Kutoka 23:1-33

  • Waisraeli wapewa sheria (1-19)

    • Kuhusu unyoofu na kutenda wema (1-9)

    • Kuhusu sabato na sherehe mbalimbali (10-19)

  • Waisraeli waongozwa na malaika (20-26)

  • Kuimiliki nchi na mipaka ya nchi (27-33)

23  “Usieneze habari za uwongo.+ Usishirikiane na mtu mwovu kwa kutoa ushahidi utakaowadhuru wengine.+  Usiufuate umati ili kutenda maovu, wala usipotoshe haki kwa kutoa ushahidi wa uwongo ili uunge mkono umati.*  Usionyeshe upendeleo katika kesi ya mtu maskini.+  “Ukikutana na ng’ombe dume au punda wa adui yako akitangatanga, unapaswa kumrudisha kwake.+  Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia amelemewa na mzigo na kuanguka, usimpuuze na kwenda zako. Unapaswa kumsaidia kufungua mnyama huyo.+  “Usipotoshe uamuzi wa kesi ya maskini aliye miongoni mwenu.+  “Jiepushe kabisa na shtaka* la uwongo, na usimuue mtu asiye na hatia na pia mwadilifu, kwa maana sitamtangaza mwovu kuwa mwadilifu.*+  “Hupaswi kukubali rushwa, kwa maana rushwa huwapofusha watu wanaoona vizuri na inaweza kupotosha maneno ya watu wenye haki.+  “Hupaswi kumkandamiza mkaaji mgeni. Mnajua jinsi mgeni anavyohisi,* kwa sababu mlikuwa wakaaji wageni katika nchi ya Misri.+ 10  “Kwa miaka sita utapanda mbegu katika shamba lako na kuvuna mazao yake.+ 11  Lakini mwaka wa saba hutalilima, utaliacha lipumzike, nao maskini walio miongoni mwa watu wako watapata chakula humo, na watakachoacha kitaliwa na wanyama wa mwituni. Hivyo ndivyo utakavyolifanyia shamba lako la mizabibu na shamba lako la mizeituni. 12  “Kwa siku sita utafanya kazi zako; lakini siku ya saba hutafanya kazi, ili ng’ombe dume wako na punda wako wapumzike na mwana wa kijakazi wako na mkaaji mgeni waweze kujiburudisha.+ 13  “Unapaswa kuwa mwangalifu kufanya mambo yote niliyokuambia,+ nawe hupaswi kutaja majina ya miungu mingine; yasisikike midomoni*+ mwako. 14  “Unapaswa kunifanyia sherehe mara tatu kwa mwaka.+ 15  Utaadhimisha Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu.+ Utakula mikate isiyo na chachu kwa siku saba, kama nilivyokuamuru, wakati uliowekwa katika mwezi wa Abibu,*+ kwa sababu ulitoka Misri wakati huo. Mtu yeyote asije mbele zangu mikono mitupu.+ 16  Pia, unapaswa kuadhimisha Sherehe ya Mavuno* ya matunda ya kwanza yaliyoiva* ya kazi zako, na ya vitu unavyopanda shambani;+ na Sherehe ya Kukusanya* mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mazao ya kazi zako.+ 17  Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuja mbele za Bwana wa kweli, Yehova.+ 18  “Hupaswi kutoa damu ya dhabihu yangu pamoja na kitu chochote kilichotiwa chachu. Na dhabihu za mafuta zinazotolewa katika sherehe zangu hazipaswi kukaa usiku kucha mpaka asubuhi. 19  “Unapaswa kuleta katika nyumba yangu mimi, Yehova Mungu wako, mazao bora ya kwanza yaliyokomaa* ya ardhi yako.+ “Usimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.+ 20  “Ninamtuma malaika awatangulie+ ili awalinde safarini na kuwapeleka mahali nilipotayarisha.+ 21  Msikilizeni, na mtii sauti yake. Msimwasi, kwa maana hatawasamehe maasi yenu,+ kwa sababu jina langu limo ndani yake. 22  Hata hivyo, mkiitii kabisa sauti yake na kufanya yote ninayowaambia, nitakuwa adui wa maadui wenu na kuwapinga wale wanaowapinga. 23  Kwa maana malaika wangu atawatangulia na kuwapeleka katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi, na Wayebusi, nami nitawaangamiza.+ 24  Hampaswi kuiinamia miungu yao wala kushawishiwa kuiabudu, nanyi hampaswi kuiga mazoea yao.+ Badala yake, mnapaswa kuharibu kabisa sanamu zao na kuvunjavunja nguzo zao takatifu.+ 25  Mnapaswa kunitumikia mimi, Yehova Mungu wenu,+ nami nitabariki mkate wenu na maji yenu.+ Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.+ 26  Hakuna mwanamke katika nchi yenu ambaye mimba yake itaharibika wala atakayekuwa tasa,+ nami nitawapa maisha marefu.* 27  “Nitafanya watu waniogope hata kabla hamjafika,+ nami nitawavuruga watu wote mtakaokutana nao, nami nitawafanya maadui wenu wote washindwe na kukimbia.*+ 28  Nitawafanya Wahivi, Wakanaani, na Wahiti wavunjike moyo* kabla hamjafika,+ nao watawakimbia.+ 29  Sitawafukuza watoke mbele yenu kwa mwaka mmoja, ili nchi isibaki ukiwa na wanyama wa mwituni waongezeke na kuwashambulia.+ 30  Nitawafukuza hatua kwa hatua kutoka mbele yenu, mpaka mtakapoongezeka na kuwa wengi na kuimiliki nchi hiyo.+ 31  “Nitaweka mpaka wenu kuanzia Bahari Nyekundu mpaka bahari ya Wafilisti na kuanzia nyikani mpaka kwenye Mto Efrati;+ kwa maana nitawatia wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, nanyi mtawafukuza kutoka mbele yenu.+ 32  Hampaswi kufanya agano pamoja nao wala na miungu yao.+ 33  Hawapaswi kuishi katika nchi yenu, wasije wakasababisha mnitendee dhambi. Mkiiabudu miungu yao, kwa hakika itakuwa mtego kwenu.”+

Maelezo ya Chini

Au “ushahidi unaoungwa mkono na wengi.”
Tnn., “neno.”
Au “sitamwondolea mashtaka mtu mwovu.”
Au “Mnajua maisha (nafsi) ya mgeni.”
Tnn., “kinywani.”
Pia inaitwa Sherehe ya Vibanda (Mahema).
Au “mazao ya kwanza yaliyokomaa.”
Pia inaitwa Sherehe ya Majuma, au Pentekoste.
Au “matunda ya kwanza bora yaliyoiva.”
Au “nitafanya idadi ya siku zenu iwe kamili.”
Au “nitawafanya maadui wenu wote wawageuzie mgongo.”
Au labda, “washikwe na wasiwasi; waogope.”