Mambo ya Walawi 15:1-33

  • Umajimaji unaotoka kwenye viungo vya uzazi (1-33)

15  Yehova akaendelea kuwaambia Musa na Haruni:  “Waambieni Waisraeli, ‘Mwanamume akitokwa na umajimaji kwenye kiungo chake cha uzazi,* umajimaji huo unamfanya asiwe safi.+  Yeye si safi kwa sababu ya umajimaji huo, iwe umajimaji huo unaendelea kutoka katika kiungo chake cha uzazi au umezuiwa kutoka, bado yeye si safi.  “‘Kitanda chochote anacholalia mtu anayetokwa na umajimaji hakitakuwa safi, na kitu chochote anachokalia hakitakuwa safi.  Mtu anayegusa kitanda cha mtu huyo ni lazima afue mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.+  Mtu yeyote anayeketi kwenye kitu kilichokaliwa na mtu anayetokwa na umajimaji anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.  Mtu yeyote anayemgusa mtu anayetokwa na umajimaji anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.  Mtu anayetokwa na umajimaji akimtemea mate mtu aliye safi, ni lazima mtu aliyetemewa mate ayafue mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.  Matandiko yoyote yaliyo mgongoni mwa mnyama yatakayokaliwa na mtu anayetokwa na umajimaji hayatakuwa safi. 10  Mtu yeyote anayegusa kitu chochote kilichokaliwa na mtu huyo hatakuwa safi mpaka jioni, na yeyote anayebeba vitu hivyo atafua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni. 11  Mtu anayetokwa na umajimaji+ akimgusa mtu mwingine bila kunawa mikono, ni lazima mtu aliyeguswa afue mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni. 12  Chombo cha udongo kinachoguswa na mtu anayetokwa na umajimaji kinapaswa kuvunjwa, na chombo chochote cha mbao kinapaswa kusafishwa kwa maji.+ 13  “‘Mtu aliyekuwa akitokwa na umajimaji akipona na kuwa safi, atangoja kwa siku saba ili atakaswe, na ni lazima afue mavazi yake na kuoga kwenye maji ya kijito, naye atakuwa safi.+ 14  Siku ya nane, anapaswa kuchukua njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga+ na kwenda mbele za Yehova, kwenye mlango wa hema la mkutano na kumpa kuhani ndege hao. 15  Kisha kuhani atamtoa ndege mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na ndege wa pili kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa, naye kuhani atamtolea mtu huyo dhabihu ya kufunika dhambi yake mbele za Yehova ili awe safi kutokana na umajimaji wake. 16  “‘Mwanamume akitokwa na shahawa, anapaswa kuoga mwili mzima kwenye maji naye hatakuwa safi mpaka jioni.+ 17  Ni lazima afue kwa maji vazi lolote na ngozi yoyote iliyomwagikiwa na shahawa, na vitu hivyo havitakuwa safi mpaka jioni. 18  “‘Mwanamume akilala na mwanamke kisha atokwe na shahawa, wote wawili wanapaswa kuoga kwenye maji na hawatakuwa safi mpaka jioni.+ 19  “‘Ikiwa mwanamke anatokwa na damu ya hedhi, hatakuwa safi kwa siku saba.+ Mtu yeyote anayemgusa hatakuwa safi mpaka jioni.+ 20  Kitu chochote anacholalia muda wote ambao yeye si safi kwa sababu ya hedhi hakitakuwa safi, na kila kitu anachokalia hakitakuwa safi.+ 21  Mtu yeyote anayegusa kitanda chake anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni. 22  Mtu yeyote anayegusa kitu chochote alichokalia mwanamke huyo anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni. 23  Ikiwa mwanamke huyo aliketi kwenye kitanda au kitu kingine, mwanamume anayekigusa hatakuwa safi mpaka jioni.+ 24  Mwanamume akilala na mwanamke huyo kisha damu ya hedhi imguse,+ mwanamume huyo hatakuwa safi kwa siku saba, na kitanda chochote anacholalia hakitakuwa safi. 25  “‘Mwanamke akitokwa na damu kwa siku nyingi+ wakati ambao si wa hedhi,+ au akitokwa na damu kwa muda unaozidi kipindi chake cha hedhi, hatakuwa safi sikuzote anazotokwa na damu, kama tu inavyokuwa wakati wa hedhi. 26  Kitanda chochote anacholalia na kitu chochote anachokalia anapotokwa na damu hakitakuwa safi,+ kitakuwa kama kinavyokuwa wakati wa hedhi. 27  Mtu yeyote anayegusa vitu hivyo hatakuwa safi, ni lazima afue mavazi yake na kuoga kwenye maji, naye hatakuwa safi mpaka jioni.+ 28  “‘Hata hivyo, damu yake ikiacha kutoka, atahesabu siku saba, na baada ya siku hizo atakuwa safi.+ 29  Siku ya nane, atachukua njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga+ na kumpelekea kuhani kwenye mlango wa hema la mkutano.+ 30  Kuhani atamtoa ndege mmoja kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na ndege wa pili kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa, kisha atamtolea mwanamke huyo dhabihu ya kufunika dhambi yake mbele za Yehova ili awe safi kutokana na damu yake.+ 31  “‘Kwa hiyo ni lazima muwalinde Waisraeli waepuke uchafu wao, ili wasife katika uchafu wao kwa kulitia unajisi hema langu la ibada ambalo liko kati yao.+ 32  “‘Hiyo ndiyo sheria kuhusu mtu anayetokwa na umajimaji, mwanamume asiye safi kwa sababu ya kutokwa na shahawa,+ 33  mwanamke asiye safi kwa sababu ya hedhi,+ mwanamume au mwanamke yeyote anayetokwa na umajimaji mwilini,+ na mwanamume anayelala na mwanamke asiye safi.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “mwili wake.”