Kutoka 22:1-31

  • Waisraeli wapewa sheria (1-31)

    • Kuhusu wizi (1-4)

    • Kuhusu kuharibu mazao (5, 6)

    • Kuhusu kulipia hasara na kumiliki mali (7-15)

    • Kuhusu kutongoza (16, 17)

    • Kuhusu ibada na kutenda haki katika jamii (18-31)

22  “Mtu akiiba ng’ombe dume au kondoo na kumchinja au kumuuza, atalipa ng’ombe dume watano kwa ajili ya ng’ombe dume huyo na kondoo wanne kwa ajili ya kondoo huyo.+  (“Mwizi+ akipatikana akivunja nyumba kisha apigwe na kufa, aliyemuua hatakuwa na hatia ya damu.  Lakini jambo hilo likitokea baada ya jua kuchomoza, atakuwa na hatia ya damu.) “Anapaswa kulipa. Ikiwa hana chochote, basi atauzwa ili kulipia vitu alivyoiba.  Kama mnyama aliyeibwa anapatikana akiwa hai mikononi mwake, awe ni ng’ombe dume au punda au kondoo, anapaswa kulipa mara mbili.  “Mtu yeyote akiwalisha wanyama wake katika shamba au shamba la mizabibu la mtu mwingine, atalipa kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au mazao bora ya shamba lake mwenyewe la mizabibu.  “Moto ukiwaka na kuenea katika vichaka vya miiba na kuteketeza masuke au nafaka iliyo shambani au shamba, yule aliyewasha moto huo lazima alipie kilichoteketea.  “Mtu akimpa jirani yake pesa au vitu amtunzie, navyo viibwe kutoka katika nyumba ya jirani huyo, mwizi akipatikana, lazima alipe mara mbili.+  Mwizi asipopatikana, mwenye nyumba ataletwa mbele za Mungu wa kweli+ ili ithibitishwe ikiwa alichukua vitu vya jirani yake au la.  Katika visa vyote vya kumiliki vitu isivyo halali, iwe ni ng’ombe dume, punda, kondoo, nguo, au kitu chochote kilichopotea ambacho huenda mtu akasema, ‘Hiki ni changu!’ wote wawili wataleta kesi yao mbele za Mungu wa kweli.+ Yule ambaye Mungu atasema ana hatia atamlipa jirani yake mara mbili.+ 10  “Mtu akimpa jirani yake punda au ng’ombe dume au kondoo au mnyama yeyote wa kufugwa amtunzie, kisha mnyama huyo afe au alemazwe au achukuliwe bila mtu yeyote kuona, 11  yule aliyepewa mali hiyo ataapa mbele za Yehova kwamba hakuchukua mali ya jirani yake; na mwenye mali anapaswa kukubali jambo hilo. Mtu huyo hatalipa chochote.+ 12  Lakini ikiwa mnyama huyo ameibwa kutoka kwake, atamlipa mwenye mnyama huyo. 13  Ikiwa mnyama huyo aliraruliwa na mnyama wa mwituni, atamleta kama ushahidi. Hatalipia kitu kilichoraruliwa na mnyama wa mwituni. 14  “Lakini mtu yeyote akiazima mnyama kutoka kwa jirani yake, na mnyama huyo alemazwe au afe wakati mwenyewe hayupo, aliyeazima mnyama huyo lazima alipe. 15  Ikiwa mwenyewe yupo, aliyeazima hatalipa. Ikiwa mnyama huyo alikodiwa, pesa iliyolipwa ili kumkodi ndiyo itakayokuwa malipo yake. 16  “Sasa mwanamume akimtongoza bikira ambaye hajachumbiwa kisha alale naye, lazima alipe mahari ili msichana huyo awe mke wake.+ 17  Baba yake akikataa kabisa kumpa msichana huyo, mwanamume huyo atalipa kiasi cha pesa kinacholingana na mahari. 18  “Hampaswi kumwacha mwanamke mchawi aishi.+ 19  “Mtu yeyote anayefanya ngono na mnyama lazima auawe.+ 20  “Mtu yeyote anayetoa dhabihu kwa miungu mingine isipokuwa kwa Yehova peke yake lazima auawe.+ 21  “Msimtese wala kumkandamiza mkaaji mgeni,+ kwa sababu ninyi mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+ 22  “Msimtese mjane wala yatima.+ 23  Mkimtesa hata kidogo, naye anililie, hakika nitasikia kilio chake;+ 24  nami nitawaka hasira, nami nitawaua kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane, na watoto wenu watakuwa mayatima. 25  “Ukimkopesha pesa mtu yeyote maskini miongoni mwa watu wangu, mtu anayeishi nawe, usiwe kama mtu anayemkopesha pesa.* Hupaswi kumtoza riba.+ 26  “Ukichukua nguo ya jirani yako kuwa dhamana ya mkopo,*+ unapaswa kumrudishia kabla ya jua kutua. 27  Kwa sababu hiyo ndiyo nguo pekee aliyo nayo ya kujifunika, nguo ya kufunika mwili wake,* atajifunikia nini anapolala?+ Akinililia, hakika nitasikia, kwa sababu mimi ni mwenye huruma.*+ 28  “Usimtukane Mungu+ wala kumlaani kiongozi* miongoni mwa watu wako.+ 29  “Usisite kutoa matoleo kutoka katika mazao yako mengi na kutoka kwenye mafuriko ya mashinikizo yako.*+ Unapaswa kunipa mzaliwa wa kwanza kati ya wanao.+ 30  Hivi ndivyo utakavyofanya kuhusu ng’ombe dume wako na kondoo wako:+ Atakaa na mama yake kwa siku saba. Siku ya nane, utanipa mimi.+ 31  “Mnapaswa kujithibitisha wenyewe kuwa watu watakatifu mbele zangu,+ nanyi hampaswi kula nyama ya mnyama yeyote ambaye ameraruliwa na mnyama wa mwituni.+ Mnapaswa kuwatupia mbwa nyama hiyo.

Maelezo ya Chini

Au “mla riba.”
Au “rehani.”
Tnn., “ngozi yake.”
Au “neema.”
Au “mtawala.”
Yaani, mashinikizo ya mafuta na mashinikizo ya divai.