Kutoka 35:1-35

  • Maagizo kuhusu Sabato (1-3)

  • Michango ya hema la ibada (4-29)

  • Bezaleli na Oholiabu wajazwa roho (30-35)

35  Baadaye Musa akalikusanya pamoja kusanyiko lote la Waisraeli na kuliambia: “Haya ndiyo mambo ambayo Yehova ameamuru yafanywe:+  Mtafanya kazi kwa siku sita, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, ni sabato ya pumziko kamili kwa Yehova.+ Mtu yeyote atakayefanya kazi siku hiyo atauawa.+  Hampaswi kuwasha moto katika makao yenu yoyote siku ya Sabato.”  Kisha Musa akaliambia kusanyiko lote la Waisraeli: “Yehova ameamuru hivi:  ‘Mtoleeni Yehova mchango kutoka miongoni mwenu.+ Kila mtu aliye na moyo wa kutoa kwa hiari+ na amletee Yehova mchango wa dhahabu, fedha, shaba,  nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, kitani bora, manyoya ya mbuzi,+  ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za sili, mbao za mshita,  mafuta kwa ajili ya taa, mafuta ya zeri ya kutengenezea mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na uvumba uliotiwa manukato,+  mawe ya shohamu, na mawe mengine ya kupambia efodi+ na kifuko cha kifuani.+ 10  “‘Watu wote ambao ni stadi*+ kati yenu na waje kutengeneza kila kitu ambacho Yehova ameamuru, 11  yaani, hema la ibada na kifuniko chake, kulabu zake na viunzi vyake vya mbao, fito zake, nguzo zake, na vikalio vyake; 12  Sanduku la Agano+ na fito zake,+ kifuniko,+ na pazia+ linalofunika sanduku hilo; 13  meza+ na fito zake na vyombo vyake vyote na mikate ya wonyesho;+ 14  kinara cha taa+ na vyombo vyake na taa zake na mafuta yake;+ 15  madhabahu ya uvumba+ na fito zake; mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na uvumba uliotiwa manukato;+ pazia la mlango wa hema la ibada; 16  madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa+ na wavu wake wa shaba, fito zake na vyombo vyake vyote; beseni na kinara chake;+ 17  mapazia ya ua yanayoning’inia,+ nguzo zake na vikalio vyake; pazia la mlango wa ua; 18  vigingi vya hema la ibada na vigingi vya ua na kamba zake;+ 19  mavazi yaliyofumwa kwa ustadi+ ya kuhudumu mahali patakatifu, mavazi matakatifu ya kuhani Haruni,+ na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.’” 20  Kwa hiyo kusanyiko lote la Waisraeli likaondoka mbele ya Musa. 21  Basi kila mtu ambaye moyo wake ulimsukuma+ na kila mtu aliyechochewa na roho yake akaja na kumletea Yehova mchango ili utumiwe katika kazi ya hema la mkutano, yaani, katika utumishi wake wote, na kwa ajili ya mavazi matakatifu. 22  Nao wakaendelea kuja, wanaume pamoja na wanawake, kila mtu aliyekuwa na moyo wa kutoa kwa hiari akaleta bizimu, vipuli, pete, na vito vingine, kutia ndani vito vya dhahabu vya kila aina. Wote wakamletea Yehova matoleo yao* ya dhahabu.+ 23  Na wote waliokuwa na nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, kitani bora, manyoya ya mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za sili, wakaleta vitu hivyo. 24  Wote waliotoa fedha na shaba wakaleta mchango wa Yehova, na wote waliokuwa na mbao za mshita za kutumiwa katika kazi yoyote ile wakazileta. 25  Wanawake wote wenye ustadi+ wa kusokota wakasokota kwa mikono yao na kuleta vitu walivyosokota: nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora. 26  Na wanawake wote wenye ustadi ambao walisukumwa na mioyo yao wakasokota manyoya ya mbuzi. 27  Nao wakuu wakaleta mawe ya shohamu na mawe mengine ya kupambia efodi na kifuko cha kifuani,+ 28  na mafuta ya zeri na mafuta kwa ajili ya taa na ya kutumiwa kutengenezea mafuta ya kutia mafuta+ na kwa ajili ya uvumba uliotiwa manukato.+ 29  Wanaume na wanawake wote waliochochewa na mioyo yao wakaleta kitu fulani kwa ajili ya kazi ambayo Yehova alimwamuru Musa ifanywe; Waisraeli walimletea Yehova vitu hivyo vikiwa toleo la hiari.+ 30  Kisha Musa akawaambia Waisraeli: “Tazameni, Yehova amemchagua Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+ 31  Amemjaza roho ya Mungu, amempa hekima, uelewaji, na ujuzi katika kila aina ya ufundi 32  ili abuni kazi za usanii akitumia dhahabu, fedha, na shaba, 33  ili achonge na kupamba kwa mawe, na kutengeneza vifaa vya mbao vya kila aina kwa usanii. 34  Naye ameweka moyoni mwake ustadi wa kufundisha, yeye na Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani. 35  Amewajaza ustadi wa*+ kufanya kazi zote za ufundi, kutarizi, na kufuma kwa nyuzi za bluu, sufu ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu, na kitani bora, na kazi zote za mfumaji. Wanaume hao watafanya kazi za kila aina na kubuni vyombo vya kila aina kwa ufundi.

Maelezo ya Chini

Au “wenye hekima moyoni.”
Au “matoleo yao ya kutikiswa.”
Au “hekima moyoni ya.”