Kutoka 13:1-22

  • Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume ni wa Yehova (1, 2)

  • Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu (3-10)

  • Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atolewa kwa Mungu (11-16)

  • Waisraeli waelekezwa kwenye Bahari Nyekundu (17-20)

  • Nguzo ya wingu na moto (21, 22)

13  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Nitakasie* kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Waisraeli. Mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mwanadamu na mnyama ni wangu.”+  Ndipo Musa akawaambia watu: “Kumbukeni siku hii mliyotoka Misri,+ kutoka katika nyumba ya utumwa, kwa sababu kwa mkono wenye nguvu Yehova aliwatoa katika nchi hii.+ Kwa hiyo hampaswi kula kitu chochote kilichotiwa chachu.  Mnatoka Misri siku ya leo, mwezi wa Abibu.*+  Mnapaswa kuiadhimisha siku hii katika mwezi huu, Yehova atakapowaleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi, na Wayebusi,+ nchi aliyowaapia mababu zenu kwamba atawapa ninyi,+ nchi inayotiririka maziwa na asali.+  Kwa siku saba mtakula mikate isiyo na chachu,+ na katika siku ya saba, mtamfanyia Yehova sherehe.  Mikate isiyo na chachu inapaswa kuliwa kwa siku hizo saba;+ nanyi msipatikane na kitu chochote kilicho na chachu+ wala unga wowote uliokandwa uliotiwa chachu katika eneo lenu lote.*  Na siku hiyo unapaswa kumwambia mwanao, ‘Ni kwa sababu ya mambo ambayo Yehova alinitendea nilipotoka Misri.’+  Nayo itakuwa ishara mkononi mwako na ukumbusho kwenye paji la uso wako,*+ ili sheria ya Yehova iwe kinywani mwako, kwa sababu kwa mkono wenye nguvu Yehova alikutoa Misri. 10  Unapaswa kuishika sheria hii kwa wakati wake uliowekwa, mwaka baada ya mwaka.+ 11  “Yehova atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, ambayo amekuapia wewe na mababu zako kwamba atakupa,+ 12  ni lazima umtolee Yehova kila mzaliwa wa kwanza wa kiume,* na pia kila mnyama dume wa mifugo yako anayezaliwa kwanza. Wazaliwa hao wa kiume ni wa Yehova.+ 13  Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa kondoo, na usipomkomboa, basi unapaswa kumvunja shingo. Nawe unapaswa kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wanao.+ 14  “Mwanao akikuuliza baadaye, ‘Jambo hili linamaanisha nini?’ basi unapaswa kumwambia, ‘Kwa mkono wenye nguvu Yehova alitutoa Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+ 15  Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu tuondoke,+ Yehova alimuua kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mpaka mzaliwa wa kwanza wa mnyama.+ Ndiyo sababu ninamtolea Yehova wazaliwa wote wa kwanza wa kiume* kuwa dhabihu, na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza kati ya wanangu.’ 16  Hiyo inapaswa kuwa ishara mkononi mwako na utepe kwenye paji la uso wako,*+ kwa sababu kwa mkono wenye nguvu Yehova alitutoa Misri.” 17  Basi Farao alipowaruhusu Waisraeli waondoke, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa ilikuwa fupi. Kwa maana Mungu alisema: “Watu hawa wakikabili vita huenda wakabadili mawazo yao na kurudi Misri.” 18  Kwa hiyo Mungu akawafanya wazunguke kupitia njia ya nyikani inayoelekea kwenye Bahari Nyekundu.+ Lakini Waisraeli waliondoka katika nchi ya Misri wakiwa wamejipanga kivita. 19  Pia Musa alibeba mifupa ya Yosefu, kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha hivi wana wa Israeli: “Mungu hatakosa kamwe kuwakazia uangalifu, nanyi mnapaswa kuiondoa huku mifupa yangu na kwenda nayo.”+ 20  Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi Ethamu, ukingoni mwa nyika. 21  Sasa Yehova alikuwa akiwatangulia mchana katika nguzo ya wingu ili awaongoze njiani,+ na wakati wa usiku katika nguzo ya moto ili awape nuru, waweze kusafiri mchana na usiku.+ 22  Ile nguzo ya wingu haikuwa ikiondoka mbele ya watu wakati wa mchana, wala nguzo ya moto wakati wa usiku.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Niwekee kando; Nitengee.”
Tnn., “katika mipaka yenu yote.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”
Tnn., “kila kifungua mimba.”
Tnn., “kila kifungua mimba.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”