Kutoka 27:1-21

  • Madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa (1-8)

  • Ua (9-19)

  • Mafuta kwa ajili ya taa (20, 21)

27  “Utatengeneza madhabahu kwa mbao za mshita;+ itakuwa na urefu wa mikono mitano* na upana wa mikono mitano. Madhabahu hiyo itakuwa ya mraba na kimo chake kitakuwa mikono mitatu.+  Utatengeneza pembe+ kwenye ncha zake nne; pembe hizo zitakuwa sehemu ya madhabahu, nawe utaifunika madhabahu hiyo kwa shaba.+  Utatengeneza ndoo za kuondolea majivu,* pia sepetu, mabakuli, nyuma,* na vyetezo; utatengeneza vyombo vyote vya madhabahu kwa shaba.+  Nawe utatengeneza wavu wa shaba kwa ajili ya madhabahu, pia utatengeneza pete nne za shaba kwenye pembe nne za wavu huo.  Nawe utauweka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu, nao utashuka ndani ya madhabahu kufikia katikati.  Utatengeneza fito za mshita kwa ajili ya madhabahu na kuzifunika kwa shaba.  Fito hizo zitaingizwa kwenye zile pete ili ziwe katika pande mbili za madhabahu wakati inapobebwa.+  Utaitengeneza madhabahu hiyo kama sanduku la mbao lenye uwazi. Inapaswa kutengenezwa kama tu Alivyokuonyesha mlimani.+  “Utatengeneza ua wa hema+ la ibada. Upande wa kusini, ua huo utakuwa na mapazia yanayoning’inia ya kitani bora kilichosokotwa; yatakuwa na urefu wa mikono 100 upande mmoja.+ 10  Ua huo utakuwa na nguzo 20 na vikalio 20 vya shaba. Kulabu za nguzo hizo pamoja na vitanzi* vyake vitakuwa vya fedha. 11  Mapazia yanayoning’inia upande wa kaskazini yatakuwa pia na urefu wa mikono 100, pamoja na nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vya shaba, lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vitakuwa vya fedha. 12  Upande wa magharibi wa ua utakuwa na mapazia yanayoning’inia yenye urefu wa mikono 50, na nguzo 10 na vikalio 10. 13  Ua utakuwa na upana wa mikono 50 upande wa mashariki, yaani, upande wa mapambazuko ya jua. 14  Mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15 yatakuwa upande mmoja, pamoja na nguzo tatu na vikalio vitatu.+ 15  Upande wa pili utakuwa na mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15, pamoja na nguzo tatu na vikalio vitatu. 16  “Mlango wa ua utakuwa na pazia lenye urefu wa mikono 20 lililotengenezwa kwa nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora kilichosokotwa na kufumwa,+ pamoja na nguzo nne na vikalio vyake vinne.+ 17  Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na kulabu na vitanzi vya fedha, lakini vikalio vyake vitakuwa vya shaba.+ 18  Ua huo utakuwa na urefu wa mikono 100,+ upana wa mikono 50, na kimo cha mikono 5, nao utatengenezwa kwa kitani bora kilichosokotwa, na utakuwa na vikalio vya shaba. 19  Vyombo na vitu vyote vitakavyotumiwa katika utumishi wa hema la ibada, pamoja na vigingi vyote vya hema na vya ua, vitakuwa vya shaba.+ 20  “Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni zilizopondwa ili taa ziwake daima.+ 21  Katika hema la mkutano, nje ya pazia lililo karibu na sanduku la Ushahidi,+ Haruni na wanawe watahakikisha kwamba taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Yehova.+ Hiyo ni sheria ya kudumu katika vizazi vyao vyote itakayotekelezwa na Waisraeli.+

Maelezo ya Chini

Mkono mmoja ulilingana na sentimita 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Au “majivu yenye mafuta,” yaani, majivu yaliyojaa mafuta ya dhabihu.
Wingi wa kifaa kinachoitwa uma.
Au “pete; vitanzi; vibanio” vya kushikia.
Au “pete; vitanzi; vibanio” vya kushikia.