Kumbukumbu la Torati 33:1-29

  • Musa ayabariki makabila (1-29)

    • ‘Mikono ya milele’ ya Yehova (27)

33  Sasa hii ndiyo baraka ambayo Musa mtu wa Mungu wa kweli aliwatangazia Waisraeli kabla ya kifo chake.+  Alisema hivi: “Yehova—alikuja kutoka Sinai,+Naye akawaangazia kutoka Seiri. Aliangaza kwa utukufu kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+Naye alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+Na mashujaa wake kwenye mkono wake wa kuume.+   Aliwapenda watu wake;+Watakatifu wao wote wako mikononi mwako.+ Waliketi miguuni pako;+Walianza kusikiliza maneno yako.+   (Musa alitupatia amri, sheria,+Kuwa miliki ya kutaniko la Yakobo.)+   Naye akawa mfalme kule Yeshuruni,*+Viongozi wa watu walipokusanyika pamoja,+Pamoja na makabila yote ya Israeli.+   Rubeni na aishi wala asife,+Na watu wake wasiwe wachache.”+   Naye akamtangazia Yuda baraka hii:+ “Ee Yehova, isikie sauti ya Yuda,+Nawe umrudishe kwa watu wake. Mikono yake imetetea* kilicho chake,Nawe umsaidie dhidi ya maadui wake.”+   Akasema hivi kumhusu Lawi:+ “Thumimu yako* na Urimu+ yako ni vya mtu aliye mshikamanifu kwako,+Uliyemjaribu kule Masa.+ Ulianza kupambana naye karibu na maji ya Meriba,+   Mtu aliyemwambia baba yake na mama yake, ‘Sijawaheshimu.’ Hata ndugu zake hakuwatambua,+Na watoto wake mwenyewe aliwapuuza. Kwa maana walitii neno lako,Na kulishika agano lako.+ 10  Acha wamfundishe Yakobo amri zako*+Na Waisraeli Sheria yako.+ Acha wakufukizie uvumba wenye harufu inayokupendeza*+Na dhabihu nzima ya kuteketezwa kwenye madhabahu yako.+ 11  Ee Yehova, bariki nguvu zake,Na ufurahie kazi ya mikono yake. Ivunje miguu ya* wale wanaoinuka dhidi yake,Ili wale wanaomchukia wasiinuke tena.” 12  Alisema hivi kumhusu Benjamini:+ “Mwache mpendwa wa Yehova akae kwa usalama kando yake;Akimkinga siku nzima,Atakaa katikati ya mabega yake.” 13  Alisema hivi kumhusu Yosefu:+ “Nchi yake na ibarikiwe na Yehova+Kwa vitu bora vya mbinguni,Kwa umande na maji kutoka katika chemchemi zilizo chini,+ 14  Kwa vitu bora vinavyoletwa na juaNa mazao bora kila mwezi,+ 15  Kwa vitu bora kabisa kutoka katika milima ya zamani*+Na vitu bora kutoka katika vilima vinavyodumu, 16  Kwa vitu bora vya dunia na vitu vinavyoijaza,+Na kwa kibali cha Yule anayekaa katika kichaka cha miiba.+ Na vije juu ya kichwa cha Yosefu,Juu ya utosi wa kichwa cha yule aliyechaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+ 17  Fahari yake ni kama ya mzaliwa wa kwanza wa ng’ombe dume,Na pembe zake ni pembe za fahali mwitu. Atazitumia kuyasukuma* mataifaYote pamoja mpaka miisho ya dunia. Wao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+Nao ni maelfu ya Manase.” 18  Alisema hivi kumhusu Zabuloni:+ “Shangilia, Ee Zabuloni, unapotoka nje,Nawe, Isakari, katika mahema yako.+ 19  Watayaita mataifa mlimani. Huko watatoa dhabihu za uadilifu. Kwa maana watafyonza* utajiri mwingi wa bahariNa marundo yaliyofichika* mchangani.” 20  Alisema hivi kumhusu Gadi:+ “Amebarikiwa yule anayepanua mipaka ya Gadi.+ Analala huko kama simba,Akiwa tayari kuunyafua mkono, naam, utosi wa kichwa. 21  Atajichagulia fungu la kwanza,+Kwa maana huko fungu la mpaji sheria limehifadhiwa.+ Viongozi wa watu watakusanyika pamoja. Uadilifu wa Yehova atautekeleza,Na amri zake* pamoja na Israeli.” 22  Alisema hivi kumhusu Dani:+ “Dani ni mwanasimba.+ Ataruka kutoka Bashani.”+ 23  Alisema hivi kumhusu Naftali:+ “Naftali ameshiba kibaliNaye amejaa baraka ya Yehova. Imiliki magharibi na kusini.” 24  Alisema hivi kumhusu Asheri:+ “Asheri amebarikiwa kuwa na wana. Na apendwe na ndugu zake,Naye achovye* miguu yake katika mafuta. 25  Makufuli ya lango lako ni chuma na shaba,+Nawe utakuwa salama siku zako zote.* 26  Hakuna aliye kama Mungu wa kweli+ wa Yeshuruni,+Anayepita mbinguni kuja kukusaidiaNa kupita juu ya mawingu katika fahari yake.+ 27  Mungu ni kimbilio tangu nyakati za kale,+Mikono yake ya milele iko chini yako.+ Naye atamfukuza adui kutoka mbele yako,+Naye atasema, ‘Waangamize!’+ 28  Israeli atakaa kwa usalama,Na chemchemi ya Yakobo itatengwa peke yakeKatika nchi ya nafaka na divai mpya,+Na anga lake litadondosha umande.+ 29  Wewe ni mwenye furaha, Ee Israeli!+ Ni nani aliye kama wewe,+Taifa linalofurahia wokovu wa Yehova,+Ngao yenu inayowalinda+Na upanga wenu wenye fahari? Maadui wenu watajikunyata mbele yenu,+Nanyi mtawakanyaga migongoni.”*

Maelezo ya Chini

Maana yake “Mnyoofu,” jina la heshima la Israeli.
Au “imepigania.”
Neno “yako” katika mstari huu linamrejelea Mungu.
Tnn., “maamuzi yako ya hukumu.”
Tnn., “inayopendeza puani mwako.”
Au “Vivunje viuno vya.”
Au labda, “milima ya mashariki.”
Au “kuyapiga.”
Tnn., “watanyonya.”
Au “hazina zilizofichika.”
Tnn., “maamuzi yake ya hukumu.”
Au “anawe.”
Tnn., “Kama zilivyo siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.”
Au labda, “mtakanyaga mahali pao pa juu.”