Kutoka 15:1-27

  • Musa na Waisraeli waimba wimbo wa ushindi (1-19)

  • Miriamu aimba akiwaitikia wanaume (20, 21)

  • Maji machungu yageuzwa kuwa matamu (22-27)

15  Wakati huo Musa na Waisraeli wakamwimbia Yehova wimbo huu:+ “Acheni nimwimbie Yehova, kwa maana amekwezwa sana.+ Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.+   Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,* kwa maana amekuwa wokovu wangu.+ Huyu ni Mungu wangu, nitamsifu;+ Mungu wa baba yangu,+ nitamkweza.+   Yehova ni shujaa mwenye nguvu.+ Yehova ndilo jina lake.+   Ametupa baharini magari ya vita ya Farao na jeshi lake,+Na mashujaa wake bora kabisa wamezama katika Bahari Nyekundu.+   Mawimbi makubwa yaliwafunika; wakazama vilindini kama jiwe.+   Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, una nguvu nyingi;+Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumvunjavunja adui.   Katika fahari yako kuu unaweza kuwaangusha chini wale wanaoinuka juu dhidi yako;+Unaituma hasira yako inayowaka, nayo inawala kama majani makavu.   Kwa pumzi moja kutoka katika mianzi ya pua yako maji yalikusanyika pamoja;Yalisimama tuli, yakazuia mafuriko;Mawimbi makubwa yaligandamana katikati ya bahari.   Adui alisema, ‘Nitawafuatia! Nitawafikia! Nitagawanya nyara mpaka nitakapotosheka! Nitauchomoa upanga wangu! Mkono wangu utawatiisha!’+ 10  Ulipuliza bahari kwa pumzi yako, ikawafunika;+Walizama kama madini ya risasi katika maji makuu. 11  Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+ Ni nani aliye kama wewe, unayejidhihirisha mwenyewe kuwa mkuu katika utakatifu?+ Wewe unayestahili kuogopwa kwa nyimbo za sifa, Wewe unayetenda mambo yanayostaajabisha.+ 12  Uliunyoosha mkono wako wa kuume, dunia ikawameza kabisa.+ 13  Kwa upendo wako mshikamanifu umewaongoza watu uliowakomboa;+Kwa nguvu zako utawaongoza kwenye makao yako matakatifu. 14  Ni lazima mataifa yasikie;+ yatatetemeka;Wakaaji wa Ufilisti watashikwa na maumivu makali.* 15  Wakati huo mashehe* wa Edomu wataogopa sana,Na watawala wenye nguvu* wa Moabu watatetemeka.+ Wakaaji wote wa Kanaani watavunjika moyo.+ 16  Watashikwa na woga na hofu.+ Kwa sababu ya ukuu wa mkono wako watatulia kama jiweMpaka watu wako watakapopita, Ee Yehova,Mpaka watu uliowatokeza+ watakapopita.+ 17  Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako,+Mahali pa kudumu ulipotayarisha pawe makao yako, Ee Yehova,Mahali patakatifu, Ee Yehova, ambapo umepajenga imara kwa mikono yako. 18  Yehova atatawala akiwa mfalme milele na milele.+ 19  Farasi wa Farao na magari yake ya vita na askari wake wapanda farasi walipoingia baharini,+Ndipo Yehova alipoyarudisha maji ya bahari yakawafunika,+Lakini Waisraeli walitembea kwenye nchi kavu katikati ya bahari.”+ 20  Kisha nabii Miriamu, dada ya Haruni, akachukua tari, na wanawake wote wakamfuata wakiwa na matari yao wakicheza dansi. 21  Miriamu akaimba hivi akiwaitikia wanaume: “Mwimbieni Yehova, kwa maana amekwezwa sana.+ Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.”+ 22  Baadaye Musa akawaongoza Waisraeli kutoka katika Bahari Nyekundu, wakaenda katika nyika ya Shuri na kusafiri kwa siku tatu nyikani, lakini hawakupata maji. 23  Wakafika Mara,*+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu alipaita mahali hapo Mara. 24  Basi watu wakaanza kumnung’unikia Musa,+ wakisema: “Tutakunywa nini?” 25  Musa akamlilia Yehova,+ naye Yehova akamwelekeza kwenye mti fulani. Alipoutupa ndani ya maji hayo, yakawa matamu. Huko Mungu akawawekea sharti na msingi wa hukumu, na huko Mungu akawajaribu.+ 26  Alisema: “Ikiwa mtaisikiliza kwa makini sauti yangu mimi, Yehova Mungu wenu na kufanya yaliyo sawa machoni pangu na kusikiliza kwa makini amri zangu na kushika masharti yangu yote,+ sitawaletea ugonjwa wowote ambao niliwaletea Wamisri,+ kwa sababu mimi, Yehova, ninawaponya.”+ 27  Baada ya hapo wakafika Elimu, mahali palipokuwa na chemchemi 12 za maji na mitende 70. Kwa hiyo wakapiga kambi hapo kando ya maji.

Maelezo ya Chini

“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “uchungu wa kuzaa.”
Shehe alikuwa mkuu wa kabila.
Au “watawala wa mabavu.”
Maana yake “Uchungu.”