Mambo ya Walawi 16:1-34

  • Siku ya Kufunika Dhambi (1-34)

16  Yehova akazungumza na Musa baada ya wana wawili wa Haruni kufa kwa sababu ya kumkaribia Yehova.+  Yehova akamwambia Musa: “Mwambie Haruni ndugu yako asiingie mahali patakatifu+ nyuma ya pazia+ mbele ya kifuniko cha sanduku la agano wakati wowote tu, asije akafa,+ kwa sababu nitatokea katika wingu juu ya kifuniko hicho.+  “Hivi ndivyo vitu ambavyo Haruni anapaswa kuleta anapoingia mahali patakatifu: ng’ombe dume mchanga kwa ajili ya dhabihu ya dhambi+ na kondoo dume kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.+  Anapaswa kuvaa kanzu takatifu ya kitani,+ na suruali fupi*+ ya kitani inapaswa kufunika mwili wake,* na anapaswa kujifunga ukumbuu wa kitani+ na kuvaa kilemba cha kitani+ kichwani. Ni mavazi matakatifu.+ Ataoga kwenye maji+ na kuyavaa.  “Anapaswa kuchukua kutoka kwa Waisraeli+ wanambuzi dume wawili kwa ajili ya dhabihu ya dhambi na kondoo dume mmoja kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.  “Kisha Haruni atamtoa yule ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe, naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe+ na za nyumba yake.  “Halafu atachukua wale mbuzi wawili na kuwapeleka mbele za Yehova kwenye mlango wa hema la mkutano.  Haruni atapiga kura kwa ajili ya mbuzi hao wawili, kura moja ya Yehova na nyingine ya Azazeli.*  Haruni atamchukua yule mbuzi aliyechaguliwa kwa kura+ kuwa wa Yehova na kutoa dhabihu ya dhambi. 10  Lakini yule mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa Azazeli anapaswa kupelekwa akiwa hai mbele za Yehova ili dhabihu ya kufunika dhambi itolewe juu yake, kusudi aachiliwe aende zake nyikani+ akiwa wa Azazeli. 11  “Haruni atamtoa yule ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi, ambaye anatolewa kwa ajili yake mwenyewe, na kutoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe na za nyumba yake; kisha atamchinja ng’ombe dume huyo wa dhabihu ya dhambi, anayetolewa kwa ajili yake mwenyewe.+ 12  “Halafu atachukua chetezo+ kilichojaa makaa ya moto kutoka katika madhabahu+ mbele za Yehova na mikono miwili iliyojaa uvumba bora uliotiwa manukato,+ naye ataleta vitu hivyo nyuma ya pazia.+ 13  Pia atatia uvumba huo juu ya moto mbele za Yehova,+ na moshi wa uvumba huo utafunika kifuniko cha sanduku la agano,+ kilicho juu ya ule Ushahidi,+ asije akafa. 14  “Atachukua kiasi fulani cha damu ya ng’ombe dume+ na kuinyunyiza kwa kidole chake mbele ya kifuniko upande wa mashariki, atanyunyiza kiasi fulani cha damu hiyo mara saba mbele ya kifuniko hicho.+ 15  “Kisha atamchinja yule mbuzi wa dhabihu ya dhambi kwa ajili ya watu+ na kuleta damu yake nyuma ya pazia,+ atafanya kama alivyofanya na damu+ ya yule ng’ombe dume; atainyunyiza kuelekea hicho kifuniko na mbele ya hicho kifuniko. 16  “Ni lazima atoe dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya uchafu, makosa, na dhambi za Waisraeli,+ na hivyo ndivyo anavyopaswa kufanya kwa ajili ya hema la mkutano ambalo liko miongoni mwao katikati ya uchafu wao. 17  “Hakuna mtu mwingine yeyote anayepaswa kuwa ndani ya hema la mkutano kuanzia wakati Haruni anapoingia mahali patakatifu kutoa dhabihu ya kufunika dhambi, mpaka anapotoka nje. Atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe na za nyumba yake+ na za kusanyiko lote la Waisraeli.