Kulingana na Luka 20:1-47

  • Wataka kujua chanzo cha mamlaka ya Yesu (1-8)

  • Mfano wa wakulima wauaji (9-19)

  • Mungu na Kaisari (20-26)

  • Swali kuhusu ufufuo (27-40)

  • Je, Kristo ni mwana wa Daudi? (41-44)

  • Onyo dhidi ya waandishi (45-47)

20  Siku moja alipokuwa akifundisha watu hekaluni na kutangaza habari njema, wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wakaja,  nao wakasema: “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Au ni nani aliyekupa mamlaka hayo?”+  Akawajibu: “Mimi pia nitawauliza swali, nanyi mnijibu:  Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”*  Wakaanza kujadiliana kati yao wakisema: “Tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Kwa nini hamkumwamini?’  Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini Yohana alikuwa nabii.”+  Basi wakamjibu kwamba hawajui chanzo chake.  Yesu akawaambia: “Nami siwaambii ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”  Yesu akaanza kuwaambia watu mfano huu: “Mtu fulani alipanda shamba la mizabibu+ akalikodisha kwa wakulima, kisha akasafiri kwenda ng’ambo, akakaa huko muda mrefu.+ 10  Majira yalipofika akamtuma mtumwa kwa wakulima ili wampe baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu. Hata hivyo, wale wakulima wakampiga na kumfukuza mikono mitupu.+ 11  Lakini akamtuma mtumwa mwingine. Huyo pia wakampiga, wakamwaibisha,* na kumfukuza mikono mitupu. 12  Bado tena akamtuma wa tatu; huyo pia walimjeruhi na kumtupa nje. 13  Ndipo mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa.+ Labda watamheshimu.’ 14  Wakulima walipomwona wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi tumuue, ili urithi wake uwe wetu.’ 15  Wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumuua.+ Kwa hiyo, mwenye shamba la mizabibu atawafanya nini? 16  Atakuja na kuwaua wakulima hao, kisha atawapa watu wengine shamba hilo la mizabibu.” Waliposikia hivyo wakasema: “Jambo hilo lisitukie kamwe!” 17  Lakini akawatazama moja kwa moja na kusema: “Basi, andiko hili linamaanisha nini: ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?*+ 18  Kila mtu anayeanguka kwenye jiwe hilo atavunjika vipandevipande.+ Na litamponda yeyote litakayemwangukia.” 19  Waandishi na wakuu wa makuhani walitambua kwamba mfano aliosema uliwahusu, basi walitaka kumkamata saa hiyo hiyo, lakini waliwaogopa watu.+ 20  Baada ya kumtazama kwa makini, wakatuma watu waliowakodi kisiri wajifanye kuwa waadilifu ili wamnase Yesu kwa maneno yake+ na kumkabidhi kwa serikali na kwa mamlaka ya gavana. 21  Nao wakamuuliza: “Mwalimu, tunajua wewe husema na kufundisha kwa usahihi na huna ubaguzi, bali unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli: 22  Je, ni halali* au si halali kwetu kumlipa Kaisari kodi?”* 23  Lakini alitambua ujanja wao na kuwaambia: 24  “Nionyesheni dinari.* Ina sura na maandishi ya nani?” Wakajibu: “Kaisari.” 25  Akawaambia: “Basi mlipeni Kaisari+ vitu vya Kaisari, na Mungu vitu vya Mungu.”+ 26  Kwa hiyo, wakashindwa kumnasa kwa maneno yake mbele ya watu, nao wakanyamaza wakiwa wameshangazwa na jibu lake. 27  Hata hivyo, baadhi ya Masadukayo, ambao husema hakuna ufufuo,+ wakaja na kumuuliza:+ 28  “Mwalimu, Musa alituandikia, ‘Ndugu ya mtu akifa na kumwacha mke, lakini hakuwa na mtoto, ndugu yake anapaswa kumchukua mke huyo ili kumwinulia ndugu yake uzao.’+ 29  Basi kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mwanamke lakini akafa bila mtoto. 30  Na wa pili 31  na wa tatu, wakamwoa mwanamke huyo. Vivyo hivyo wote saba; walikufa bila kupata watoto. 32  Mwishowe pia yule mwanamke akafa. 33  Kwa hiyo, katika ufufuo, atakuwa mke wa nani? Kwa maana wote saba walikuwa wamemwoa.” 34  Yesu akawaambia: “Watoto wa mfumo huu wa mambo* huoa na kuolewa, 35  lakini wale waliohesabiwa kuwa wanastahili kuupata mfumo huo wa mambo na kufufuliwa kutoka kwa wafu hawaoi wala kuolewa.+ 36  Kwa kweli, hawawezi kufa tena kamwe, kwa maana wao ni kama malaika, nao ni watoto wa Mungu kwa kuwa watoto wa ufufuo. 37  Lakini hata Musa alifunua kwamba wafu watafufuliwa, katika masimulizi kuhusu kichaka cha miiba, anapomwita Yehova* ‘Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’+ 38  Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa maana kwake,* wote wako hai.”+ 39  Baadhi ya waandishi wakasema: “Mwalimu, umesema vema.” 40  Kwa maana hawakuwa tena na ujasiri wa kumuuliza hata swali moja. 41  Naye akawauliza: “Kwa nini watu husema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 42  Kwa maana Daudi mwenyewe anasema katika kitabu cha Zaburi, ‘Yehova* alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume 43  mpaka niwaweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.”’+ 44  Basi, Daudi anamwita Bwana; kwa hiyo anawezaje kuwa mwanawe?” 45  Watu wote walipokuwa wakimsikiliza, akawaambia wanafunzi wake: 46  “Jihadharini na waandishi wanaopenda kutembea wakiwa wamevaa kanzu na wanaopenda kusalimiwa sokoni, na viti vya mbele* katika masinagogi na mahali penye heshima zaidi kwenye milo ya jioni,+ 47  na ambao humaliza nyumba* za wajane na kutoa sala ndefu ili waonekane.* Hao watapata hukumu kali* zaidi.”

Maelezo ya Chini

Au “chanzo chake ni wanadamu?”
Au “wakamvunjia heshima.”
Tnn., “kichwa cha pembeni.”
Au “sawa.”
Au “kodi ya kichwa.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “kwa maoni yake.”
Au “vilivyo bora.”
Au “mali.”
Au “kuwa kisingizio.”
Au “nzito.”