Kutoka 20:1-26

  • Amri Kumi (1-17)

  • Matukio ya ajabu yawaogopesha Waisraeli (18-21)

  • Maagizo kuhusu ibada (22-26)

20  Kisha Mungu akasema maneno haya yote:+  “Mimi ni Yehova Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa.+  Usiwe na miungu mingine yoyote ila mimi.*+  “Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa au mfano wa* kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani au kilicho ndani ya maji chini ya dunia.+  Usiviinamie wala kushawishiwa kuviabudu,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu ninayetaka watu waniabudu mimi peke yangu,+ nami huwaadhibu watoto kwa sababu ya makosa ya baba zao, kufikia kizazi cha tatu na kizazi cha nne cha wale wanaonichukia,  lakini ninawatendea kwa upendo mshikamanifu watu wanaonipenda na kushika amri zangu, kufikia kizazi cha elfu cha watu hao.+  “Usilitumie jina langu mimi, Yehova Mungu wako, kwa njia isiyofaa,+ kwa maana mimi, Yehova, sitakosa kumwadhibu yule anayelitumia jina langu kwa njia isiyofaa.+  “Ikumbuke siku ya Sabato na uione kuwa takatifu.+  Fanya shughuli na kazi zako zote kwa siku sita,+ 10  lakini siku ya saba ni sabato kwa Yehova Mungu wako. Usifanye kazi yoyote, wewe wala mwana wako wala binti yako wala mtumwa wako wala kijakazi wako wala mnyama wako wa kufugwa wala mgeni aliye katika makazi* yako.+ 11  Kwa maana kwa siku sita mimi, Yehova, niliumba mbingu na dunia, bahari, na vitu vyote vilivyomo, nami nikaanza kupumzika siku ya saba.+ Ndiyo sababu mimi Yehova niliibariki siku ya Sabato na kuifanya kuwa takatifu. 12  “Mheshimu baba yako na mama yako+ ili uishi muda mrefu katika nchi ambayo mimi Yehova Mungu wako ninakupa.+ 13  “Usiue.+ 14  “Usifanye uzinzi.+ 15  “Usiibe.+ 16  “Usitoe ushahidi wa uwongo dhidi ya jirani yako.+ 17  “Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako+ wala mtumwa wake wala kijakazi wake wala ng’ombe dume wake wala punda wake wala kitu chochote cha jirani yako.”+ 18  Sasa watu wote walikuwa wakishuhudia ngurumo na radi, sauti ya pembe, na mlima ukifuka moshi; na walipoona mambo hayo walitetemeka na kusimama mbali.+ 19  Basi wakamwambia Musa: “Wewe ongea nasi, tutasikiliza, lakini Mungu asiongee nasi tusije tukafa.”+ 20  Kwa hiyo Musa akawaambia watu: “Msiogope, kwa sababu Mungu wa kweli amekuja kuwajaribu,+ ili mwendelee kumwogopa, msitende dhambi.”+ 21  Kwa hiyo watu wakaendelea kusimama mbali, lakini Musa akalikaribia lile wingu jeusi mahali alipokuwa Mungu wa kweli.+ 22  Kisha Yehova akamwambia Musa: “Hivi ndivyo utakavyowaambia Waisraeli, ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimezungumza nanyi kutoka mbinguni.+ 23  Msijitengenezee miungu ya fedha na kuiabudu huku mkiniabudu mimi, wala msijitengenezee miungu ya dhahabu.+ 24  Mtanijengea madhabahu ya udongo, na juu yake mtanitolea dhabihu zenu za kuteketezwa, dhabihu zenu za ushirika,* kondoo, mbuzi, na ng’ombe wenu. Mahali popote nitakapochagua jina langu likumbukwe,+ nitawajia, nami nitawabariki. 25  Ikiwa mtanijengea madhabahu ya mawe, msiijenge kwa mawe yaliyokatwa kwa vifaa.*+ Kwa maana mkiyachonga kwa tindo, mtaitia madhabahu hiyo unajisi. 26  Nanyi msipande madhabahu yangu kwa ngazi, ili sehemu zenu za siri zisionekane* juu yake.’

Maelezo ya Chini

Au “na kuniasi mimi.” Tnn., “dhidi ya uso wangu.”
Au “umbo la.”
Tnn., “malango.”
Au “matoleo yenu ya amani.”
Au “yaliyochongwa.”
Tnn., “uchi wenu usionekane.”