Kutoka 31:1-18

  • Mafundi wajazwa roho ya Mungu (1-11)

  • Sabato, ishara kati ya Mungu na Waisraeli (12-17)

  • Mabamba mawili ya mawe (18)

31  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Tazama, nimemchagua* Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+  Nitamjaza roho ya Mungu, na kumpa hekima, uelewaji, na ujuzi katika kila aina ya ufundi,  ili abuni kazi za usanii akitumia dhahabu, fedha, na shaba,  ili achonge na kupamba kwa mawe,+ na kutengeneza vifaa vya mbao vya kila aina.+  Pia, nimemchagua Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani ili amsaidie, nami ninaweka hekima katika mioyo ya wote wenye ustadi,* ili watengeneze kila kitu nilichokuamuru:+  hema la mkutano,+ sanduku la Ushahidi+ na kifuniko chake,+ vyombo vyote vya hema,  meza+ na vyombo vyake, kinara cha taa cha dhahabu safi na vyombo vyake vyote,+ madhabahu ya uvumba,+  madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa+ na vyombo vyake vyote, beseni na kinara chake,+ 10  yale mavazi bora yaliyofumwa, mavazi matakatifu ya kuhani Haruni, mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani,+ 11  mafuta yanayotumiwa kutia mafuta, na ule uvumba wenye manukato kwa ajili ya mahali patakatifu.+ Watafanya mambo yote niliyokuamuru.” 12  Yehova akaendelea kumwambia Musa: 13  “Waambie Waisraeli, ‘Mnapaswa hasa kushika sabato zangu,+ kwa maana ni ishara kati yangu pamoja nanyi katika vizazi vyenu ili mjue kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa ninyi. 14  Ni lazima mshike Sabato kwa sababu ni takatifu kwenu.+ Mtu yeyote atakayeitia unajisi ni lazima auawe. Mtu yeyote atakayefanya kazi siku hiyo, ni lazima auawe kutoka kati ya watu wake.+ 15  Mnaweza kufanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba ni sabato ya pumziko kamili.+ Ni takatifu kwa Yehova. Mtu yeyote atakayefanya kazi siku ya Sabato ni lazima auawe. 16  Ni lazima Waisraeli washike Sabato; ni lazima waadhimishe Sabato katika vizazi vyao vyote. Ni agano la kudumu. 17  Ni ishara ya kudumu kati yangu na Waisraeli,+ kwa sababu katika siku sita mimi, Yehova, niliziumba mbingu na dunia na katika siku ya saba nilipumzika na kustarehe.’”+ 18  Sasa mara tu alipomaliza kuzungumza naye kwenye Mlima Sinai, alimpa Musa mabamba mawili ya Ushahidi,+ mabamba ya mawe yaliyoandikwa kwa kidole cha Mungu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “nimemwita kwa jina.”
Au “wenye hekima moyoni.”