Kutoka 4:1-31

  • Ishara tatu ambazo Musa angefanya (1-9)

  • Musa ahisi hastahili (10-17)

  • Musa arudi Misri (18-26)

  • Musa akutana tena na Haruni (27-31)

4  Hata hivyo, Musa akamwambia: “Lakini tuseme kwamba hawaniamini wala kuisikiliza sauti yangu,+ kwa maana watasema, ‘Yehova hakukutokea.’”  Ndipo Yehova akamuuliza: “Ni nini hicho kilicho mkononi mwako?” Akajibu: “Fimbo.”  Akamwambia: “Itupe chini.” Basi akaitupa chini, nayo ikawa nyoka;+ Musa akamkimbia.  Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Unyooshe mkono wako umkamate mkia.” Basi akaunyoosha mkono wake na kumkamata, nyoka huyo akawa fimbo mkononi mwake.  Kisha Mungu akamwambia: “Fanya hivyo ili waamini kwamba Yehova Mungu wa mababu zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo,+ amekutokea.”+  Tena Yehova akamwambia: “Tafadhali, utie mkono wako ndani ya mkunjo wa juu wa vazi lako.” Basi akautia mkono wake ndani ya mkunjo wa vazi lake. Alipoutoa, tazama, mkono wake ulikuwa umepigwa na ukoma, ukawa mweupe kama theluji!+  Kisha Mungu akamwambia: “Urudishe mkono wako kwenye mkunjo wa juu wa vazi lako.” Basi akaurudisha mkono wake ndani ya vazi lake. Alipoutoa katika vazi lake, ulikuwa umerudia hali yake na kuwa kama sehemu nyingine za mwili wake!  Mungu akasema: “Wasipokuamini au wakipuuza ishara ya kwanza, basi kwa hakika watatii ishara+ ya pili.  Lakini hata wasipoamini ishara hizo mbili na kukataa kuisikiliza sauti yako, utachota maji kutoka katika Mto Nile na kuyamwaga kwenye nchi kavu, na maji hayo yatakuwa damu kwenye nchi kavu.”+ 10  Sasa Musa akamwambia Yehova: “Ee Yehova, niwie radhi, lakini sijawahi kuwa msemaji mwenye ufasaha, tangu zamani na hata baada ya wewe kuzungumza nami mtumishi wako, kwa maana mimi si msemaji mzuri* na ulimi wangu ni mzito.”+ 11  Yehova akamuuliza: “Ni nani aliyemuumbia mwanadamu kinywa, au ni nani anayewafanya wawe bubu, viziwi, waone vizuri, au wawe vipofu? Je, si mimi, Yehova? 12  Basi nenda sasa, nami nitakuwa pamoja nawe utakapokuwa ukizungumza,* nami nitakufundisha unalopaswa kusema.”+ 13  Lakini akasema: “Ee Yehova, niwie radhi, tafadhali, mtume yeyote unayetaka kumtuma.” 14  Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Musa, akasema: “Namna gani ndugu yako Haruni,+ Mlawi? Ninajua kwamba anaweza kuzungumza vizuri sana. Na sasa yuko njiani anakuja hapa kukutana nawe. Atakapokuona, moyo wake utashangilia.+ 15  Basi unapaswa kuzungumza naye na kuweka maneno hayo kinywani mwake,+ nami nitakuwa pamoja nawe na yeye pia mnapozungumza,+ nami nitawafundisha jambo la kufanya. 16  Atazungumza na watu kwa niaba yako, naye atakuwa msemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.*+ 17  Nawe utachukua fimbo hii mkononi mwako na kuitumia kufanya zile ishara.”+ 18  Basi Musa akarudi kwa Yethro baba mkwe wake+ na kumwambia: “Ninataka kwenda, tafadhali, nirudi kwa ndugu zangu walio Misri nione kama wangali hai.” Yethro akamwambia Musa: “Nenda kwa amani.” 19  Basi Yehova akamwambia Musa huko Midiani: “Nenda, rudi Misri, kwa sababu watu wote waliotaka kukuua* wamekufa.”+ 20  Kisha Musa akamchukua mke wake na wanawe na kuwapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi nchini Misri. Pia, Musa aliichukua ile fimbo ya Mungu wa kweli mkononi mwake. 21  Halafu Yehova akamwambia Musa: “Baada ya kurudi Misri, hakikisha kwamba unafanya mbele ya Farao miujiza yote ambayo nimekupa nguvu za kuifanya.+ Lakini nitauacha moyo wake uwe mkaidi,+ naye hatawaruhusu watu hao waondoke.+ 22  Unapaswa kumwambia Farao, ‘Hivi ndivyo Yehova anavyosema: “Israeli ni mwanangu, mzaliwa wangu wa kwanza.+ 23  Ninakwambia, Mruhusu mwanangu aondoke ili anitumikie. Lakini ukikataa kumruhusu aondoke, nitamuua mwana wako, mzaliwa wako wa kwanza.”’”+ 24  Sasa walipokuwa njiani, mahali pa kulala, Yehova+ akakutana naye, na alikuwa akitafuta kumuua.+ 25  Hatimaye Sipora+ akachukua jiwe gumu lenye makali* na kumtahiri mwanawe, kisha akagusa miguu yake* kwa govi hilo na kusema: “Ni kwa sababu wewe ni bwana harusi wa damu kwangu.” 26  Basi Mungu akamwacha aende. Wakati huo Sipora akasema, “bwana harusi wa damu,” kwa sababu ya tohara hiyo. 27  Kisha Yehova akamwambia Haruni: “Nenda nyikani ukakutane na Musa.”+ Basi akaenda na kukutana naye kwenye mlima wa Mungu wa kweli+ na kumsalimu kwa busu. 28  Na Musa akamwambia Haruni maneno yote ya Yehova, aliyekuwa amemtuma,+ na ishara zote alizomwamuru afanye.+ 29  Kisha Musa na Haruni wakaenda kuwakusanya wazee wote wa Waisraeli.+ 30  Haruni akawaambia maneno yote ambayo Yehova alimwambia Musa, naye akafanya zile ishara+ machoni pa watu. 31  Kwa hiyo watu wakaamini.+ Waliposikia kwamba Yehova alikuwa amewaelekezea uangalifu Waisraeli+ na kwamba alikuwa ameona mateso yao,+ wakainama chini na kusujudu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “nina kinywa kizito.”
Tnn., “nitakuwa na kinywa chako.”
Au “atakuona kuwa mwakilishi wa Mungu.”
Au “waliokuwa wakiitafuta nafsi yako.”
Labda ni miguu ya malaika.
Au “kisu cha jiwe gumu.”