi,*+Nao utateketeza dunia na mazao yakeNa kuchoma moto misingi ya milima. 23  Nitazidisha misiba yao;Nitawapiga kwa mishale yangu mpaka iishe. 24  Watachoka kwa sababu ya njaa+Na kuliwa na homa kali na maangamizi machungu.+ Nitawatumia meno ya wanyama ili yawashambulie+Na sumu ya wanyama wanaotambaa mavumbini. 25  Nje, upanga utawaangamiza watoto wao;+Na ndani, kuna hofu+ Kwa kijana na bikira,Mtoto anayenyonya pamoja na mzee mwenye mvi.+ 26  Ningesema: “Nitawatawanya;Nitafanya ukumbusho wao usahauliwe kabisa miongoni mwa wanadamu,” 27  Isingekuwa kwa sababu ya kuogopa jinsi maadui wangu watakavyotenda,+Kwa sababu huenda wapinzani wakalielewa vibaya jambo hilo.+ Huenda wakasema: “Nguvu zetu zimeshinda;+Si Yehova aliyefanya mambo haya yote.” 28  Kwa maana wao ni taifa lisilo na akili,*Na hawana uelewaji miongoni mwao.+ 29  Laiti wangekuwa na hekima!+ Wangetafakari jambo hili.+ Wangefikiria mwisho wao.+ 30  Mtu mmoja angewezaje kuwakimbiza 1,000,Na wawili kuwafanya 10,000 wakimbie?+ Kama Mwamba wao hangekuwa amewauza+Na Yehova kuwatia mikononi mwa maadui? 31  Kwa maana mwamba wao si kama Mwamba wetu,+Hata maadui wetu wameelewa hilo.+ 32  Kwa maana mzabibu wao unatoka katika mzabibu wa SodomaNa kutoka katika matuta ya Gomora.+ Zabibu zao ni zabibu za sumu,Vishada vyao ni vichungu.+ 33  Divai yao ni sumu ya nyoka,Sumu kali ya swila. 34  Je, hili sijaliweka akibani,Na kulifungia kabisa katika ghala langu?+ 35  Kisasi ni changu, na malipo,+Wakati utakapofika ambapo mguu wao utateleza,+Kwa maana siku ya msiba wao iko karibu,Na kinachowasubiri kitafika haraka.’ 36  Kwa maana Yehova atawahukumu watu wake,+Naye atawahurumia* watumishi wake+Atakapoona nguvu zao zimeisha,Na kwamba waliobaki ni wasio na uwezo na walio dhaifu peke yao. 37  Ndipo atakaposema, ‘Miungu yao iko wapi,+Mwamba ambao waliukimbilia, 38  Iliyokuwa ikila mafuta ya dhabihu zao,*Na kunywa divai ya matoleo yao ya kinywaji?+ Acheni iinuke na kuwasaidia ninyi. Na iwe kimbilio lenu. 39  Sasa tazameni kwamba mimi—mimi ndiye,+Na hakuna miungu mingine ila mimi.+ Mimi huua, nami hufanya kuwa hai.+ Ninajeruhi,+ nami nitaponya,+Na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote kutoka mikononi mwangu.+ 40  Kwa maana nainua mkono wangu mbinguni,Na kuapa hivi: “Kwa hakika kama niishivyo milele,”+ 41  Nikiunoa upanga wangu unaometametaNa kuutayarisha mkono wangu ili uhukumu,+Nitawalipiza kisasi maadui wangu+Na kuwalipa wale wanaonichukia. 42  Nitailewesha mishale yangu kwa damu,Na upanga wangu utakula nyama,Pamoja na damu ya waliouawa na pia mateka,Pamoja na vichwa vya viongozi wa adui.’ 43  Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,+Kwa maana atailipizia kisasi damu ya watumishi wake,+Atawalipiza kisasi maadui wake+Na kufunika dhambi ya* nchi ya watu wake.” 44  Basi Musa akaja na kuyasema maneno yote ya wimbo huo watu wakisikia;+ alikuwa na Hoshea*+ mwana wa Nuni. 45  Musa alipomaliza kuwaambia Waisraeli wote maneno hayo yote, 46  akawaambia hivi: “Wekeni mioyoni mwenu maonyo yote niliyowapa leo,+ ili muwaamuru wana wenu wawe waangalifu kutenda maneno yote ya Sheria hii.+ 47  Kwa maana haya si maneno matupu kwenu, bali yanamaanisha uhai wenu,+ na kwa maneno haya mnaweza kuishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.” 48  Yehova akaongea na Musa siku hiyohiyo na kumwambia hivi: 49  “Panda juu ya mlima huu wa Abarimu,+ Mlima Nebo,+ ulio katika nchi ya Moabu, unaoelekeana na Yeriko, nawe utazame nchi ya Kanaani, ninayowapa Waisraeli waimiliki.+ 50  Kisha utakufa juu ya mlima utakaopanda hivi punde, na kuzikwa pamoja na watu wako,* kama Haruni ndugu yako alivyokufa juu ya Mlima Hori+ na kuzikwa pamoja na watu wake, 51  kwa sababu nyote wawili hamkuwa waaminifu kwangu miongoni mwa Waisraeli kwenye maji ya Meriba+ kule Kadeshi katika nyika ya Zini, kwa sababu hamkunitakasa mbele ya Waisraeli.+ 52  Utaiona nchi hiyo kwa mbali, lakini hutaingia katika nchi hiyo ninayowapa Waisraeli.”+

Maelezo ya Chini

Au labda, “Alipoitenganisha jamii ya wanadamu.”
Yaani, Yakobo.
Tnn., “mafuta ya kondoo.”
Tnn., “mafuta ya figo ya ngano.”
Au “maji.”
Maana yake “Mnyoofu,” jina la heshima la Israeli.
Au “wivu wangu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au labda, “lisilosikia ushauri.”
Au “ataghairi kwa sababu ya.”
Au “kula dhabihu zao bora.”
Au “Na kuisafisha.”
Jina la awali la Yoshua. Hoshea ni ufupisho wa jina Hoshaya, linalomaanisha “Aliyeokolewa na Yah; Yah Ameokoa.”
Tnn., “kukusanywa kwa watu wako.” Huu ni msemo wa kishairi unaorejelea kifo.