+ 18  “Kisha atatoka nje na kwenda kwenye madhabahu+ iliyo mbele za Yehova, naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya madhabahu hiyo, kisha atachukua kiasi fulani cha damu ya yule ng’ombe dume na kiasi fulani cha damu ya yule mbuzi na kupaka pembe za madhabahu pande zote. 19  Pia atainyunyizia madhabahu kiasi fulani cha damu hiyo mara saba kwa kidole chake na kuisafisha na kuitakasa kwa sababu ya uchafu wa Waisraeli. 20  “Baada ya kutoa dhabihu ya kufunika dhambi+ kwa ajili ya mahali patakatifu, hema la mkutano, na madhabahu,+ atamtoa pia yule mbuzi aliye hai.+ 21  Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi huyo aliye hai na kuungama juu yake makosa yote ya Waisraeli na maovu yao yote na dhambi zao zote, ataziweka juu ya kichwa cha mbuzi+ huyo na kumwagiza mtu aliyechaguliwa* ampeleke mbuzi huyo nyikani. 22  Mbuzi huyo atazibeba dhambi zao zote+ na kuzipeleka jangwani,+ mtu huyo atampeleka mbuzi huyo na kumwacha aende zake nyikani.+ 23  “Kisha Haruni ataingia katika hema la mkutano na kuyavua yale mavazi ya kitani aliyovaa alipoingia mahali patakatifu, naye atayaweka chini humo. 24  Ni lazima aoge mwili wake kwa maji+ mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake;+ kisha atatoka nje na kutoa dhabihu yake ya kuteketezwa+ na dhabihu ya watu ya kuteketezwa;+ atatoa dhabihu ya kufunika dhambi zake mwenyewe na za watu wote.+ 25  Atayateketeza mafuta ya dhabihu ya dhambi ili yafuke moshi kwenye madhabahu. 26  “Yule mtu aliyempeleka mbuzi wa Azazeli+ anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, kisha anaweza kurudi kambini. 27  “Yule ng’ombe dume wa dhabihu ya dhambi na yule mbuzi wa dhabihu ya dhambi, ambao damu yao ililetwa mahali patakatifu ili itumiwe kufunika dhambi, watapelekwa nje ya kambi, na ngozi zao na nyama yao na mavi yao vitateketezwa motoni.+ 28  Mtu atakayeteketeza vitu hivyo anapaswa kufua mavazi yake na kuoga kwenye maji, kisha anaweza kurudi kambini. 29  “Ifuatayo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu: Katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi huo, mnapaswa kujitesa,* hampaswi kufanya kazi yoyote,+ awe ni mwenyeji au mgeni anayeishi miongoni mwenu. 30  Siku hiyo dhabihu ya kufunika dhambi+ itatolewa kwa ajili yenu ili mtangazwe kuwa safi. Mtasafishwa dhambi zenu zote mbele za Yehova.+ 31  Ni sabato ya pumziko kamili kwenu, mnapaswa kujitesa.*+ Ni sheria ya kudumu. 32  “Kuhani atakayetiwa mafuta+ na kuwekwa rasmi*+ ili atumike akiwa kuhani baada ya baba yake,+ atatoa dhabihu ya kufunika dhambi na kuvaa yale mavazi matakatifu+ ya kitani.+ 33  Atatoa dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya mahali patakatifu,+ hema la mkutano,+ na madhabahu;+ naye atatoa dhabihu ya kufunika dhambi za makuhani na za watu wote.+ 34  Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu+ ili dhabihu ya kufunika dhambi itolewe kwa ajili ya Waisraeli ili kufunika dhambi zao zote mara moja kila mwaka.”+ Basi Haruni akafanya kama Yehova alivyomwamuru Musa.

Maelezo ya Chini

Au “suruali ya ndani.”
Au “uchi wake.”
Huenda neno hili linamaanisha “Mbuzi Anayetoweka.”
Au “aliye tayari.”
Kwa ujumla inaeleweka kwamba “kujitesa” kunamaanisha kujinyima kwa njia mbalimbali, kutia ndani kufunga.
Au “kuitesa nafsi yenu.”
Tnn., “ambaye mkono wake utajazwa.”