Kumbukumbu la Torati 7:1-26

  • Mataifa saba yataangamizwa (1-6)

  • Sababu ya Waisraeli kuchaguliwa (7-11)

  • Utii utawaletea mafanikio wakati ujao (12-26)

7  “Yehova Mungu wenu atakapowaleta katika nchi mnayokaribia kuingia na kuimiliki,+ atayaondoa pia mataifa makubwa kutoka mbele yenu:+ Wahiti, Wagirgashi, Waamori,+ Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ mataifa saba makubwa zaidi na yenye nguvu kuliko ninyi.+  Yehova Mungu wenu atawatia watu hao mikononi mwenu, nanyi mtawashinda.+ Mnapaswa kuwaangamiza kabisa.+ Msifanye agano lolote pamoja nao wala kuwahurumia.+  Msioane nao kamwe. Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao wala msikubali wana wenu wawaoe mabinti wao.+  Kwa maana watawapotosha wana wenu waache kumfuata Mungu na kuanza kuabudu miungu mingine;+ kisha hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu, naye atawaangamiza upesi.+  “Lakini hivi ndivyo mtakavyowatendea: Bomoeni madhabahu zao, vunjeni nguzo zao takatifu,+ kateni miti yao mitakatifu,*+ na kuteketeza sanamu zao za kuchongwa.+  Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu, na Yehova Mungu wenu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali yake ya pekee,* kutoka kati ya mataifa yote yaliyo duniani.+  “Yehova hakuwapenda na kuwachagua ninyi eti kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote,+ kwa maana mlikuwa taifa dogo zaidi kati ya mataifa yote.+  Badala yake, ni kwa sababu Yehova anawapenda na alitimiza kiapo alichowaapia mababu zenu,+ ndiyo maana Yehova aliwatoa Misri kwa mkono wake wenye nguvu na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa,+ kutoka katika nguvu za* Farao mfalme wa Misri.  Mnajua vizuri kwamba Yehova Mungu wenu ndiye Mungu wa kweli, Mungu mwaminifu, anayetimiza agano lake na kutenda kwa upendo mshikamanifu kufikia kizazi cha elfu cha wale wanaompenda na kushika amri zake.+ 10  Lakini wale wanaomchukia atawalipa waziwazi* kwa kuwaangamiza.+ Hatakawia kuwaadhibu wale wanaomchukia; atawalipa waziwazi.* 11  Kwa hiyo, muwe waangalifu kushika amri na masharti na sheria ambazo* ninawaamuru leo, kwa kuzifuata. 12  “Mkiendelea kusikiliza sheria hizi na kuzifuata na kuzitekeleza, Yehova Mungu wenu atatimiza lile agano na kuwatendea kwa upendo mshikamanifu kama alivyowaapia mababu zenu. 13  Atawapenda na kuwabariki na kuwafanya mwongezeke. Naam, atawabariki kwa kuwapa watoto wengi,*+ mazao ya ardhi yenu, nafaka yenu, divai yenu mpya, mafuta yenu,+ ndama na wanakondoo wa makundi yenu, katika nchi aliyowaapia mababu zenu kwamba atawapa ninyi.+ 14  Mtabarikiwa kuliko mataifa mengine yote;+ hakuna mwanamume au mwanamke yeyote miongoni mwenu atakayekosa mtoto, wala mifugo yenu haitakosa kuzaa.+ 15  Yehova atawaondolea magonjwa yote, naye hatawaletea ugonjwa wowote unaotisha mlioujua kule Misri.+ Badala yake, atawaletea magonjwa hayo wote wanaomchukia. 16  Mtayaangamiza* mataifa yote ambayo Yehova Mungu wenu atayatia mikononi mwenu.+ Msiwahurumie*+ kamwe, nanyi msiabudu kamwe miungu yao,+ kwa sababu jambo hilo litakuwa mtego kwenu.+ 17  “Mkijiambia mioyoni mwenu, ‘Mataifa haya yana watu wengi kuliko sisi. Tunawezaje kuyafukuza?’+ 18  msiwaogope.+ Mnapaswa kujikumbusha mambo ambayo Yehova Mungu wenu alimtendea Farao na nchi yote ya Misri,+ 19  zile hukumu kubwa* ambazo mliona kwa macho yenu na ishara na miujiza+ na mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa ambao Yehova Mungu wenu aliutumia kuwatoa huko.+ Hivyo ndivyo Yehova Mungu wenu atakavyoyatendea mataifa yote mnayoyaogopa.+ 20  Yehova Mungu wenu atawafanya wavunjike moyo* mpaka watakapoangamia wale waliobaki+ na waliokuwa wakijificha ili msiwapate. 21  Msishtuke kwa sababu yao, kwa maana Yehova Mungu wenu yuko pamoja nanyi,+ Mungu mkuu na mwenye kuogopesha.+ 22  “Kwa hakika Yehova Mungu wenu atayafukuza mataifa haya kutoka mbele yenu kidogo kidogo.+ Hamtaruhusiwa kuwaangamiza upesi, ili wanyama wa mwituni wasiongezeke na kuwashambulia ninyi. 23  Yehova Mungu wenu atayatia mikononi mwenu na kuyashinda kabisa mpaka yaangamie.+ 24  Atawatia wafalme wa mataifa hayo mikononi mwenu,+ nanyi mtayafutilia mbali majina yao kutoka duniani.*+ Hakuna mtu atakayewazuia,+ mpaka mtakapowaangamiza.+ 25  Mnapaswa kuchoma moto sanamu za kuchongwa za miungu yao.+ Msitamani fedha na dhahabu ya sanamu hizo wala msiichukue,+ ili isiwe mtego kwenu, kwa maana ni chukizo kwa Yehova Mungu wenu.+ 26  Msilete ndani ya nyumba zenu kitu kinachochukiza kwa sababu mtakuwa kama kitu hicho kinachopaswa kuharibiwa. Mnapaswa kukichukia kabisa na kukikirihi kabisa, kwa sababu ni kitu kinachopaswa kuharibiwa.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “mali yake anayothamini sana.”
Tnn., “kutoka mikononi mwa.”
Tnn., “mbele ya uso wao.”
Tnn., “mbele ya uso wao.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”
Tnn., “atabariki uzao wa tumbo lenu.”
Tnn., “Mtayameza.”
Tnn., “Jicho lenu lisiwahurumie.”
Au “yale majaribu makubwa.”
Au labda, “washikwe na wasiwasi; waogope.”
Tnn., “kutoka chini ya mbingu.”