Kutoka 11:1-10

  • Pigo la kumi latangazwa (1-10)

    • Waisraeli watawaomba Wamisri zawadi (2)

11  Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Nitamletea Farao na Misri pigo moja zaidi. Baada ya pigo hilo atawaruhusu mwondoke hapa.+ Atakapowaruhusu mwondoke, atawafukuza kabisa kutoka hapa.+  Sasa waambie watu kwamba wanaume wote na wanawake wote wanapaswa kuwaomba majirani wao vito vya fedha na dhahabu.”+  Basi Yehova akawafanya watu wapate kibali machoni pa Wamisri. Isitoshe, wakati huo Musa mwenyewe alikuwa mtu anayeheshimiwa sana na watumishi wa Farao na watu wengine nchini Misri.  Basi Musa akasema: “Yehova amesema hivi: ‘Karibu katikati ya usiku, nitapita katikati ya Misri,+  na kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri atakufa,+ kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao anayeketi kwenye kiti chake cha ufalme mpaka mzaliwa wa kwanza wa kijakazi anayesaga nafaka kwa jiwe la kusagia, na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.+  Katika nchi yote ya Misri, kutakuwa na kilio kikubwa ambacho hakijawahi kamwe kuonekana na wala hakitaonekana tena kamwe.+  Lakini hakuna hata mbwa atakayewabwekea* Waisraeli, iwe ni wanadamu au mifugo yao, ili mjue kwamba mimi Yehova ninaweza kutofautisha kati ya Wamisri na Waisraeli.’+  Na watumishi wako wote hakika watakuja mbele zangu na kuniinamia, wakisema, ‘Nenda, wewe na watu wote wanaokufuata.’+ Na baada ya hapo, nitaondoka.” Ndipo akatoka mbele ya Farao kwa hasira kali.  Kisha Yehova akamwambia Musa: “Farao hatakusikiliza,+ ili miujiza yangu iongezeke katika nchi ya Misri.”+ 10  Musa na Haruni walifanya miujiza hiyo yote mbele ya Farao,+ lakini Yehova aliuacha moyo wa Farao uwe mkaidi, hivi kwamba hakuwaruhusu Waisraeli waondoke katika nchi yake.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “atakayeunoa ulimi wake dhidi ya.”