Kumbukumbu la Torati 5:1-33

  • Agano la Yehova kule Horebu (1-5)

  • Amri Kumi zarudiwa (6-22)

  • Watu waogopa kwenye Mlima Sinai (23-33)

5  Kisha Musa akawaita Waisraeli wote na kuwaambia hivi: “Enyi Waisraeli, sikilizeni masharti na sheria ambazo* ninawatangazia ninyi leo, nanyi mnapaswa kujifunza na kushika kwa uangalifu masharti na sheria hizo.  Yehova Mungu wetu alifanya agano pamoja nasi kule Horebu.+  Yehova hakufanya agano hilo pamoja na mababu zetu, bali pamoja nasi, sisi sote tulio hai hapa leo.  Yehova alizungumza nanyi uso kwa uso mlimani, kutoka katika moto.+  Wakati huo nilisimama kati yenu na Yehova+ ili niwaambie neno la Yehova, kwa maana mliogopa kwa sababu ya moto nanyi hamkupanda mlimani.+ Alisema hivi:  “‘Mimi ni Yehova Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+  Hupaswi kamwe kuwa na miungu mingine ila mimi.*+  “‘Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa+ au mfano wa* kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani au kilicho ndani ya maji chini ya dunia.  Usiviinamie wala kushawishiwa kuviabudu,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu ninayetaka watu waniabudu mimi peke yangu,+ nami huwaadhibu watoto kwa sababu ya makosa ya baba zao, kufikia kizazi cha tatu na kizazi cha nne cha wale wanaonichukia,+ 10  lakini ninawatendea kwa upendo mshikamanifu* watu wanaonipenda na kushika amri zangu, kufikia kizazi chao cha elfu. 11  “‘Usilitumie jina langu mimi, Yehova Mungu wako, kwa njia isiyofaa,+ kwa maana mimi Yehova sitakosa kumwadhibu yule anayelitumia jina langu kwa njia isiyofaa.+ 12  “‘Ishike siku ya Sabato na uione kuwa takatifu, kama mimi Yehova Mungu wako nilivyokuamuru.+ 13  Fanya shughuli na kazi zako zote kwa siku sita,+ 14  lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako.+ Usifanye kazi yoyote,+ wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala kijakazi wako, wala ng’ombe dume wako, wala punda wako, wala mnyama yeyote unayemfuga, wala mgeni anayekaa katika majiji*+ yenu, ili mtumwa wako na kijakazi wako wapumzike kama wewe.+ 15  Kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa nchini Misri, na mimi Yehova Mungu wako nikakutoa huko kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa.+ Ndiyo sababu mimi Yehova Mungu wako nilikuamuru uishike siku ya Sabato. 16  “‘Mheshimu baba yako na mama yako,+ kama mimi Yehova Mungu wako nilivyokuamuru, ili uishi muda mrefu na kufanikiwa* katika nchi ambayo mimi Yehova Mungu wako ninakupa.+ 17  “‘Usiue.+ 18  “‘Wala usifanye uzinzi.+ 19  “‘Wala usiibe.+ 20  “‘Wala usitoe ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yako.+ 21  “‘Wala usimtamani mke wa jirani yako.+ Wala usitamani kwa ubinafsi nyumba ya jirani yako, wala shamba lake, wala mtumwa wake, wala kijakazi wake, wala ng’ombe dume wake, wala punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.’+ 22  “Yehova aliwapa amri hizo* ninyi nyote mlimani, kutoka katika moto, wingu, na utusitusi mzito,+ kwa sauti kubwa, naye hakuongeza lolote; kisha akaziandika kwenye mabamba mawili ya mawe na kunipa.+ 23  “Lakini mara tu mliposikia sauti kutoka katika lile giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto,+ viongozi wote wa makabila yenu na wazee wakanijia. 24  Kisha mkasema, ‘Tazama, Yehova Mungu wetu ametuonyesha utukufu wake na ukuu wake, nasi tumesikia sauti yake kutoka katika moto.+ Leo tumeona kwamba Mungu anaweza kuongea na mwanadamu na mwanadamu huyo aendelee kuishi.+ 25  Sasa, kwa nini tufe? Kwa maana moto huu mkubwa unaweza kututeketeza. Tukiendelea kuisikia sauti ya Yehova Mungu wetu, hakika tutakufa. 26  Kwa maana ni nani kati ya wanadamu wote* aliyesikia sauti ya Mungu aliye hai ikiongea kutoka katika moto kama tulivyosikia na bado anaishi? 27  Wewe mwenyewe nenda karibu, usikie yote ambayo Yehova Mungu wetu atasema, nawe ndiwe utakayetuambia mambo yote ambayo Yehova Mungu wetu anakuambia, nasi tutasikiliza na kutenda mambo hayo.’+ 28  “Basi Yehova alisikia maneno mliyoniambia, naye Yehova akaniambia, ‘Nimesikia maneno ambayo watu hawa wamekuambia. Mambo yote waliyosema ni sawa.+ 29  Laiti sikuzote wangekuwa na moyo wenye mwelekeo wa kuniogopa+ na kushika amri zangu zote;+ basi mambo yangewaendea vyema wao na wana wao milele!+ 30  Nenda uwaambie hivi: “Rudini kwenye mahema yenu.” 31  Lakini unapaswa kubaki hapa pamoja nami, nami nitakuambia amri zote, masharti, na sheria unazopaswa kuwafundisha na ambazo wanapaswa kushika katika nchi ninayowapa wamiliki.’ 32  Sasa ninyi watu mnapaswa kuwa waangalifu kufanya kama Yehova Mungu wenu alivyowaamuru.+ Msigeuke kwenda kulia wala kushoto.+ 33  Mnapaswa kutembea katika njia yote ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mfuate,+ ili mwishi na kufanikiwa na kurefusha siku zenu katika nchi mtakayomiliki.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”
Au “dhidi yangu.” Tnn., “dhidi ya uso wangu.”
Au “umbo la.”
Au “fadhili zenye upendo.”
Tnn., “malango.”
Au “na ili mambo yakuendee vyema.”
Tnn., “maneno hayo.”
Au “ni nani mwenye mwili wa nyama.”