Kumbukumbu la Torati 9:1-29

  • Sababu ya Waisraeli kupewa ile nchi (1-6)

  • Waisraeli wamkasirisha Yehova mara nne (7-29)

    • Ndama wa dhahabu (7-14)

    • Musa aingilia kati (15-21, 25-29)

    • Wamkasirisha mara tatu zaidi (22)

9  “Sikilizeni, enyi Waisraeli, leo mnavuka Yordani+ na kuingia kumiliki nchi yenye mataifa makubwa zaidi na yenye nguvu zaidi kuliko ninyi,+ majiji makubwa na yenye ngome zinazofika mbinguni,*+  watu wenye nguvu na warefu, wana wa Waanaki,+ mnaowajua na ambao mmesikia watu wakisema hivi kuwahusu: ‘Ni nani anayeweza kuwashinda wana wa Anaki?’  Kwa hiyo, mnapaswa kujua leo kwamba Yehova Mungu wenu atawatangulia mnapovuka.+ Yeye ni moto unaoteketeza,+ atawaangamiza. Atawashinda mbele ya macho yenu ili mwafukuze* na kuwaangamiza haraka, kama Yehova alivyoahidi.+  “Yehova Mungu wenu atakapowafukuza kutoka mbele yenu, msiseme hivi mioyoni mwenu: ‘Yehova amenileta ili nimiliki nchi hii kwa sababu ya uadilifu wangu mwenyewe.’+ Badala yake, Yehova anayafukuza mataifa hayo+ kutoka mbele yenu kwa sababu ya uovu wao.  Hamwendi kumiliki nchi yao kwa sababu ya uadilifu wenu au unyoofu wa mioyo yenu. Badala yake, Yehova Mungu wenu anayafukuza mataifa hayo kutoka mbele yenu+ kwa sababu ya uovu wao na ili Yehova atimize neno alilowaapia mababu zenu, Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+  Basi, mjue kwamba Yehova Mungu wenu hawapi nchi hii nzuri mwimiliki kwa sababu ya uadilifu wenu; kwa maana ninyi ni watu wakaidi.*+  “Kumbukeni, msisahau kamwe jinsi mlivyomkasirisha Yehova Mungu wenu nyikani.+ Tangu siku mliyotoka nchini Misri mpaka mlipofika mahali hapa, mmekuwa mkimwasi Yehova.+  Hata kule Horebu mlimkasirisha Yehova, na Yehova akapandwa na hasira sana hivi kwamba alitaka kuwaangamiza.+  Nilipopanda mlimani ili kupokea yale mabamba ya mawe,+ mabamba ya agano ambalo Yehova alifanya pamoja nanyi,+ nilikaa mlimani siku 40 mchana na usiku,+ sikula chakula wala kunywa maji. 10  Kisha Yehova akanipa yale mabamba mawili ya mawe yaliyoandikwa kwa kidole cha Mungu, nayo yalikuwa na maneno yote ambayo Yehova aliwaambia mlimani kutoka katika moto siku ya kusanyiko.*+ 11  Mwishoni mwa zile siku 40 mchana na usiku, Yehova alinipa yale mabamba mawili ya mawe, yale mabamba ya agano, 12  na Yehova akaniambia, ‘Ondoka, shuka upesi kutoka hapa, kwa sababu watu wako uliowatoa Misri wametenda mambo mapotovu.+ Wamegeuka upesi kutoka katika njia niliyowaamuru wafuate. Wamejitengenezea sanamu ya chuma.’*+ 13  Kisha Yehova akaniambia, ‘Nimewatazama watu hawa, nikaona ni watu wakaidi.*+ 14  Niache, nami nitawaangamiza na kufutilia mbali jina lao kutoka duniani,* na acha nikufanye wewe kuwa taifa lenye nguvu zaidi na lenye watu wengi kuliko wao.’+ 15  “Basi nikageuka na kushuka mlimani huku mlima ukiwaka moto,+ nami nilikuwa nimebeba yale mabamba mawili ya agano kwa mikono yangu miwili.+ 16  Kisha nikatazama na kuona kwamba mlikuwa mmemtendea dhambi Yehova Mungu wenu! Mlikuwa mmejitengenezea ndama wa chuma.* Mlikuwa mmegeuka upesi kutoka katika njia ambayo Yehova alikuwa amewaamuru mfuate.+ 17  Basi nikashika yale mabamba mawili na kuyatupa chini kwa mikono yangu miwili na kuyavunja mbele ya macho yenu.+ 18  Kisha nikalala kifudifudi mbele za Yehova kwa siku 40, mchana na usiku, kama nilivyofanya mwanzoni. Sikula chakula wala kunywa maji,+ kwa sababu ya dhambi zote mlizokuwa mmetenda kwa kufanya uovu machoni pa Yehova na kumkasirisha. 19  Kwa maana niliogopa sana kwa sababu Yehova alikuwa amewakasirikia sana,+ naye alitaka kuwaangamiza. Hata hivyo, Yehova alinisikiliza wakati huo pia.+ 20  “Yehova alimkasirikia sana Haruni hivi kwamba alitaka kumwangamiza,+ lakini wakati huo niliomba dua kwa ajili ya Haruni pia. 21  Halafu nikachukua kile kitu cha dhambi mlichokitengeneza, yule ndama,+ na kumteketeza kwa moto; nikamponda na kumsagasaga kabisa mpaka akawa laini kama mavumbi, nami nikayatupa mavumbi hayo katika kijito kinachotiririka kutoka mlimani.+ 22  “Pia, mlimkasirisha Yehova kule Tabera,+ kule Masa,+ na Kibroth-hataava.+ 23  Yehova alipowatuma kutoka Kadesh-barnea+ na kuwaambia, ‘Pandeni mwimiliki nchi ambayo kwa hakika nitawapa!’ mliasi tena agizo la Yehova Mungu wenu,+ nanyi hamkuonyesha imani+ kumwelekea wala hamkumtii. 24  Mmekuwa mkimwasi Yehova tangu nilipowajua. 25  “Kwa hiyo niliendelea kulala kifudifudi mbele za Yehova siku 40, mchana na usiku,+ nililala kifudifudi kwa sababu Yehova alisema atawaangamiza. 26  Nikaanza kutoa dua kwa Yehova na kusema, ‘Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, usiwaangamize watu hawa. Wao ni mali yako binafsi,*+ watu uliowakomboa kwa ukuu wako na kuwatoa Misri kwa mkono wenye nguvu.+ 27  Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Yakobo.+ Usikazie fikira ukaidi wa watu hawa, uovu wao, na dhambi yao.+ 28  Kama sivyo watu wa nchi ulimotutoa huenda wakasema: “Yehova alishindwa kuwaingiza katika nchi aliyowaahidi, na kwa sababu aliwachukia, aliwatoa ili awaue nyikani.”+ 29  Kwa maana ni watu wako na mali yako binafsi,*+ watu uliowatoa kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulionyooshwa.’+

Maelezo ya Chini

Yaani, yana kuta ndefu sana.
Au “mchukue nchi yao.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Au “kukutanika.”
Au “sanamu ya kuyeyushwa.”
Au “wenye shingo ngumu.”
Tnn., “kutoka chini ya mbingu.”
Au “kuyeyushwa.”
Au “urithi wako.”
Au “urithi wako.”