Kumbukumbu la Torati 6:1-25

  • Mpende Yehova kwa moyo wako wote (1-9)

    • “Sikilizeni, enyi Waisraeli” (4)

    • Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto (6, 7)

  • Msimsahau Yehova (10-15)

  • Msimjaribu Yehova (16-19)

  • Kiambieni kizazi kinachofuata (20-25)

6  “Sasa hizi ndizo amri, masharti, na sheria ambazo Yehova Mungu wako ametoa ili ufundishwe, ili uzishike unapovuka kuingia katika nchi ambayo utaimiliki,  ili umwogope Yehova Mungu wako na kushika sheria zake zote na amri zake ambazo ninakuamuru wewe—wewe na mwana wako na mjukuu wako+—siku zote za maisha yako, ili uishi muda mrefu.+  Sikilizeni, enyi Waisraeli, na mzishike kwa uangalifu, ili mfanikiwe na kuwa wengi sana katika nchi inayotiririka maziwa na asali, kama Yehova, Mungu wa mababu zenu, alivyowaahidi.  “Sikilizeni, enyi Waisraeli: Yehova Mungu wetu ni Yehova mmoja.+  Ni lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi*+ yako yote na kwa nguvu zako zote.*+  Maneno haya ninayokuamuru leo lazima yawe moyoni mwako,  nawe lazima uyakazie* kwa wanao+ na kuongea kuyahusu unapoketi nyumbani mwako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.+  Yafunge yawe kumbukumbu mkononi mwako, na lazima yawe kama utepe kwenye paji la uso wako.*+  Yaandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na kwenye malango yako. 10  “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi aliyowaapia mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atawapa ninyi+—majiji makubwa na yenye kupendeza ambayo hamkujenga,+ 11  nyumba zilizojaa vitu vizuri vya aina mbalimbali ambavyo hamkufanya kazi ili kuvipata, visima ambavyo hamkuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni ambayo hamkupanda—nanyi mtakapokuwa mmekula na kushiba,+ 12  jihadharini msimsahau Yehova,+ aliyewatoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa. 13  Mnapaswa kumwogopa+ Yehova Mungu wenu, mnapaswa kumtumikia yeye,+ nanyi mnapaswa kuapa kwa jina lake.+ 14  Msifuate miungu mingine, miungu yoyote ya mataifa yote yanayowazunguka,+ 15  kwa maana Yehova Mungu wenu ambaye yuko miongoni mwenu ni Mungu anayetaka watu wamwabudu yeye peke yake.+ Msipofanya hivyo, hasira ya Yehova Mungu wenu itawaka dhidi yenu,+ naye atawaangamiza kabisa kutoka duniani.+ 16  “Msimjaribu Yehova Mungu wenu kama mlivyomjaribu+ kule Masa.+ 17  Mnapaswa kuzishika kwa bidii amri za Yehova Mungu wenu na vikumbusho vyake na masharti yake ambayo amewaamuru mshike. 18  Ni lazima mfanye mambo mema na yanayofaa machoni pa Yehova, ili mfanikiwe na ili mwingie na kuimiliki nchi nzuri ambayo Yehova aliwaapia mababu zenu,+ 19  kwa kuwafukuza maadui wenu wote kutoka mbele yenu, kama Yehova alivyoahidi.+ 20  “Wakati ujao, mwana wako akikuuliza, ‘Vikumbusho, masharti, na sheria* ambazo Yehova Mungu wetu ametuamuru tushike zinamaanisha nini?’ 21  ndipo utakapomwambia mwana wako, ‘Tulikuwa watumwa wa Farao kule Misri, lakini Yehova alitutoa Misri kwa mkono wenye nguvu. 22  Basi mbele ya macho yetu, Yehova aliendelea kufanya ishara na miujiza mikubwa na iliyoleta uharibifu nchini Misri,+ na pia kwa Farao na nyumba yake yote.+ 23  Naye akatutoa huko ili atulete hapa na kutupatia nchi ambayo aliwaapia mababu zetu.+ 24  Kisha Yehova akatuamuru tufuate masharti hayo yote na kumwogopa Yehova Mungu wetu ili tufanikiwe daima,+ na ili tuendelee kuishi,+ kama ilivyo leo. 25  Tukimtii Yehova Mungu wetu kwa kushika kwa uangalifu amri hizo zote, kama alivyotuamuru, tutakuwa waadilifu.’+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “uwezo wako wote.”
Au “uyarudie; uyasisitize.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu.”