Kutoka 17:1-16

  • Walalamika kuhusu ukosefu wa maji huko Horebu (1-4)

  • Maji yatoka mwambani (5-7)

  • Waamaleki wawashambulia na kuwashinda (8-16)

17  Kusanyiko lote la Waisraeli likaondoka katika nyika ya Sini+ hatua kwa hatua kama Yehova alivyoagiza,+ wakapiga kambi Refidimu.+ Lakini watu hawakuwa na maji ya kunywa.  Basi watu wakaanza kugombana na Musa+ wakisema: “Tupe maji ya kunywa!” Lakini Musa akawauliza: “Kwa nini mnagombana nami? Kwa nini mnaendelea kumjaribu Yehova?”+  Lakini watu walikuwa na kiu sana mahali hapo, nao wakaendelea kumnung’unikia Musa+ wakisema: “Kwa nini umetupandisha kutoka Misri ili kutuua kwa kiu sisi na wana wetu na mifugo yetu?”  Mwishowe Musa akamlilia Yehova akisema: “Nifanye nini na watu hawa? Hivi punde watanipiga mawe!”  Kisha Yehova akamwambia Musa: “Nenda mbele ya watu, wachukue wazee kadhaa wa Israeli na fimbo yako uliyotumia kupiga maji ya Mto Nile.+ Ibebe mkononi mwako na uendelee kutembea.  Tazama! Nitakuwa nimesimama mbele yako kwenye mwamba huko Horebu. Unapaswa kuupiga mwamba huo, na maji yatatoka ndani yake, kisha watu watayanywa.”+ Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli.  Basi akapaita mahali hapo Masa*+ na Meriba,*+ kwa sababu ya ugomvi wa Waisraeli na kwa sababu walimjaribu+ Yehova kwa kusema: “Je, Yehova yuko katikati yetu au la?”  Kisha Waamaleki+ wakaja na kupigana na Waisraeli huko Refidimu.+  Ndipo Musa akamwambia Yoshua:+ “Tuchagulie wanaume wakapigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima, nikiwa na fimbo ya Mungu wa kweli mkononi mwangu.” 10  Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia,+ akapigana na Waamaleki. Naye Musa, Haruni, na Huru+ wakapanda juu ya kilima. 11  Wakati wote ambapo Musa aliinua mikono yake, Waisraeli walishinda, lakini mara tu alipoishusha mikono yake, Waamaleki walishinda. 12  Mikono ya Musa ilipochoka, walichukua jiwe wakaliweka chini yake, akaketi juu ya jiwe hilo. Kisha Haruni na Huru, mmoja upande huu na mwingine upande mwingine, wakaitegemeza mikono yake, hivi kwamba mikono yake ikabaki imara mpaka jua lilipotua. 13  Kwa hiyo Yoshua akawashinda kwa upanga Waamaleki na watu walioshirikiana nao.+ 14  Sasa Yehova akamwambia Musa: “Andika jambo hili katika kitabu liwe ukumbusho,* na uliseme tena kwa Yoshua: ‘Nitawaangamiza kabisa Waamaleki kutoka chini ya mbingu, nao hawatakumbukwa tena.’”+ 15  Kisha Musa akajenga madhabahu na kuiita Yehova-nisi,* 16  na kusema: “Kwa sababu mkono wa Waamaleki unapinga kiti cha ufalme cha Yah,+ Yehova atapigana vita na Waamaleki kizazi baada ya kizazi.”+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”
Maana yake “Kugombana.”
Au “kikumbusho.”
Maana yake “Yehova Ni Nguzo Yangu ya Ishara.”